Libya: Arrests made in deadly consulate attack

Hivi hao katika mji wa Benghazi wametokea wapi!!!!!??? na ndio kilikuwa kitovu cha ukombozi!???

Simple you invade other countries using rebels, you arm them to help you mission then you insult them they come after you..
 
Hawa wanaoonekana katika hii video wajitayarishe kwa vifo vya drones.

 
Last edited by a moderator:
The cure is worse than the disease.
Sptember 11 attack killed 3000.
War on the so called terrorism killed millions,and is manufacturing more terrorists and create more hate towards west.
hapa ndipo wengi wetu hatupatazami kwa sababu wengi wetu tunasema "MAISHA BORA YAKO WEST" waliojenga maendeleo yale wangefufuka leo!! au waliopigania uhuru wangefufuka leo huh!
 
America and Libya give completely different versions of Benghazi consulate attack

One week after an assault in Benghazi left an US ambassador and three fellow Americans dead, conflicting reports into the details surrounding their passing from both the White House and Libyan officials leave the facts of the raid uncertain.

Zaidi hapa link utata
 
[h=2]American ambassador's car attacked in China[/h]­Anti-Japanese demonstrators in China attacked the car of the US ambassador to the country. The diplomat is unhurt, though the car has been slightly damaged. Over 50 Chinese activists protesting against Japanese claims over the Diaoyu Islands - known in Japan as the Senkaku Islands – took part in the incident. The American embassy has already demanded that the Chinese Foreign Ministry ensure the security of US diplomats and assets in China. Anti-Chinese protests continue in over 100 Chinese cities. All Japanese enterprises in China are closed. Observers have noticed before that since the US is regarded as close ally of Japan, Chinese protesters might turn their rage on American citizens, too.

link vituko
 
Vumbi la filamu halijatulia, Ufaransa waanzisha lengine. Gazeti lachora cartoons.

France ups embassy security after prophet cartoons

Pata habari hapa cartoons
 
Mwili wa Balozi wa US (Benghazi).Anaonekana mwisho wa video.

 
Last edited by a moderator:
Jambo muhimu kuhusu kichwa ni ya kwamba ni watu wa Beghazi walioandamana kwa wengi kuwafukuza wahalfu walioshambulia ubalozi.
cf
Libyans storm militia building after giant protest in wake of attack on US consulate - The Washington Post

Pro-government demonstrators storm militia compound in eastern Libya - Xinhua | English.news.cn

Libyan demonstrators wreck militia compound in Benghazi

Protesters seek to disband Libya militias - Africa - Al Jazeera English

Naona ni dalili nzuri ya kwamba wananchi wameonyesha kuwa wamechoka na wahalifu wanaojisikia wako huru kutenda wanavyotaka wakishika silaha. Wananchi wameamua kutetea mapindizi yao.
 
Bengazi ni ubalozi mdogo wa Marekani (consular office). Ni kawaida ya kwamba nchi inaweza kuwa na ofisi ndogo kando la ubalozi katika nchi fulani.
Mbaöozi marehemu alikuwa Benghazi akitembela ofisi ndogo.

Mwandishi wa makala hapingi mambo ya consular office lakini alipotembelea webpage ya Hillary (US department) hiyo ofisi ya Banghazi haipo kwenye orodha.
 
Hawa walibya siwahurumii hata kidogo wacha wauwane mpaka waishe wote,mchezea zuri baya liko karibu'na hii iwe fundisho kwa nchi kama yetu kutwa watu wanaichokoa amani iliyopo,

Amani ikishatoweka ni ndoto kurudi,nimeishi middle east na mpaka sasa naishi middle east, nchi za UAE na Qatar ndio nchi zinazoongoza kwa kuwa na vijana wengi wanaokwenda kutafuta maisha kutoka africa asia na hata europe, wakati wa gadafi nikikuambia nitafutie mlibya katika nchi hizi hutampata labda business man'kwa sababu kwao walikuwa na goo time,
Leo hii tembelea miji ya dubai,doha utakutana na rundo la vijana wakilibya wanatafuta kazi?
Walishindwa kujifunza kwa wa iraq baada ya wao nao kuaminishwa kuwa saddam ndio adui wa maisha yao na maendeleo yao leo kiko wapi saddam hayupo lakini iraq sio salama hata kidogo'
Hata kama hao walibya wakiwaondoa answar bado nchi haiko salama amani wameshaweka rehani na kuikomboa ni ndoto za mchana,
Hili liwe funzo kwa wa tz kuchezea amani ni kosa kubwa sana
 
Mwandishi wa makala hapingi mambo ya consular office lakini alipotembelea webpage ya Hillary (US department) hiyo ofisi ya Banghazi haipo kwenye orodha.
Sindiyo, kama nimeelewa vema kutokana na tovuti ya ubalozi mjini Tripoli huyu mbalozi alikwenda Benghazi kwa kufungua rasmi ofisi ndogo.
 
... hii iwe fundisho kwa nchi kama yetu kutwa watu wanaichokoa amani iliyopo,

.. mpaka sasa naishi middle east, nchi za UAE na Qatar ndio nchi zinazoongoza kwa kuwa na vijana wengi wanaokwenda kutafuta maisha kutoka africa asia na hata europe, wakati wa gadafi nikikuambia nitafutie mlibya katika nchi hizi hutampata labda business man'kwa sababu kwao walikuwa na goo time,
Leo hii tembelea miji ya dubai,doha utakutana na rundo la vijana wakilibya wanatafuta kazi?

Mpendwa, nakubali kabisa ni vema kutafakari kabla ya kupindua utaratibu kama tunataka kweli yale yanayofuata na tukibomoa utaratibu - je kuna mpango wa baadaye?

Ila tu picha yako ya Paradiso Libia chini ya Gadafi inaoekana ni tofauti na Walibia wengi. Ajabu? Nchi ilijaa watu maskini kutoka nchi za Afrika (waliokuwa na maisha mabaya) ilhali asilimia ya vijana wake wenyewe walijaribu kwenda nje.
Kufuatana na factsheet ya world bank http://siteresources.worldbank.org/INTPROSPECTS/Resources/334934-1199807908806/Libya.pdf kabla ya mapinduzi walikuwa Walibia 110,000 walioondoka nchini mwaka 2010. Hawakuenda UAE bali nchi nyingine zinazotajwa.

Je umeshauliza kama labda wakati wa Gadafi serikali ya UAE haikutaka Walibia kutokana na uhusiano mbaya kati ya Gadafi na Waarabu wengine?
Ilhali sasa mlango umefunguliwa ?
 
Mpendwa, nakubali kabisa ni vema kutafakari kabla ya kupindua utaratibu kama tunataka kweli yale yanayofuata na tukibomoa utaratibu - je kuna mpango wa baadaye?

Ila tu picha yako ya Paradiso Libia chini ya Gadafi inaoekana ni tofauti na Walibia wengi. Ajabu? Nchi ilijaa watu maskini kutoka nchi za Afrika (waliokuwa na maisha mabaya) ilhali asilimia ya vijana wake wenyewe walijaribu kwenda nje.
Kufuatana na factsheet ya world bank http://siteresources.worldbank.org/INTPROSPECTS/Resources/334934-1199807908806/Libya.pdf kabla ya mapinduzi walikuwa Walibia 110,000 walioondoka nchini mwaka 2010. Hawakuenda UAE bali nchi nyingine zinazotajwa.

Je umeshauliza kama labda wakati wa Gadafi serikali ya UAE haikutaka Walibia kutokana na uhusiano mbaya kati ya Gadafi na Waarabu wengine?
Ilhali sasa mlango umefunguliwa ?

