Leo ni siku ya emoji Duniani

Leo ni siku ya emoji Duniani

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
1,221
Reaction score
2,425
1_20250717_181647_0000.png


Kila mwaka ifikapo tarehe 17 July Duniani watu huweza kusherekea siku ya Emoji Duniani. Emoji ni ishara inayoelezea kwa Namna gani mtu anajisikia Kwa wakati huo.

Emojis Kwa mara ya kwanza iligunduliwa mwaka 1999 na jamaa anaitwa Shigetaka Kurita, ni mjapani ambaye aliamua kuunda Emoji ili kuweza kurahisisha watu katika kueleza hisia aliyonayo kupitia mfumo wa kidigitali.

2_20250717_181647_0001.png


Kwa mara ya kwanza aliweza kutoa emoji zenye ishara 176 pekee, na ziliweza kushika Kasi Nchini Japan kabla ya kusambaa Duniani kote. Mpaka kufikia Desemba 2024 jumla ya emoji zote Duniani zilikua 3,790.

emoji-gty-er-250716_1752685284512_hpMain_16x9_992.jpg


Hesabu hii inajumuisha Emoji zote kuanzia za bendera, solo emoji , jinsia nk. mwaka zinaweza kuongezeka emoji 164 mpaka kufikia Desemba 2025 tutakua na jumla ya emoji 3954. Emojis ni zaidi ya hisia inayomtambulisha binadamu.

Ebu tuambie emoji gani unapenda sana kuzitumia kwenye simu yako !!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom