Let's share: Uliwahi kusaidiwa na mtu usiyemfahamu kabla (msamaria mwema)? Kipi kilitokea?

Nakumbuka wakati nipo kidato cha nne nilikuwa suspended shuleni nikatakiwa kurudi nyumbani na kuleta mzazi wangu. Tulikuwa wawili na mwenzangu. Basi tukasafiri hadi iringa mjini. Tulipanga kupeleka mzazi bandia shuleni. Tulipofika mjini mwenzangu akaniambia wacha tulale hapa mjini kesho tutajua cha kufanya.

Basi tukaenda kwny nyumba moja (mwenzangu alikuwa mwenyeji maana walikuwa wanaishi hapo iringa mjini mie natokea Dar) tukaingia geto. Kumbe ni kwa boyfriend wake mi sina habar nikajua ndio nyumbani.

Ilipofika mida ya saa mbili usiku wakaja wakaka wawili, nikatambulishwa huyu ni shemeji yako na huyu rafiki yake! Tukaenda mgahawani kula baadae tukarudi pale geto. Kumbe bwana watu wana mipango yao mie sina hili wala lile, story story badae mwenzangu akaniita nje, ananiambia mie nalala hapa wewe ukatafute pa kulala, lol!

Nilidata kabisa duh, usiku huu mi naenda wapi jamani, akaniambia kama vp kalale kwa yule (yule rafiki sasa) nikasema hapana ntaenda kulala stendi. Nikaingia ndani nikachukua kibegi changu nikaaga huyo nikatoka, ilikuwa kama saa nne hv usiku.

Nikaanza kutembea sijui naenda wapi, nikawaza pa kwenda, hela sina zaidi ya nauli ya kurudia shuleni, nikaanza kulia njiani huku natembea. Kumbe yule kaka (rafiki) hakupenda nilichofanyiwa akawa ananifuata nyuma mie sijui. Nikatembea kufika barabarani nikaa pembeni sielewi cha kufanya. Akatokea yule kaka akaniuliza kwani yule sio rafiki yako? Nikamwambia nimwanafunzi mwenzangu tunasoma darasa moja. Akashangaa, sasa mbona hauko shule? Nikamweleza ukweli kama nimefukuzwa shule natakiwa nipeleke mzazi kwa sababu tulifanya mgomo shuleni.

Akaniuliza shule gani nasoma na kwa nini nisiende nyumbani sasa. Nikamwambia siwez kwenda nyumbani mama yangu atanikata masikio akijua nimefukuzwa shule. Akaniuliza sasa utafanyaje, nikamwambia itabidi nitafute mzazi bandia ndo niende nae. Yule kaka akaniambia nyanyuka twende mi nitakusaidia. Nikanyanyuka tukaenda hadi nyumbani kwake (chumba kimoja). Akanionesha choo nikaoge nikakataa, nilikuwa naogopa na natetemeka kama nimeshikwa na homa. Akaniambia usiogope mi sitakufanya chochote, kuwa na amani panda kitandani ulale. Duh!

Nikamuuliza wewe unalala wapi akasema ntalala chini,wee moyo unadunda hatari. Akasema niamini kweli sitakufanya chochote we lala tu kesho nitakusaidia kutafuta mama akupeleke shule. Nikapanda kitandani na jinsi,viatu, na kibegi changu mgongoni. Akanipa shuka jifunike baridi. Nikalala kwani usingizi ulikuja?? Yule kaka akalala chini,katandika shuka akaweka manguo kichwani kama mto akalala. Nikakaa nawaza mpaka nikapitiwa na usingizi. Kushtuka asbh yule kaka hayupo. Nikaa kitandani siamini kama nimelala salama salimini.

Kidogo akarudi akaniuliza umelala salama? Umejikagua uko salama? Ulikuwa unaogopa nini sasa? Nikatoa tabasam feki pale, nikamwambia asante kwa kunihifadhi. Akaniambia nenda kaoge nikupeleke ujanywe chai. Nikasema nataka nitafute mama wa kwenda nae shule kwanza akasema usijali si nimekwambia ntakusaidia? Basi nikaenda chooni kuoga nilipomaliza tukatoka nje, akanipeleka kwny stend ya kalenga kuna mama ntilie kibao, tukaingia kibanda kimoja cha mama wa kichaga kumbe alishaongea nae akamweleza shida yangu yule mama akakubali. Tumekunywa chai akanitambulisha kwa yule mama, kwamba ndo atanisaidia kwenda shule kama mzazi wangu, duh! Nimampanga yule mama vya kwenda kuongea shuleni akakubali. Akafunga biashara yake kaenda kujiandaa hao tukaenda stendi kuu kupanda gari za shuleni. Yule kaka alinipa na nauli yangu na ya yule mama aisee.

Nilimshukuru sana sana na kumuomba msamaha nilimfikiria vibaya usiku. Akaniambia kuwa na amani bado wanaume wastaarabu tupo. Nikarudi shuleni. Sikumtafuta tena yule kaka na sijui kama yuko tena, ila kati ya watu muhimu walionishika mkono kwny maisha yangu na yeye alikuwepo japo hata sikufanikiwa kumjua jina lake.

It is well with my Soul!
 
Ilikuwa mtihani wangu wa form 4 miaka kadhaa ilopita, sikuwa nimemaliza ada, bro alinipa cheki hewa ili kusogeza siku nikawapelekea,jamaa walipoenda hawajakuta kit, wakarudi kwa speed ya 5g, nikatolewa kwenye chumba cha mtihani ilikuwa civis national na kumbuka, hivo nikamis mtihani, nikiww nimechukia na nimekata tamaa, nimejifungia chumbani nalia vibaya, nlikuja kuitwa kwamba kuna mtuananihitaji, naakajitambulisha jina, then akaniambia why nalia, nikamwambia nimefukuzwa kufanya necta sijalipa ada, jamaa akanichukua hadi shule na kwenda kuclear deninikaendelea na mitiahani. Ikabidi nimtafute jamaa sehem alonielekeza ofisi za nssf, ambako nlikuwa naenda kuchukua helaya matumizi, sijamkuta, nikauliza kwa jamaa alokuwa ananipa hela ya matumizi akaniambia hamjui na sio mfanyakazi wa pale. Nikahesabu ni muujiza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka wakati nipo kidato cha nne nilikuwa suspended shuleni nikatakiwa kurudi nyumbani na kuleta mzazi wangu. Tulikuwa wawili na mwenzangu. Basi tukasafiri hadi iringa mjini. Tulipanga kupeleka mzazi bandia shuleni. Tulipofika mjini mwenzangu akaniambia wacha tulale hapa mjini kesho tutajua cha kufanya.

Basi tukaenda kwny nyumba moja (mwenzangu alikuwa mwenyeji maana walikuwa wanaishi hapo iringa mjini mie natokea Dar) tukaingia geto. Kumbe ni kwa boyfriend wake mi sina habar nikajua ndio nyumbani.

Ilipofika mida ya saa mbili usiku wakaja wakaka wawili, nikatambulishwa huyu ni shemeji yako na huyu rafiki yake! Tukaenda mgahawani kula baadae tukarudi pale geto. Kumbe bwana watu wana mipango yao mie sina hili wala lile, story story badae mwenzangu akaniita nje, ananiambia mie nalala hapa wewe ukatafute pa kulala, lol!

Nilidata kabisa duh, usiku huu mi naenda wapi jamani, akaniambia kama vp kalale kwa yule (yule rafiki sasa) nikasema hapana ntaenda kulala stendi. Nikaingia ndani nikachukua kibegi changu nikaaga huyo nikatoka, ilikuwa kama saa nne hv usiku.

Nikaanza kutembea sijui naenda wapi, nikawaza pa kwenda, hela sina zaidi ya nauli ya kurudia shuleni, nikaanza kulia njiani huku natembea. Kumbe yule kaka (rafiki) hakupenda nilichofanyiwa akawa ananifuata nyuma mie sijui. Nikatembea kufika barabarani nikaa pembeni sielewi cha kufanya. Akatokea yule kaka akaniuliza kwani yule sio rafiki yako? Nikamwambia nimwanafunzi mwenzangu tunasoma darasa moja. Akashangaa, sasa mbona hauko shule? Nikamweleza ukweli kama nimefukuzwa shule natakiwa nipeleke mzazi kwa sababu tulifanya mgomo shuleni.

Akaniuliza shule gani nasoma na kwa nini nisiende nyumbani sasa. Nikamwambia siwez kwenda nyumbani mama yangu atanikata masikio akijua nimefukuzwa shule. Akaniuliza sasa utafanyaje, nikamwambia itabidi nitafute mzazi bandia ndo niende nae. Yule kaka akaniambia nyanyuka twende mi nitakusaidia. Nikanyanyuka tukaenda hadi nyumbani kwake (chumba kimoja). Akanionesha choo nikaoge nikakataa, nilikuwa naogopa na natetemeka kama nimeshikwa na homa. Akaniambia usiogope mi sitakufanya chochote, kuwa na amani panda kitandani ulale. Duh!

Nikamuuliza wewe unalala wapi akasema ntalala chini,wee moyo unadunda hatari. Akasema niamini kweli sitakufanya chochote we lala tu kesho nitakusaidia kutafuta mama akupeleke shule. Nikapanda kitandani na jinsi,viatu, na kibegi changu mgongoni. Akanipa shuka jifunike baridi. Nikalala kwani usingizi ulikuja?? Yule kaka akalala chini,katandika shuka akaweka manguo kichwani kama mto akalala. Nikakaa nawaza mpaka nikapitiwa na usingizi. Kushtuka asbh yule kaka hayupo. Nikaa kitandani siamini kama nimelala salama salimini.

Kidogo akarudi akaniuliza umelala salama? Umejikagua uko salama? Ulikuwa unaogopa nini sasa? Nikatoa tabasam feki pale, nikamwambia asante kwa kunihifadhi. Akaniambia nenda kaoge nikupeleke ujanywe chai. Nikasema nataka nitafute mama wa kwenda nae shule kwanza akasema usijali si nimekwambia ntakusaidia? Basi nikaenda chooni kuoga nilipomaliza tukatoka nje, akanipeleka kwny stend ya kalenga kuna mama ntilie kibao, tukaingia kibanda kimoja cha mama wa kichaga kumbe alishaongea nae akamweleza shida yangu yule mama akakubali. Tumekunywa chai akanitambulisha kwa yule mama, kwamba ndo atanisaidia kwenda shule kama mzazi wangu, duh! Nimampanga yule mama vya kwenda kuongea shuleni akakubali. Akafunga biashara yake kaenda kujiandaa hao tukaenda stendi kuu kupanda gari za shuleni. Yule kaka alinipa na nauli yangu na ya yule mama aisee.

Nilimshukuru sana sana na kumuomba msamaha nilimfikiria vibaya usiku. Akaniambia kuwa na amani bado wanaume wastaarabu tupo. Nikarudi shuleni. Sikumtafuta tena yule kaka na sijui kama yuko tena, ila kati ya watu muhimu walionishika mkono kwny maisha yangu na yeye alikuwepo japo hata sikufanikiwa kumjua jina lake.

It is well with my Soul!
Mwaka gani hiyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kipindi ndo natoka Mbeya kwa mara ya kwanza kwenda kilosa Boys kuanza advance.sijui hata njia wa A wala B.niliambiwa nishukie Mikumi then nichukue gari za Kilosa.Sasa Kufika stend nlikosindikizwa na dada Gari ikang'oa nanga hadi Stendi ya Nanenane hapo kojo limebana.Nikamwomba konda niende nikojoe fasta.Ile narudi napishana na Gari ndo inang'oa nanga.Ndani kuna facilities zote.ila pesa zilikuwa mfukoni.Ghafla wazo likaja nikabeba bodaboda niifukuzie hadi uyole lakin wapi,naambiwa imepita dakika kama 5 zilopita.Duh!nikabaki nimepanic.Dereva bodaboda akanishauri niende ofisi kuu za Kampuni ilikuwa ni NGANGA.

Basi nikapanda daladala kuelekea stend kuu nikiwa na mawazo tele na hofu kubwa ya kuwa ntawaeleza nini hom.Basi kufika ofisini nikaambiwa msaada pekee ni eidha nisafiri tena kesho,au nipande Nganga ya kuelekea Iringa inatoka saa 3.Basi mi nikachukulia rahisi.nikakubali saa 3 ikatoka stendi kuu.saa 8 mchna tupo makambako.saa 10 nikashushwa pale stendi fulani jina limenitoka lakin kabla hujaanza kupanda Iringa.

Basi nikafaulishwa na mshikaji mmoja aliyeachiwa jukumu hilo,wengi walikataa ila tukafanikiwa kwenye tank za kubeba mafuta.Ilikuwa inakimbi balaa.na tulikuwa na jamaa wengine nao walipandia Ilula.Basi saa 2.00 usiku nikashushwa mikumi na kumbe kuna jamaa pia alikuwa anashuka pale.Akafika akapanda Bodaboda akaenda zake Gueast fulani.Mi nikaenda nikaambiwa vyumba vimeisha.Nikaanza kuzurura tu.Baadae nikafanikiwa kukutana na washkaji ambao walimwita jamaa wa pikipiki akanipeleka Guest fulan na.kweli nikapata chumba ilikuwa 5000 tu.Nikalipia nikamwuliza,Nganga ya kutoka Ifakara saa ngapi asubuhi inapita akanambia saa 1 kasoro.Basi mi nikaenda huko nikala nikarudi kulala.kuna.mbu balaa.na net hakuna.

Basi saa 12 na robo niko stendi nasubiri Nganga ya Kutoka Ifakara.Ikafika nikamweleza konda(maana alipewa taarifa zangu)akanielewa na kunikabidhi matranka na begi kubwa.la nguo.

shida ikawa namna ya kwenda kilosa toka mikumi,magari mabovu,barabara mbovu hatari lakin kwa neema nilifika.kilosa jinsi nilivyozea huku mbeya na majina.maarufu kama Mikumi na kilosa kwa kweli sikutegemea hali ya miji jinsi ilivyo hovyo.

