Les wanyika na wimbo wa sina makosa

Les wanyika na wimbo wa sina makosa

Mzee2000

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2009
Posts
528
Reaction score
221
Nakumbuka wimbo huu nilipokuwa mdogo sikuufatilia sana sasa nimekuwa DAD duh,zilipendwa hizi nazipenda sana sasa hivi, je hawa jamaa wa les wanyika bado wapo? Na huu wimbo uliimbwa lini? Nakumbuka kuna mnigeria mmoja huku majuu alinimbia wimbo wote, nikashangaa aliujuaje? Kwa kweli bongo enzi zile tulikuwa na waimbaji, sina ubaya na bongo fleva, lakini tutakubaliana originality ya music hasa hapa bongo imepungua sana.
 
Sina Makosa ulirekodiwa na Les Wanyika mwaka 1978. Bendi hiyo iliyokuwa ikiundwa na wanamuziki wengi kutoka Tanzania ilikuwa na makao yake jijini Nairobi na ilikuwa iliongozwa na mpiga rhythm 'Profesa' Omari Shabani, ambaye sasa ni marehemu. Baadhi ya wanamuziki wengine Watanzania walioshiriki katika kibao hicho kilichotungwa na Profesa Omari in mwimbaji Issa Juma na mpiga solo John Ngereza, ambao nao pia wameshatangulia mbele ya haki. Les Wanyika ni kama haipo baada ya bendi hiyo kufifia kufuatia wengi wa wanamuziki wake kufariki dunia. Baada ya Profesa Omari na Ngereza kufariki mwishoni mwa miaka ya 1990, bendi iliongozwa na mwanamuziki Mkenya, Freshley Mwamburi.
 
Sina Makosa ulirekodiwa na Les Wanyika mwaka 1978. Bendi hiyo iliyokuwa ikiundwa na wanamuziki wengi kutoka Tanzania ilikuwa na makao yake jijini Nairobi na ilikuwa iliongozwa na mpiga rhythm 'Profesa' Omari Shabani, ambaye sasa ni marehemu. Baadhi ya wanamuziki wengine Watanzania walioshiriki katika kibao hicho kilichotungwa na Profesa Omari in mwimbaji Issa Juma na mpiga solo John Ngereza, ambao nao pia wameshatangulia mbele ya haki. Les Wanyika ni kama haipo baada ya bendi hiyo kufifia kufuatia wengi wa wanamuziki wake kufariki dunia. Baada ya Profesa Omari na Ngereza kufariki mwishoni mwa miaka ya 1990, bendi iliongozwa na mwanamuziki Mkenya, Freshley Mwamburi.

Mkuu big up! mm sasa hivi natizama video yao, kwahiyo video hii ya nyimbo zao wale wakongwe hawamo isipokuwa Freshley pekee ndo yumo?
 
Mkuu big up! mm sasa hivi natizama video yao, kwahiyo video hii ya nyimbo zao wale wakongwe hawamo isipokuwa Freshley pekee ndo yumo?

Hiyo video hata mimi nimeiona YouTube. Ni video ambayo imetengenezwa miaka michache iliyopita, miaka mingi baada ya kibao cha Sina Makosa kurekodiwa. Nimechunguza sana lakini sikuona hata mwanamuziki mmoja aliyeshiriki katika kurekodi kibao hicho mwaka 1978. Ninahisi hili ni kundi tu la vijana wanaoishi Nairobi waliojikusanya na kurekodi video hiyo lakini nadhani wamefanya makosa kutumia wimbo 'original' katika kazi yao hiyo. Hawa ingefaa warekodi 'version' yao ya Sina Makosa na kuitumia katika video hiyo kama walivyofanya wanamuziki wengine kama marehemu Cool James.
 
Naukubali sana huo wimbo wa Sina Makosa. Siku haiwezi kukamilika bila kuusikiliza huo wimbo.
 
Sina Makosa ulirekodiwa na Les Wanyika mwaka 1978. Bendi hiyo iliyokuwa ikiundwa na wanamuziki wengi kutoka Tanzania ilikuwa na makao yake jijini Nairobi na ilikuwa iliongozwa na mpiga rhythm 'Profesa' Omari Shabani, ambaye sasa ni marehemu. Baadhi ya wanamuziki wengine Watanzania walioshiriki katika kibao hicho kilichotungwa na Profesa Omari in mwimbaji Issa Juma na mpiga solo John Ngereza, ambao nao pia wameshatangulia mbele ya haki. Les Wanyika ni kama haipo baada ya bendi hiyo kufifia kufuatia wengi wa wanamuziki wake kufariki dunia. Baada ya Profesa Omari na Ngereza kufariki mwishoni mwa miaka ya 1990, bendi iliongozwa na mwanamuziki Mkenya, Freshley Mwamburi.

Wilson Peter Kinyonga na George Peter Kinyonga pia walikuwa ndugu na pia wamamuziki mahiri wa bendi hii, Watanzania wenyeji wa Mkoa wa Tanga. Nao wameshatangulia mbele ya haki, ila kazi yao nzuri inatufanya tuwakumbuke.
 
Wilson Peter Kinyonga na George Peter Kinyonga pia walikuwa ndugu na pia wamamuziki mahiri wa bendi hii, Watanzania wenyeji wa Mkoa wa Tanga. Nao wameshatangulia mbele ya haki, ila kazi yao nzuri inatufanya tuwakumbuke.

Sahihisho mkuu. Wilson na George Peter Kinyonga hawakuwahi kuwemo katika kundi la Les Wanyika. Hawa walikuwa SIMBA WANYIKA ambayo ni chimbuko la Les Wanyika iliyoanzishwa na 'Profesa' Omari Shabani aliyekuwa mpiga rhythm wa Simba Wanyika. Les Wanyika ni miongoni mwa bendi nyingi zilizotokana na Simba Wanyika (offshoots) na ambazo zilikuwa na neno 'Wanyika' katika majina yao. Itakumbukwa kuwa mwimbaji Issa Juma Singano (aliyeimba Sina Makosa) alijitoa Les Wanyika mwaka 1981 na kuunda Super Wanyika. Baadae kukawa na bendi nyingine kama Wanyika Stars na Super Wanyika Stars.
 
Back
Top Bottom