Hapana mkuu nchi ya UAE imekuwa haifungamani na siasa za nchi nyingine kabisa iko huru sana kwa mtu yeyote kuingia, si kama Qatar ilivyo, nina rafiki yangu mlibya yeye siku nyingi anaishi Dubai na anafanya business zake hapa?mara nyingi namuuuliza maswali kama hayo, jambo moja mara nyingi huwa ananiambia kosa la gaddafi lilikuwa kulewa madaraka na hasira zaidi za walibya zilikuwa kwa gadaffi kuwaandalia mrithi wakati nchi ina wasomi wakutosha,

Pia nina rafiki yangu kutoka iraq yeye ni mtu mzima sana anajua mambo mengi sana nakumbuka mara nyingi ananiambia hakika saddam alikuwa ni mzalendo wakweli kwa nchi yake alikuwa anaipenda toka moyoni,ananiambia wairaq walikuwa wanaheshimiwa sana duniani wakati wa yule mzee lakini sio sasa ananiambia kwa sasa iraq haina usalama kabisa mpaka yeye na family yake yote wamehamia UAE japo anajisikia tabu kuishi nje ya kwao lakini anasema hana jinsi
 
Mpendwa, nakubali kabisa ni vema kutafakari kabla ya kupindua utaratibu kama tunataka kweli yale yanayofuata na tukibomoa utaratibu - je kuna mpango wa baadaye?

Ila tu picha yako ya Paradiso Libia chini ya Gadafi inaoekana ni tofauti na Walibia wengi. Ajabu? ....
Ilhali sasa mlango umefunguliwa ?

Walibya ingekuwa kuna second chance,wangesema Gaddafi arudi na awe kiongozi wa maisha.
Libya ilifata mfumo wa serikali,siasa ambao wengi wetu hatuujui.

Libya mbali na vikwazo na vitimbi walivyofanyiwa na US na West bado ilikuwa ni Uswisi ya Afrika na huduma za kijamii ambazo walibya walipata hata nchi za ulaya na US kwao ni ndoto, au wangesema haiwezekani kuwapatia huduma hizo wananchi bure.

Sasa nchi haikaliki tena,kwa hiyo kweli kama usemavyo, mlango umefunguliwa.

Pitia hizi huenda ukaambulia "big picture" link Hugh Roberts · Who said Gaddafi had to go? · LRB 17 November 2011

link Destroying a Country's Standard of Living: What Libya Had Achieved, What has been Destroyed | Global Research

link GADDAFI'S LIBYA THREATENED AFRICA'S SUBORDINATE ROLE « Libya 360°

link maishamazuri
 
Ila tu picha yako ya Paradiso Libia chini ya Gadafi inaoekana ni tofauti na Walibia wengi. Ajabu? Nchi ilijaa watu maskini kutoka nchi za Afrika (waliokuwa na maisha mabaya) ilhali asilimia ya vijana wake wenyewe walijaribu kwenda nje.
Kufuatana na factsheet ya world bank http://siteresources.worldbank.org/INTPROSPECTS/Resources/334934-1199807908806/Libya.pdf kabla ya mapinduzi walikuwa Walibia 110,000 walioondoka nchini mwaka 2010.

Sasa leo wangapi wamerudi kufurahia Libya mpya? Una twakimu mpya?

Au wameongezeka kuikimbia nchi?

Link Did Libya
 
Sasa leo wangapi wamerudi kufurahia Libya mpya? Una twakimu mpya?

Au wameongezeka kuikimbia nchi?

Link Did Libya
Sina takwimu juu ya hilo (na katika hali jinsi walivyo nina wasiwasi ya kwamba wanaweza kupata namba halisi sasa).

Nadhani tuko pamoja ya kwamba vita ya wenyewe kwa wenyewe ni jambo baya sana ni mara chache tu ya kwamba matokeo yanaleta nafuu kweli .....
Syria ni mfano mbele ya macho yangu - yaani pamoja na ukorofi wote wa serikali iliyopo hii vita ni vibaya zaidi.

Ila tu napendelea kurudi kwenye mada yenyewe. Je huoni hatua zinazochukuliwa sasa dhidi ya wanamigambo (wengiwao wa mwelekeo wa kijihadi) ni dalili zuri za kurudisha kiwangocha amani na usalama nchini Libia?
 
Back
Top Bottom