Nikafika kuuliza shule hawaijui.Wakanitajia shule za pale lakin wapi.nikawaambia shule ina ghorofa sijui nini hawaijui.mh! wakawa wanasema labda ni "KIZUNGUZI" nikasema sio.Lakin baadae ikathibitika kuwa Kizunguzi ndio jina.maarufu zaidi kwa kilosa.kuna mama mmoja alinisaidia sana.Alinitembeza madukani kununua mashuka,mashati,na godoro na vitu vingine.Alijitambulisha kwa jina.moja la Mama Maulid.Akasema ana mtoto pale kilosa anaitwa maulid.Alinisaidia sana akaita Bodaboda hadi kilosa.Barabara ilikuwa mbovu maana mvua ilinyesha japo ilikuwa mwezi wa 7.Nilimshukuru sana Mama yule,alinipa namba yake japo ilikuja ikapotea. kabla sijaiweka kwene lain..Mungu ambariki Mama huyu popote alipo.Wakazi wa Kilosa ni wakarim sana.Mungu awabariki wakazi wote wa wilaya ya kilosa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ilikua mwaka jana mwanzoni nilipata uhitaji wa haraka haraka sana kifedha, nikahangaika nikapata kiasi fulani, ikabaki shilingi laki mbili nilihangaika sana sana sikufanikiwa nikaamua kupiga magoti kusali wazo likanijia kumpigia dada mmoja tulifahamiana tu kwenye group la maombi huko what'sapp na hatujawahi kuonana kwa sura hata mara moja, nilimweleza shida yangu huwezi amini yule dada aliniuliza tu nikutumie kwa namba yako ya voda au tigo? yani nilitamani kupiga kelele kwa furaha. kweli yule dada alinitumia na hela ya kutolea huwezi amini.

kilichonishangaza hatukuwahi kuonana hata mara moja, hakuniuliza hata maswali ya kuonyesha kunihofia alisema tu nakutumia sasa hivi ukipata utanirudishia..

namshukuru sana Mungu maana kupitia huyu dada alinifichia aibu kubwa sana la sivyo ningefedheheka mimi jamani, basi mwisho wa mwezi ulipofika nilimlipa yule dada hela yake yote, kwa kweli mpaka leo ni wa pekee sana kwangu, kwanza alinisaidia wakati ambao kama mwanadamu nilikua nimeshakata tamaa, zaidi ni kile kitendo cha yeye kuniamini mimi asiye nijua daaaahhh ni jambo kubwa mno kwangu....
 
ilikua mwaka 2002 sitasahau hii siku, ilikua kipindi ambacho tulikua tunakaribia kufunga shule,
sasa siku hiyo nilienda shule kama kawaida maana nilikua napenda sana siku za kufunga shule zilikua na michezo mingi hamna kuingia darasani....

ilipofika saa tano ghafla nilianza kujiskia vibaya mno kizunguzungu,kichwa kilikua kinaniuma sana nikaamua kufunga safari ya kurudi nyumbani.Nilitembea hatua kadhaa tu nikazidiwa nikaanguka chini, nilikua pale chini nisijue nitafikaje nyumbani kwakweli nilikua nawaza leo nafia hapahapa,ilikua saa sita na nusu wanafunzi wenzangu nao walikua wanarudi nyumbani wengi walikua wananipita tu wakihisi nimejipumzisha wala hawakua na muda na mimi,Mungu si athumani akapita classmate mmoja aliponiona alinionea huruma sana maana nilikua katika hali ambayo hata kuongea siwezi,

Basi yule jamaa akanibeba mgongoni nakumbuka nilikua kibonge enzi hizo, hivo jamaa alikua ananibeba hatua kadhaa anapumzika, alijikongoja hivo hivo mpaka tulifika nyumbani kwao...maana nyumbani kwetu ilikua mbali kidogo
tulipofika tuliwakuta wazazi wake wote wakaniogesha kupunguza joto la mwili maana nilikua nimechemka sana...wakanipa na panadol

yule classmate alikua anapajua nyumbani kwetu tulipofika ye alikimbia nyumbani kutoa taarifa, baada ya muda mfupi mama alikuja hapo nilikua nimepata nguvu kidogo, dah mama aliponiona alilia japo sijui alilia nini

nimekumbuka mbali sana kuna watu wana roho nzuri, maana bila huyo comrade leo sidhani kama ningekuwepo.

natafuta namba za huyu comrade sijazipata ila i promice sitosahau wema wako bro and one day i will repay your kindness
daah imenigusa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka wakati nipo kidato cha nne nilikuwa suspended shuleni nikatakiwa kurudi nyumbani na kuleta mzazi wangu. Tulikuwa wawili na mwenzangu. Basi tukasafiri hadi iringa mjini. Tulipanga kupeleka mzazi bandia shuleni. Tulipofika mjini mwenzangu akaniambia wacha tulale hapa mjini kesho tutajua cha kufanya.

