Abdul Nondo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 515
- 2,875
Leo Nape na Kinana wanaitwa waasi ndani ya CCM ,Siku zinaenda kasi kweli aisee ! ,Mbaya zaidi wanatumia neno "Waasi" "Wahaini" unajiuliza hivi hawa wanaotumia haya maneno wanajua maana ya maneno hayo? Au wanatumia tuu !! ,Kutofautiana kimawazo au kupinga na kukosoa jambo katika taasisi au dhidi ya kiongozi haijawahi kuwa uwasi wala uhaini.
Tena wanaitwa waasi na wahaini na mtu ambaye hajawahi hata kuongeza mwanachama hata mmoja ndani ya CCM. Kinana aliyelala nje ili kukuza chama ,aliyezunguka vijijini akilima na kusaidia kujenga nyumba za wanakijiji ili kukuza chama na kurudisha imani ya chama kwa wananchi leo anaitwa Muasi ,duuu ! Poleni sana Kinana , Makamba na Nape.
Ipo hivi ,huo mgogoro unaokuzwa na kuonekana ni uhaini na uwasi wa Kinana ,Nape na Makamba haujawahi kuwa mgogoro ,labda kuwe kuna kitu kinapikwa.
Katika falsafa ya Johann Fichte iliyokujakuendelezwa na George Friedrich Hegel na Karl Max inayoitwa Contradiction/au dialectical methods/Materialism inaangazia mgogoro kama njia ya kuzaliwa mawazo mapya ,au mabadiliko dhidi ya pande mbili zenye msuguano.
Katika Nadharia hii ya mgogoro au contradiction kuna hatua 3 ,zinaitwa "The triad" ya kwanza ni Thesis ,pili ni anthesis tatu ni Synthesis .
1.Thesis ni maelezo , statement ya upande fulani ambayo yanaweza kera au kuudhi upande wa pili (Maelezo ya Musiba dhidi ya Kinana na Makamba ,haya huitwa Thesis au statement au proposition). 2.Anthesis ,ni reaction ya thesis yaani ni mkanusho wa Thesis (Negation of Thesis) ,hapa ni Makamba na Kinana kutoa waraka dhidi ya maelezo na tuhuma za Musiba dhidi yao pia hata audio dhidi ya yanayoendelea,hapa ni Anthesis dhidi ya Thesis .
3.Synthesis ,hii ni hatua ya mwisho kabisa ya kuhakikisha suluhu inapatikana kati ya pande hizi yaani kati ya Thesis na Anthesis na hutoa suluhisho ,(Climax) Mara zote Synthesis ndio huwa inatoa majibu kamili ya maana ya mgogoro na contradiction iliyokuwepo.
Hivyo,tusubiri Synthesis sababu hatua zote mbili zimeonekana ,hivyo mgogoro hauwezi kuisha bila hatua ya mwisho ,hivyo tuvute subra ! Mgogoro kidogo ! tutaelewa tuu maana ya yanayoendelea!
Tena wanaitwa waasi na wahaini na mtu ambaye hajawahi hata kuongeza mwanachama hata mmoja ndani ya CCM. Kinana aliyelala nje ili kukuza chama ,aliyezunguka vijijini akilima na kusaidia kujenga nyumba za wanakijiji ili kukuza chama na kurudisha imani ya chama kwa wananchi leo anaitwa Muasi ,duuu ! Poleni sana Kinana , Makamba na Nape.
Ipo hivi ,huo mgogoro unaokuzwa na kuonekana ni uhaini na uwasi wa Kinana ,Nape na Makamba haujawahi kuwa mgogoro ,labda kuwe kuna kitu kinapikwa.
Katika falsafa ya Johann Fichte iliyokujakuendelezwa na George Friedrich Hegel na Karl Max inayoitwa Contradiction/au dialectical methods/Materialism inaangazia mgogoro kama njia ya kuzaliwa mawazo mapya ,au mabadiliko dhidi ya pande mbili zenye msuguano.
Katika Nadharia hii ya mgogoro au contradiction kuna hatua 3 ,zinaitwa "The triad" ya kwanza ni Thesis ,pili ni anthesis tatu ni Synthesis .
1.Thesis ni maelezo , statement ya upande fulani ambayo yanaweza kera au kuudhi upande wa pili (Maelezo ya Musiba dhidi ya Kinana na Makamba ,haya huitwa Thesis au statement au proposition). 2.Anthesis ,ni reaction ya thesis yaani ni mkanusho wa Thesis (Negation of Thesis) ,hapa ni Makamba na Kinana kutoa waraka dhidi ya maelezo na tuhuma za Musiba dhidi yao pia hata audio dhidi ya yanayoendelea,hapa ni Anthesis dhidi ya Thesis .
3.Synthesis ,hii ni hatua ya mwisho kabisa ya kuhakikisha suluhu inapatikana kati ya pande hizi yaani kati ya Thesis na Anthesis na hutoa suluhisho ,(Climax) Mara zote Synthesis ndio huwa inatoa majibu kamili ya maana ya mgogoro na contradiction iliyokuwepo.
Hivyo,tusubiri Synthesis sababu hatua zote mbili zimeonekana ,hivyo mgogoro hauwezi kuisha bila hatua ya mwisho ,hivyo tuvute subra ! Mgogoro kidogo ! tutaelewa tuu maana ya yanayoendelea!