Sethshalom
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 581
- 1,000
Ndugu mm ni mlokole nimezaliwa huko nimekulia huko, lakin nakushauri kwa majibu hayo unayopewa hata ukibadili dini anaweza asije akawa mke sahihi kwako. Wanawake wengi wa hivyo siyo wife materials kivile kama wanavyodai wako kwa Muungu zaidi. Wanakua ba tabia za kujisahau na kusikiliza viongozi wao wa kanisa kuliko ww mume wako. Ila kwa ufupi punguza kasi kama unaweza kutafuta mbadala itakua vizuri zaidi. Kwenye ndoa unahitaji mtu anaekuelewa zaidi na anaeishi Maisha halisi na si ya kujificha nyuma ya kivuli cha dini.Kwanza poleni kwa msiba uliotukumbu sisi site wa kuondokewa na mpendwa wetu Rais JPM Mungu atutie nguvu kipindi hiki kigumu.Leo naomba niletr mrejesho wa uzi wangu nilioandika hapa takribani miezi kadhaa iliyopita.
Awali ya yote nitoe shukurani zangu za dhati kwa michango yenu kwa uzi uliopita, ambao hamkuweza kusoma huu uzi mwanzoni,basi mnaweza upitia hapa Yamenikuta kwa huyu msichana, naomba ushauri wenu .
Pamoja na michango yenu lakini sikuacha kufanya mawasiliano na huyu binti na mpaka ninavyoandika hapa jana tu nimetoka tukibadilishana nae mawili matatu kuhusiana na kile tulichokua tukijalidili mwanzoni kama mlivyosoma kwenye uzi hapo juu.
Kwa awamu nyingine Jana nimebahatika kwenda kwake na kuongea mambo mengi lakini kubwa kabisa ni kukumbushia kuhusu swala letu la mahusiano. Kumbuka tulipokutana kwa mala ya mwisho alinijibu kwamba hawezi kuolewa wala kuwa na mahusiano na Mwanaume asiye wa dhehebu lake (asiye okoka) na hakutaka mtu aokoke kwa kigezo cha kumfata au kumpata yeye yaani tayari awe anaishi kwenye dini hiyo.
Jana nilipoonana naye nilijaribu kukumbushia hili suala,alichojibu ni kwamba hawezi kusema chochote kinachohusuana na mahusiano au kuolewa mpaka suala la kubadili dini kwa mimi lifanyike halafu suala lingine lifuate.Hii inaama kwamba kwa sasa hatuwezi kujadili au kutoa jibu la moja kwa moja juu ya kuoana au mahusiano mpaka suala la kwanza lifanyike yaani la mimi kuokoka.
Binafsi sijamwelewa huyu mwanamke ana maana gani na itoshe pale kwake anakaa pekeyake karibu nyumba nzima na ikitokea mimi naenda pale, yeye ananikaribisha nje ,akijibu kwamba yeye ni mtumishi wa Mungu so hawezi kumkaribisha mwanaume ndani ilihali hamna watu wengine pale ndani ,atanikaribisha tu endapo ndani patakua na mtu mwingine watu 3 na sio watu 2.
Kiujumla sijaelewa kabisa juu ya huyu msichana naleta huu mrejesho ili tuendelee kujadili kidogo juu ya hii kitu kwa sababu naamini kuna jf ndio kila kitu na kuna manguli wa haya mambo.Mniwie radhi sio mzuri sana wa kuandika wadau.