Basi tukaenda kwny nyumba moja (mwenzangu alikuwa mwenyeji maana walikuwa wanaishi hapo iringa mjini mie natokea Dar) tukaingia geto. Kumbe ni kwa boyfriend wake mi sina habar nikajua ndio nyumbani.

Ilipofika mida ya saa mbili usiku wakaja wakaka wawili, nikatambulishwa huyu ni shemeji yako na huyu rafiki yake! Tukaenda mgahawani kula baadae tukarudi pale geto. Kumbe bwana watu wana mipango yao mie sina hili wala lile, story story badae mwenzangu akaniita nje, ananiambia mie nalala hapa wewe ukatafute pa kulala, lol!

Nilidata kabisa duh, usiku huu mi naenda wapi jamani, akaniambia kama vp kalale kwa yule (yule rafiki sasa) nikasema hapana ntaenda kulala stendi. Nikaingia ndani nikachukua kibegi changu nikaaga huyo nikatoka, ilikuwa kama saa nne hv usiku.

Nikaanza kutembea sijui naenda wapi, nikawaza pa kwenda, hela sina zaidi ya nauli ya kurudia shuleni, nikaanza kulia njiani huku natembea. Kumbe yule kaka (rafiki) hakupenda nilichofanyiwa akawa ananifuata nyuma mie sijui. Nikatembea kufika barabarani nikaa pembeni sielewi cha kufanya. Akatokea yule kaka akaniuliza kwani yule sio rafiki yako? Nikamwambia nimwanafunzi mwenzangu tunasoma darasa moja. Akashangaa, sasa mbona hauko shule? Nikamweleza ukweli kama nimefukuzwa shule natakiwa nipeleke mzazi kwa sababu tulifanya mgomo shuleni.

Akaniuliza shule gani nasoma na kwa nini nisiende nyumbani sasa. Nikamwambia siwez kwenda nyumbani mama yangu atanikata masikio akijua nimefukuzwa shule. Akaniuliza sasa utafanyaje, nikamwambia itabidi nitafute mzazi bandia ndo niende nae. Yule kaka akaniambia nyanyuka twende mi nitakusaidia. Nikanyanyuka tukaenda hadi nyumbani kwake (chumba kimoja). Akanionesha choo nikaoge nikakataa, nilikuwa naogopa na natetemeka kama nimeshikwa na homa. Akaniambia usiogope mi sitakufanya chochote, kuwa na amani panda kitandani ulale. Duh!

Nikamuuliza wewe unalala wapi akasema ntalala chini,wee moyo unadunda hatari. Akasema niamini kweli sitakufanya chochote we lala tu kesho nitakusaidia kutafuta mama akupeleke shule. Nikapanda kitandani na jinsi,viatu, na kibegi changu mgongoni. Akanipa shuka jifunike baridi. Nikalala kwani usingizi ulikuja?? Yule kaka akalala chini,katandika shuka akaweka manguo kichwani kama mto akalala. Nikakaa nawaza mpaka nikapitiwa na usingizi. Kushtuka asbh yule kaka hayupo. Nikaa kitandani siamini kama nimelala salama salimini.

Kidogo akarudi akaniuliza umelala salama? Umejikagua uko salama? Ulikuwa unaogopa nini sasa? Nikatoa tabasam feki pale, nikamwambia asante kwa kunihifadhi. Akaniambia nenda kaoge nikupeleke ujanywe chai. Nikasema nataka nitafute mama wa kwenda nae shule kwanza akasema usijali si nimekwambia ntakusaidia? Basi nikaenda chooni kuoga nilipomaliza tukatoka nje, akanipeleka kwny stend ya kalenga kuna mama ntilie kibao, tukaingia kibanda kimoja cha mama wa kichaga kumbe alishaongea nae akamweleza shida yangu yule mama akakubali. Tumekunywa chai akanitambulisha kwa yule mama, kwamba ndo atanisaidia kwenda shule kama mzazi wangu, duh! Nimampanga yule mama vya kwenda kuongea shuleni akakubali. Akafunga biashara yake kaenda kujiandaa hao tukaenda stendi kuu kupanda gari za shuleni. Yule kaka alinipa na nauli yangu na ya yule mama aisee.

Nilimshukuru sana sana na kumuomba msamaha nilimfikiria vibaya usiku. Akaniambia kuwa na amani bado wanaume wastaarabu tupo. Nikarudi shuleni. Sikumtafuta tena yule kaka na sijui kama yuko tena, ila kati ya watu muhimu walionishika mkono kwny maisha yangu na yeye alikuwepo japo hata sikufanikiwa kumjua jina lake.

