Library au huduma za kipesa kama Tigo Pesa

flulanga

JF-Expert Member
Jul 1, 2016
4,861
6,342
Habarini ndugu zangu,

Mimi nina goli la huduma za kipesa kama M-Pesa, Tigo na Airtel Money. Hapo awali nilikuwa kwa mwezi naingiza sio chini ya laki 5 ila kwa sasa biashara sio nzuri nimeshuka hadi laki 4 mpaka 380.

Na yote hii imechangiwa na kuongezeka kwa watoa huduma kama yangu hapa jirani maana kwa haraka haraka nimepata majirani sio chini ya watano ndani ya muda mfupi.

Sasa ninachokiona kwa kipato hiki nisipojiongeza nitachelewa sana kufikia malengo yangu.

Kwa hiyo sasa najiuliza nifungue goli jingine kama hili au nifungue library (kuuza CD na kuingiza nyimbo na movie kwenye flash).

Hii biashara sina uzoefu nayo na wala sina mtu ninayemfahamu anafanya hii biashara zaidi huwa nawaonaga tu.

Mtaji wangu nilionao wa kuanzia ni shilingi Milion 1 ila uwezekano wakuongeza japo kidogo upo.

Ninaomba wenye uzoefu wa hii biashara ya library watiririke ili nipime kati ya hii nayoifanya maana hii nayoifanya nina uzoefu nayo kwa asilimia kubwa maana ndio biashara yangu ya kwanza katika maisha yangu.

Karibuni




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama una eneo la kutosha na mazingira ni rafiki kwa biashara ya library nakushauri fungua tu hiyo library ila ongezea na Kompyuta yako moja kwa ajili ya nyimbo na kuwakopia hizo muvi kwenye flash, Kwa Bajeti ya laki 5 unapata desktop nzuri tu yenye hard disk kubwa za kuhifadhia nyimbo, video, muvi na Sezoni. laki 5 iliyobakia unapata Sezoni, muvi single au bongo muvi za kutosha sana bila kusahau matengenezo ya shelfu za kuwekea CD

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eb na mimi nipate ujuzi hapa, mlio na uzoefu wa haya mambo mtujuze, pia mwenye uzoefu na salon pia naomba maelezo, vitu gani ni muhimu pia niandae mtaji kiasi gani?
 
Library ni nzuri kikubwa ni location na upatikanaji wa CD.
(nilishafungua hii biashara japo niliyemuachia akaniulia biashara).
Kama sehemu iko poa weka hapo hapo hyo libary pia usisahau gadget za simu kama screen protector,cover,usb cable, charger,memory card, card reader na flash kama unaweza.
Kila la kheri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upoo maeneoo ganii mkuu kabla sijakushaurii maana biashara ya library Nina miaka mitatu sasa nafanya hii biashara

Sent using Jamii Forums mobile app
tupe habari zaidi
mtaji wake ulianza na kiasi gani, lakini pia wastani wa mapato huingiza shilingi ngapi kwa siku

muundo wa uendeshaji uko vipi, yaani unaajiri kijana wa kazi au unafanya mwenyewe
kama unaajiri malipo kwa uliyemwajiri ni kiasi gani
 
Ukitaka kufanikiwa, usifanye biashara iliyo kinyume na sheria! Ukija kufanikiwa mbeleni ukawa mtu mkubwa, inaweza kukusumbua kimahakama au walau ki majuto nafsini. Kumbuka KUNAKILI FILAMU, MIZIKI, VIDEO n.k na kuuza si biashara halali. Itakuwa halali tu pale una mkataba na mwenye hati miliki ya hizo content nawe uwe unamlipa. Bahati mbaya hakuna anayefuatilia, ila kila unayemwona na pc anauza nyimbo, alitakiwa awe jela. Filamu hasa ni shida, walau muziki game imechange kwa sasa wanatoa nyimbo bure (Youtube huko) ili wajulikane, walipwe kwa views au wapate shows, ila kuuza kwa flash/cd kienyeji bado si biashara halali.
 
UNA MTAJI MKUBWA SANA MKUU,
UKIFANYA MAMBO KWA UTULIVU NA KUIPA NAFASI AKILI-
UTAFANIKIWA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Milioni 1 kwa library siyo mtaji mkubwa. Na hapo ni hata kama tayari ana fremu.

Nimekua katika hii ishu tangu enzi hizo Kikosi cha Mizinga wanazunguka kukamata watu wanaoburn CD.

Mleta uzi, kutegemea na eneo utakalofungua library unakua na uwezo wa kuingiza kuanzia 15K mpaka 40K kwa siku.

Kwa library kinachofanya pesa uione ni kua na movies zote ambazo rivals wako hawana. Kingine ni bei, mfano Komakoma ili DVD mtu iwe yake ni 2000 na kukodi ni 1500 au 1500 kwa 1000, wakati Msisiri ili DVD iwe yako ni 1000 na kukodi ni 500.

Unachohitaji ni PC yenye uwezo, nahisi Core I3 yenye processor na ram kubwa ni dawa kwa hapa. Na unahitaji hard drive (external na internal) kubwa nafikiri ukiwa na Terabyte 3 utakua umejiweka sehemu salama kwa kuanzia. PC iwe na milango 2 ili uweze kudeal na mtu zaidi ya mmoja.

Sehemu utakayofungua pia inamatter. Kibaha wimbo mmoja kwenye flash ni 500 muvi CD ni 2000, too bad sikukaa muda mrefu as nilienda kumuelekeza jamaa ishu fulani hivi.

So location, bei na movies ndiyo guide yako katika hii ishu.
 
apakati,
Hizi hoja ndiyo zilitumiwa na Siro na Makonda katika kunyang'anya computer na vifaa vingine watu wa library.
 
Castr, Mkuu kutokana namaelezo uliyoyatoa hasa upande pc yenye uwezo mkubwa, nahiyo hard drive external na internal nahiyo pc yenye milango miwili inanibidi niandae kiasi gani? Ubarikiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kutokana namaelezo uliyoyatoa hasa upande pc yenye uwezo mkubwa, nahiyo hard drive external na internal nahiyo pc yenye milango miwili inanibidi niandae kiasi gani? Ubarikiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
PC za kusimama (Tower) zile unaweza kuziongezea mlango so siyo kwamba utaikuta dukani ina milango 2 tayari. Mlango ni 25, kwahiyo ukishanunua PC unanunua na mlango mwingine unainstall.

Dukani unaweza nunua CPU yenye uwezo wa kuanzia Core i3 peke yake kwa pesa isiyozidi 250 (ndiyo maana naprefer kununua mkononi) so screen, mouse, keyboard utatafuta kivyake. Wakati mkononi utakuta mashine ina uwezo huo ikiwa full unainunua kwa 280 - 320.

Pia hard drive za 1TB dukani ni kuanzia 130 wakati mkononi na unaweza ikuta na vitu ni 70 mpaka 90. Najaribu kukumbuka 3TB ya ndani nilinunua shilingi ngapi nakwama, ila nafikiri kwenye 190.
 
Back
Top Bottom