Leo ndio nimegundua, Mzee Lowassa ana akili nyingi na ustaarabu mwingi

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Leo nimegundua kuwa Mzee Edward Lowassa ni mstaarabu sana. Warusi wanatumia neno kachestveni ( high quality a person).

Kama kila tusi analotukanwa mtu lingekuwa linaleta kovu mwilini, Mzee huyu asingekuwa anatazamika kwa sasa.

Ukimya wake kila anaposhambuliwa ni kitabu tosha kabisa chenye kurasa zinazozungumzia uvumilivu na ustaarabu anaopaswa kuwanao mwanadamu mwenye kujifahamu.

Pengine Mzee afikirie juu ya kuandika kitabu kuhusu maisha yake ya kisiasa, vizazi vijavyo vya wanasiasa vitabakiwa na kumbukumbu elimishi.

Watoto wake waanze kufikiria juu ya utamaduni huo, zile kumbukizi (legacy) za kina Malcom X na Martin Luther na wanaharakati wengine, bado zipo hai kwa sababu ya ukweli kwamba maandishi huwa hayafi.

Unapokaa kimya na kutii mamlaka hata kama unaona upungufu mwingi ndani ya hizo mamlaka, ni kuendelea kuitunza amani ya rohoni.

Wanasiasa mjifunze kwamba kupayukapayuka kunaweza kukupunguzia heshima mbele ya jamii.
 
Leo nimegundua kuwa Mzee Edward Lowassa ni mstaarabu sana. Warusi wanatumia neno kachestveni ( high quality a person).

Kama kila tusi analotukanwa mtu lingekuwa linaleta kovu mwilini, Mzee huyu asingekuwa anatazamika kwa sasa.

Ukimya wake kila anaposhambuliwa ni kitabu tosha kabisa chenye kurasa zinazozungumzia uvumilivu na ustaarabu anaopaswa kuwanao mwanadamu mwenye kujifahamu.

Pengine Mzee afikirie juu ya kuandika kitabu kuhusu maisha yake ya kisiasa, vizazi vijavyo vya wanasiasa vitabakiwa na kumbukumbu elimishi.

Watoto wake waanze kufikiria juu ya utamaduni huo, zile kumbukizi (legacy) za kina Malcom X na Martin Luther na wanaharakati wengine, bado zipo hai kwa sababu ya ukweli kwamba maandishi huwa hayafi.

Unapokaa kimya na kutii mamlaka hata kama unaona upungufu mwingi ndani ya hizo mamlaka, ni kuendelea kuitunza amani ya rohoni.

Wanasiasa mjifunze kwamba kupayukapayuka kunaweza kukupunguzia heshima mbele ya jamii.
Ni hulka na haiba yake haiigiki
 
Mda mwingine kuacha mapungufu yaendelee ni kuacha tatzo likue
Leo nimegundua kuwa Mzee Edward Lowassa ni mstaarabu sana. Warusi wanatumia neno kachestveni ( high quality a person).

Kama kila tusi analotukanwa mtu lingekuwa linaleta kovu mwilini, Mzee huyu asingekuwa anatazamika kwa sasa.

Ukimya wake kila anaposhambuliwa ni kitabu tosha kabisa chenye kurasa zinazozungumzia uvumilivu na ustaarabu anaopaswa kuwanao mwanadamu mwenye kujifahamu.

Pengine Mzee afikirie juu ya kuandika kitabu kuhusu maisha yake ya kisiasa, vizazi vijavyo vya wanasiasa vitabakiwa na kumbukumbu elimishi.

Watoto wake waanze kufikiria juu ya utamaduni huo, zile kumbukizi (legacy) za kina Malcom X na Martin Luther na wanaharakati wengine, bado zipo hai kwa sababu ya ukweli kwamba maandishi huwa hayafi.

Unapokaa kimya na kutii mamlaka hata kama unaona upungufu mwingi ndani ya hizo mamlaka, ni kuendelea kuitunza amani ya rohoni.

Wanasiasa mjifunze kwamba kupayukapayuka kunaweza kukupunguzia heshima mbele ya jamii.
 
Angekuwa na akili nyingi basi 2005 yeye ndo angegombea Urais. Watoto wa mjini wakamtumia kisa tu eti alietoka ni mkristo basi Lowassa asubiri baada ya JK. And everything ilikuwa against him baada ya hapo. Its sad that he will never be the president of Tanzania.
Kawa mstaarabu na mwenye kutii mamlaka. Kaamua kutulia, tofauti na hawa wengine wanaendekeza majungu.

Sad, aliutamani sana urais, maishani sio kila unachokitaka utakuja kukipata.
 
Leo nimegundua kuwa Mzee Edward Lowassa ni mstaarabu sana. Warusi wanatumia neno kachestveni ( high quality a person).

Kama kila tusi analotukanwa mtu lingekuwa linaleta kovu mwilini, Mzee huyu asingekuwa anatazamika kwa sasa.

Ukimya wake kila anaposhambuliwa ni kitabu tosha kabisa chenye kurasa zinazozungumzia uvumilivu na ustaarabu anaopaswa kuwanao mwanadamu mwenye kujifahamu.

