Ila tu napendelea kurudi kwenye mada yenyewe. Je huoni hatua zinazochukuliwa sasa dhidi ya wanamigambo (wengiwao wa mwelekeo wa kijihadi) ni dalili zuri za kurudisha kiwangocha amani na usalama nchini Libia?
Watawaua hao wa mwelekeo wa jihadi wote?
Wajihadi hao wanaweza kujificha kwa muda halafu tifu litaibuka upya.
Itazame Iraq, Afghanistan, Yemen, Somalia, Congo utaelewa mziki wa Libya utachezwa kwa miaka kadhaa.
Elewa kuwa Uongozi wa sasa hauungwi mkono na wengi, na uongozi huo umefanya kosa kuwatenga waliokuwa wapenzi na washabiki wa Gaddafi katika siasa za kuongoza nchi na kuleta mshikamano wa kitaifa.