It is well with my Soul!
Rafiki yako sijui ana hali gani sasa kama kaanza kugegedwa kwa kulala geto tangu form four

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aprili 2008, Maputo Msumbiji
Kuna hoteli inaitwa Rovuma ipo katikati ya jiji tulivamiwa usiku saa tisa tukaporwa kila kitu. Kuna dada mmoja raia wa Kenya aliposikia mimi ni mtz alinichukua kwake na nikaishi mwezi mzima na kila kitu alinisaidia. Nililia sana mwaka jana nilipopata smsn kutoka kwa mumewe kwamba kafariki kwa ajali akiwa Afrika Kusini. Alinichukulia kama kaka yake alisaidia sana, maana niliibiwa kila kitu hadi nguo. Mungu amlaze mahali pema.
Apumzike kwa amani mdada mwema
 
Mimi nakumbuka 2006 nasafiri kutoka bongo kwenda south africa, kupitia Mozambique. Nilikuwa na passport ile ya karatasi, nilitoka vizuri bongo, mpaka Malawi. Nilifika mzuzu, nikachuka ndinga mpaka brantire. Nilipofika brantire nikaghaili kupitia Mozambique, nikavuka boda ya mwanza kwenda Zambia, nikapitia mbali kabisa mpaka kuingia Lusaka. Nilipofika Lusaka nikachukua basi mpaka Livingstone, hapo sasa nikachukua minbuss mpaka kazungula boda ya Zambia na Botswana, acha bwana ndio Mara ya kwanza kuuona mto Zambezi acheni bwana. Nimeingia kwenye pantoni nikavuka ng'ambo nikagonga nikapewa siku 30, sasa niko njiani kwenda Gabs, wewe acheni bwana kuna watu wanasaidia watu wasio wajua kabisa. Acha niishie hapo
Mkuu, ulitaka kutueleza wema uliofanyiwa na mtu ama ulitaka kutujulisha tu maeneo uliyopitaga??
 
This thread touches my heart.

Some few years back... kwa life la manati, nikawa nimehitimu O level. Matokeo yakatoka, nikachaguliwa kujoin A level kwenye shule fulani iliyopo pale Tabora mjini.

Tarehe ya kuripoti skonga ikafika. Ramani bado haijakaa mkao. Unga unga hapa na pale, nikapata nauli tu. Ada bado channel hazisomi. Nikakata shauri kuwa niende tu shule, ada itafuata.

Siku ya safari ikawadia. Saa 10 alfajiri nipo hewani, jicho kodoo... siku hiyo hata sikupata usingizi, shauku ya kusafiri na kwenda kuanza maisha ya 'boding' ilitawala mtima wangu na Wizara yangu ya kichwa.

11:30 sharp nipo stendi. Nina nauli tu mfukoni. Saa 8 alasiri tukashuka makao makuu ya Nchi na chama... Dodoma! Nina njaa na kiu si ya nchi hii. Nikanunua maji ndogo Uhai nikatuliza koo. Fasta nikaulizia gari la kwenda Tabora.... nikaoneshwa zilipo. Nikajongea pale, mbele yangu naziona Bus kadhaa zikiita abiria. Zikanivutia bus mbili... moja ni NBS Bus nyuma imeandikwa 'Tabora Kwetu'. Nyingine nyuma imeandikwa 'Mboka Manyema'.

I boarded the NBS Bus 'Tabora Kwetu'. Hapa ndiyo kuna mtu baki (a stranger) ambaye huwa sisahau wema wake.

Safari ikaanza. Nimekaa pembeni ya mdada, ni mchangamfu. Mtu wa Urambo. Kufika porini maeneo ya Singida, around saa 2 hivi usiku, bus likaharibika! Aisee nina njaa ya hatari sana muda huo. Nikashuka chini kwenda nje kupunga upepo, almost abiria wote wameshuka chini na story za hapa na pale, Suka & kondakta wanaendelea kurekebisha gari huku wakipakwa mbovu na abiria. Kufika pale chini, kumbe yule mdada ameshahisi nina njaa. Naye akashuka na kuja pale nilipo, akaniuliza "vipi husikii baridi hapa nje? hujabeba hata sweta"? Nikamjibu usijali dada, ni tumbo tu ndiyo nasikia linauma. Aisee yule mdada akapanda kwenye gari na kurudi chini akiwa amebeba kihotpot kidogo, na maji ya chupa. Akaniambia tukae chini tule. Ilikuwa ni kuku wa kukaanga, tamu to the fullest! Daah this lady touched my heart kwakweli.

Saa 7 usiku hivi ndiyo tunaingia stendi ya Tabora mjini. Tukashuka pale, nikamshukuru sana na nikamuuliza shule fulani ipo maeneo gani? Akanijibu ilipo ila akashauri ni risk kwenda usiku, na hakuna wa kunipokea muda huo pale shuleni. Akasema yeye safari yake bado, anaenda urambo, ila kwa usiku huo hakuna usafiri, so analala hapo town. Mie nikaanza kama kusisitiza tu niende shule nikapokelewe hata na mlinzi, the point is sikuwa na hela ya kulala guest. Nakumbuka yule mdada akafungua mkoba wake akanipa Tsh elfu 5, akanambia shuleni sio mbali ila kwavile ni mida mibovu nichukue taxi. Tukaagana pale, nikasema 'Ahsante' nyingi sana zenye adabu ilotukuka. Sikuwaza hata kumuomba namba ya simu coz sikuwa na simu. Akaita taxi, nikamsaidia kupandisha mizigo yake, akateleza!

Nami nikaita taxi. Nikaanza kusaundisha as if ni mwenyeji napoenda. Hapo nishaipigia mahesabu hiyo buku 5 kwamba niamke nayo asubuhi kuanza maisha mapya at skonga. Dereva taxi akataka buku 3, nikasema baridi, twen'zetu. Tukala mguu wa kuku, haooo kuelekea skonga. Hapo ni usiku mkubwa mida ya wanga! Kweli nilipokelewa na mlizi, tukaenda dormitory akanipa kitanda kimoja kilichokuwa wazi nikauchapa. Asubuhi kumekucha nina buku mbili mfukoni, freeesh. Saa nne asubuhi mara nasikia kengele kuuubwa linagongwa, nauliza ni nini, naambiwa ni mida ya uji. Wadau mbio mbio na vikombe/bakuli/visado mkononi. Nami nikaunga tela, hakuna kushangaa. Nafika kwenye foleni nasikia sauti kavu ya Mwalimu wa zamu: "Kwa wale wa form five... kama bado hujawa registered, haruhusiwi kupata uji wala kula chakula cha shule. Usijisumbue kukaa foleni, nishagawa kadi (koponi). Afu form five wote mlojisajiri leo, baada ya kunywa uji muende kufuata kuni, gari (tiper Jiefang) lipo pale Administration Block linawasubiri.. " nikajisemea moyoni duuh ama kweli maisha ya boarding noma, mtoto wa mama bora usome day Bongo DarSlum. Basi nikaenda canteen, ile buku mbili ilosalia ikasimamia shoo na kunilinda siku hiyo.

Maisha yakaendelea pale skonga. Mwaka ukapita. Nikaingia form Six. Siku moja mida ya mchana nipo na washkaji chini ya kivuli cha mti tunapata lunch... kitu dona, harage tatu mchuzi kisado! Nakumbuka was weekend. Mara gafla nasikia naitwa kuwa kuna mgeni wangu. Nanyanyuka na bakuli langu la ugali kuelekea kwenye guests guarden, namuona yule mdada wa kwenye safari. Daaamn, sikuamini macho yangu. Kashikilia kiparcel chenye machungwa na ndizi, na mche wa sabuni. Seriously kuna machozi ya furaha yakaanza kunilengalenga machoni mwangu. Sikuamini kabisa if I was still in her mind. I was so deeply touched, sio kwa vile kaniletea mazagazaga, ni kwa vile she still remembers me after a year to perish since our encounter. Kumbe siku ilee kwenye bus wakati namtajia jina langu na combi nilochaguliwa alinote.

Baada tu ya kusalimiana, nakumbuka kauli yake: "umepungua mdogo wangu, ila vumilia tu na kazana kusoma, ndiyo maisha. Naamini hapa shule unajifunza mengi". Tukaongea mengi na kuchukua namba yake, by that time tayari nishapata simu.

Tangia siku hiyo till todate hatujaonana tena na huyu mpendwa.

Towards completion of my A level, nilimualika na kumuomba aje kwenye gradu yangu japo aniveshe ua na tupige picha za ukumbusho. She cordially confirmed to attend the event. But too sad, closer to gradu day she informed me that hataweza kuhudhuria coz she had undergone miscarriage. She was not okay. Daaah. Eventually nikafunga dirisha la Elimu yangu mjini Tabora. I left Mboka.

Days months years have passed sina mawasiliano na huyu dada mpendwa. Namba yake haipatikani nearly two years now. I don't know, I don't have a clue what happened to this samaritan lady.

Dada angu wa hiari Farida, much love to you out there wherever you might be. You were a total stranger who turned being my best friend & sister. You are sincerely appreciated. You were the first & only person to visit me as ndugu at the school. Your warm kindness embedded in my mind & heart always always always. Popote ulipo nakuombea kwa Mola akuongezee nuru na kukulinda na akuzidishie riziki.

Mdogo wako nipo DarSlum kwa sasa, kicking and hustling. Bado 'sijatusua', still at the scratch. Ila have put it down in my diary kwamba siku Mwenyezi Mungu akinifanyia wepesi, I will come back to Tabora for you dada Farida, just to give hug and tangible thanking.

This world is sick, but watu wema bado wapo jamani. I learnt!

God bless the Woman.

# unconditional love #

-Kaveli-
...Nice Story...Touching Story...!
 