Pengine Mzee afikirie juu ya kuandika kitabu kuhusu maisha yake ya kisiasa, vizazi vijavyo vya wanasiasa vitabakiwa na kumbukumbu elimishi.

Watoto wake waanze kufikiria juu ya utamaduni huo, zile kumbukizi (legacy) za kina Malcom X na Martin Luther na wanaharakati wengine, bado zipo hai kwa sababu ya ukweli kwamba maandishi huwa hayafi.

Unapokaa kimya na kutii mamlaka hata kama unaona upungufu mwingi ndani ya hizo mamlaka, ni kuendelea kuitunza amani ya rohoni.

Wanasiasa mjifunze kwamba kupayukapayuka kunaweza kukupunguzia heshima mbele ya jamii.

Mnafiki mkubwa wewe, leo hii baada ya kumdhalilisha mzee wa watu ndiyo mnafahamu kwamba alikuwa ni muungwana ? Ninyi waafrika sijui mlilaaniwa na nani: Mzee wa watu mpaka leo hii ni mgonjwa kisa upumbavu wa wachumia matumbo wachache kama ninyi ambao mlikuja kumpa kashfa, matusi na kejeli za kila namna mitandaoni kisa kulinda tumbo lako na kufuata mkumbo wa wana-CCM waliokuwa na chuki naye ambazo chanzo chake wengi hamkikujua.

Leo hii umetokea ugomvi ndani ya chama ndiyo unajifanya unazijua busara za mzee wa watu. Jitu zima hovyo, kabisa......
 
Mzee ana roho ngumu sana tena sana, alikubali kutolewa kafara kwa kubambikiziwa rushwa ya ki-mfumo ndani ya chama, haikutosha rafiki yake na mwanamkakati mwenzake akamtosa mchana kweupe. Bado yupo tu.

Kisasi ni cha Bwana, maana hukumu zake ni za haki na kweli
 
Tukiangalia nyuma katika siasa za Tanzania, Lowassa aliponea awamu ya Nyerere kwa kuamini kuwa ukimya na kumnyenyekea aliye mamlakani ni njia bora kuliko kuliko kujipambanua na kutofautiana.

Lowassa huyo huyo akapona kipindi cha Mwinyi kwa njia hiyo hiyo na pia kipindi cha Mkapa. Lowassa aliweza kupenya kote huko mpaka alipofikia kilele cha siasa zake pale alipoteuliwa kuwa waziri mkuu na swahiba wake JK.

Kosa alilolifanya Lowassa ni kuamini kuwa yeye alikuwa juu kuliko kiti cha urais wakati wa swahiba wake JK. Akasahau kuwa urais ni mamlaka na siyo mtu. Hakujua kumbe hata mbumbumbu angeweza kuwekwa hapo na nchi ikaenda. Aliamini kabisa kuwa JK ni saizi yake. Akaamini njia ya kumkabili JK itakuwa tofauti na ile aliyoizoea kuitumia awamu zilizopita. Akaanza kujiwekea mfumo wake, akakiteka chama kupitia NEC, akaiteka serikali kwa kumchagulia JK wakuu wa mikoa na viongozi wa taasisi mbalimbali, akaanzisha "TEAM LOWASSA".

JK kushtuka, mara ameshathibitiwa kila kona. Njia pekee ikabaki ni kumfukuza Lowassa uwaziri mkuu ili aweza kumnyoosha kwa kuua mfumo wake ndani ya serikali na chama. Mipango ikasukwa, mambo yakapangwa yakapangika, Lowassa akatengenezewa jeraha la maisha kwa kutengenezewa kashfa kubwa ya Richmond.

Wanamipango wakatafuta namna yoyote wamuue mzee wa watu. Wakafanikiwa kumwekea sumu ila bahati nzuri Mungu akaepusha hilo, akakimbilia Ujerumani, wazungu wakamponyesha.

Mzee wa watu hakuchoka, akaendeleza harakati zake huku akiamini haki yake ataipata ndani ya CCM. Msimamo huu ukamfanya kuwa mdudu anayetisha ndani ya CCM na serikalini. Akawatia hofu kuu wale wote waliomtesa. Wakajiapiza kuwa hata chama kitampitisha, jina lake litakatwa kwenye hatua za awali.

Pamoja na maapizo hayo, Lowassa bado aliamini kuwa haki yake ataipata ndani ya CCM. Akaamini ule mtandao aliouasisi utamsaidia kuwashinda wakuu wa chama na serikali. Akaendeleza safari yake alitoibatiza "safari ya matumaini".

Siku ya hukumu ilipowadia, mzee wakamwandalia ambulance nje, wakaandaa wanausalama na wanajeshi wa kutosha kuzuia jaribio lolote la mapinduzi, wakamtorosha aliyekuwa mkuu wa majeshi Jenerali Mwamunyange ambaye aliaminika ni mmoja wa "TEAM LOWASSA".

Siku ikawadia, jina la Lowassa likakatwa...........

HADITHI HII YAPASWA IMPATE MWANDISHI MAHIRI AIWEKE KWENYE MAANDISHI.

Napendekeza kitabu kiitwe

"Safari ya Matumaini - Kushindwa kwa Demokrasia ndani ya Chama cha Mapinduzi".
 
Back
Top Bottom