LESENI ZA UDEREVA TRA NI WAZEMBE.

LESENI ZA UDEREVA TRA NI WAZEMBE.

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
23,277
Reaction score
28,437
Lipo tatizo sugu la upewaji wa leseni za udereva kwa kisingizio cha uhaba wa kadi! Mimi binafsi muda wa leseni yangu kuisha ni mwezi wa sita, mwezi wa tatu nilikwenda TRA kulipia muendelezo wa leseni yangu nikaambiwa nitaipata baada ya wiki mbili, hata hivyo niliongeza zangu hivyo mwezi huu wa nne nikaenda TRA nikijua nitapata leseni yangu, hola! Niliambiwa nirudi baada ya wiki mbili kama watanijulisha kupitia ujumbe wa simu yangu! Nina mashaka kama TRA wanajua umuhimu wa leseni za udereva, inaelekea kwako kutupa leseni hizo ni hisani si lazima. Idadi ya madereva ni ndogo sana sana ni uzembe uliotukuka wanaposhindwa kuwa na kadi za kutosha.
 
Mkuu mbona walalama wakati hata mda wa leseni yako kuisha bado?

Nnachojua wenyewe hawapendi kusumbua wananchi sema kuna sehemu kuna shida hasa kwenye manunuzi ya matirio za hizo leseni, nahisi mkulu kabana sana ela
 
Mbona mimi pele samora nimepata leseni bila usumbufu mwezi huu wa nne ndo leseni yangu imeisha muda wake sasa wewe wapi wamekusumbua
 
Mkuu mbona walalama wakati hata mda wa leseni yako kuisha bado?
Nnachojua wenyewe hawapendi kusumbua wananchi sema kuna sehemu kuna shida hasa kwenye manunuzi ya matirio za hizo leseni, nahisi mkulu kabana sana ela
Ukisubiri muda wa leseni yako kuisha ufike hautapata nyingine zaidi ya miezi miwili au mitatu mbele.
Usitumie lugha ya kijiweni kwenye jambo usilolijua. Tatizo hili limelalamikiwa kwa miaka sasa bila utatuzi!
 
Kiukweli kuna tatizo kwenye kutoa leseni. Mimi nilipeleka leseni yangu iliyokwisha muda wake mwaka jana mwezi wa nane,nimekuja kupata leseni mpya mwezi wa pili mwaka huu. Kila nilipokuwa nikienda kuulizia niliambiwa bado haijawa tayari. Kuna kitu hatuambiwi hapa! Kuna tatizo.
 
So leseni ikiisha, kuipata nyingine ndo wanasumbua hivyo??

Duh leseni yangu imeisha tarehe 21/04/2019, sijui kama nitawahi kuipata
 
So leseni ikiisha, kuipata nyingine ndo wanasumbua hivyo??
Duh leseni yangu imeisha tarehe 21/04/2019, sijui kama nitawahi kuipata
leseni yangu nilipata baada ya miezi mitatu, wanachokifanya ni kutengeneza mainya ya rushwa bila ulazima ,
 
Me navyojua leseni ikiisha ukailipia basi ile risiti ya malipo ukiipiga copy unaweza tembea nayo hata miaka bila hiyo leseni yao!. Au wenzetu mnamiliki leseni kama kitambulisho!?..
We walipe baki na risiti yako watapojisikia kukuita ufate card utafata!.
 
Me navyojua leseni ikiisha ukailipia basi ile risiti ya malipo ukiipiga copy unaweza tembea nayo hata miaka bila hiyo leseni yao!. Au wenzetu mnamiliki leseni kama kitambulisho!?..
We walipe baki na risiti yako watapojisikia kukuita ufate card utafata!.
unatunzaje hicho kikaratasi cha risiti kisichanike au kupotea?
 
unatunzaje hicho kikaratasi cha risiti kisichanike au kupotea?
Kikiwa kipya piga copy itatoka clear then kilaminate sababu matumizi yake ni kwenye gari basi kiweke kwenye glove box huna haja ya kutembea nacho, ukipigwa mkono unawatolea watajiongeza wenyewe!..
Usisahau laminate na copy ya expired card kuna wale wanoko wataokuomba ya zamani!..
Baada ya hapo fanya mambo yako, siku moja wenyewe TRA watakumiss utaona sms yao!.
 
Kikiwa kipya piga copy itatoka clear then kilaminate sababu matumizi yake ni kwenye gari basi kiweke kwenye glove box huna haja ya kutembea nacho, ukipigwa mkono unawatolea watajiongeza wenyewe!..
Usisahau laminate na copy ya expired card kuna wale wanoko wataokuomba ya zamani!..
Baada ya hapo fanya mambo yako, siku moja wenyewe TRA watakumiss utaona sms yao!.
Umeongea vyema Sana,
Tatizo tunahitaji Kama kitambulisho kwenye issues zingine
 
Umeongea vyema Sana,
Tatizo tunahitaji Kama kitambulisho kwenye issues zingine
Mkuu mpaka leo hii huna ID ya Kupiga kura au ya NIDA?.. Mbona vyote hivi matumizi yake ni aina moja tu!.
Ingawa kwa madereva waomba ajira kweli ni changamoto ila kwa watu wengine card ya Leseni ya Udereva haina maana sana!.
Poleni lakini!.
 
Me navyojua leseni ikiisha ukailipia basi ile risiti ya malipo ukiipiga copy unaweza tembea nayo hata miaka bila hiyo leseni yao!. Au wenzetu mnamiliki leseni kama kitambulisho!?..
We walipe baki na risiti yako watapojisikia kukuita ufate card utafata!.
Usitake tuvunje sheria, tueleze kifungu cha sheria kinachoruhusu karatasi ya malipo kuwa mbadala wa leseni ili nasi tukitumie.
 
Ukisubiri muda wa leseni yako kuisha ufike hautapata nyingine zaidi ya miezi miwili au mitatu mbele.
Usitumie lugha ya kijiweni kwenye jambo usilolijua. Tatizo hili limelalamikiwa kwa miaka sasa bila utatuzi!
Huyo kapata kwa njia ya mlungula.
Leseni sasa hivi watu wanakaa hadi miezi sita kusotea. Wanasema hawana material ya kutengenezea.
Ajabu pesa wanaingiza nyingi mno
 
Umeongea vyema Sana,
Tatizo tunahitaji Kama kitambulisho kwenye issues zingine
Kumbuka kadi iliyokwisha muda kuwa muda mrefu inakufa na ukitaka kuifufua itabidi urudi mafunzoni tena.
 
Me navyojua leseni ikiisha ukailipia basi ile risiti ya malipo ukiipiga copy unaweza tembea nayo hata miaka bila hiyo leseni yao!. Au wenzetu mnamiliki leseni kama kitambulisho!?..
We walipe baki na risiti yako watapojisikia kukuita ufate card utafata!.
Waliwahi nikamata na hiyo risiti na hawakuelewa
 
Back
Top Bottom