Story hii imenitoa machozi, daaahh
Huu uzi umenikumbusha mbali na kwa kweli umenitoa machozi. Mwaka 1999 nilisaidiwa na "mpigadebe" pale Msamvu Stend, kamwe siji kusahau. Baada ya kumaliza form four matokeo yalitoka nikawa nimefaulu vizuri sana lakini kwa bahati mbaya sikwenda form five kwa wakati kwani baba yangu alikuwa amelezwa hospitali kwa muda mrefu. Mjomba yangu wa Dodoma alipata taarifa akanitumia barua niende ili nikaanze form five seminari moja pale Dodoma.
Kwa kuwa ni stori ndefu naomba nifupishe. Kwa kuwa sikuwa na nauli ya kutosha nilitoka kijijini kwetu nikafika Mbeya ambapo nilipanda treni kwa mara ya kwanza na kushukia Mang'ura. Kutoka Mang'ura mpaka Morogoro mjini (Msamvu ya zamani) nilipanda basi, nikawa nimebakiwa na Sh. 1000 tu mfukoni.

Nilipofika tu Msamvu huku nikiwa nimevaa blauzi nyekundu nakumbuka (mi ni mwanaume) wapiga debe walinivamia huku wakiuliza kwa shauku naenda wapi. Bahati nzuri "Malaika" huyu mpigadebe ndiye alifanikiwa kuchukua begi langu na kunipeleka kwenye gari lililo kuwa linaenda Dodoma. Nilipo uliza nauli Sh ngapi nikaambiwa Sh. 5,000; niliwaambia kwa huruma ninayo Sh 1,000. Konda wa lile basi na baadhi ya wapiga debe walianza kunitolea lugha chafu.

Yule mpiga debe aliniita pembeni na kunitaka nimweleze ukweli Dom naenda kufanya nini na kwa nini sina nauli. Nilimweleza habari zangu zote na hatimaye akaniambia dogo usijali utasafiri. Muda wa kuanza safari ulipofika (kama saa tisa hivi alasiri) yule mpiga debe alichukua begi langu akaweka ndani ya gari akamwambia konda na wenzake "dogo (mimi) lazima asafiri. Kulizuka mzozo mkubwa sana lakini yule "malaika wangu" alishinda. Tulikubaliana nikae chini koridoni na tukifika Dom niache begi nikachukue nauli ndo nije kulikomboa. Tulianza safari na tulipofika Wami kuna mtu alishuka konda akaniambia naweza kukaa sasa kwenye kiti.

Dodoma tulifika saa tatu usiku na ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika Dom. Nakumbuka siku hiyo umeme ulikuwa umekatika sehemu kubwa ya mji wa Dom. Stendi ilikuwa ilipojengwa maktaba ya mkoa hivi sasa. Baada ya watu wote kushuka konda na dreva walinambia niondoke nakichukue hela ndo nije nikomboe begi. Nilichanganyikiwa kwani sikujua nitaendaje kwa mjomba usiku ule ukizingatia ni mara yangu ya kwanza kufika Dom na ushamba juu. Niliamua nilale pale stendi kukicha ndo niende Ihumwa jeshini nikamtafute mjomba. Nilivyokuwa naondoka ghafla dreva aliniuliza dogo kwani mjomba ako anakaa sehemu gani? Nikajibu anakaa Makole shule ya msingi. Waliniambia na wao walikuwa wanaenda kulala Makole kwa hiyo waliniambia nipande tukajaribu kumtafuta mwenyeji wangu.
Tulipofika Makole Guest (saa nne usiku) walipaki gari wakamwita kijana mmoja waliyekuwa wanafahamiana na ambaye baadae alikuja akawa jirani yangu na rafiki yangu. Walimwuliza yule kijana kama anamfaham mama fulani maana akina mama ndo huwa wanafahamika sana na majirani. Yule kijana akajibu "aaaah, namfaham ni jirani yetu na rafiki wa mama.
Yule kijana alichukua begi na kunisindikiza kwa mjomba ambae pamoja na shangazi walishangaa mno. Walilipa ile nauli, na hapo nikawa nimeshuhudia Matendendo Makuu ya Mungu.
Hivi sasa nimesoma na nimepata kazi kubwa na yenye heshima. Bahati mbaya yule mpiga debe hata nikimwona siwezi kumkumbuka tena. Huwa napita pale Msamvu nawasimulia wapigadebe jinsi nilivyosaidiwa na mpiga debe mwenzao na kujaribu kupeleleza lakini sijawahi kumpata. Huenda sijafanya jitihada ya kutosha kumtafuta.

Nimesimlia tukio hili kwa ufupi tu ili kuwatia moyo wenzangu wenye shida na waliokata tamaa, wakumbuke yupo Mungu ambaye ukimwomba kwa imani daima hushuka na kutoa msaada. Mwisho niwaombe tusidharau kazi za wenzetu, mwenzenu nilisaidiwa na mpigadebe,,, watu ambao huwa tunawachukulia kama wezi na wavuta bangi.
 
Back
Top Bottom