Leo katika Historia: Simba S.C

sembo

JF-Expert Member
May 25, 2011
4,350
3,451
Wahenga walishawahi kunena;
"If you don't know history, then you don't know anything. You are a leaf that doesn't know it is part of a tree."

Wanamsimbazi wenzangu, hebu tukumbushane baaadhi ya kumbukumbu mujarabu, ili tusiwe kama jani walilokua wanalizungumzia wahenga.

LiGI KUU.
1. Miaka 39, Siku 15 zilizopita [July 19, 1977]!!
Simba S.C v Yanga S.C 6-0
WAFUNGAJI:
SIMBA; Abdallah King Kibadeni Mputa dk. 10, 42 na 89 [hii rekodi yake haijavunjwa mpaka sasa], Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73.
YANGA; Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

2. Miaka 22, Siku 31 zilizopita [July 2, 1994]!!
Simba S.C v Yanga S.C 4-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: George Magere Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani "Mzee wa Kiminyio" na Dua Saidi.
YANGA; Constantine Kimanda.

3. Miaka 4, Siku 84 tu zilizopita [May 6, 2012]
Simba S.C v Yanga S.C 5-0
WAFUNGAJI:
SIMBA: Emmanuel Anorld Okwi dk 1 na 52, Felix Sunzu dk 47, Juma Kaseja dk 66 na Patrick Mutesa Mafisango dk 73.

BONUS: KOMBE LA TUSKER.
Miaka 12, Siku 125 zilizopita [March 31, 2002]!!
Simba S.C Vs Yanga S.C 4-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: Mark Sirengo dk. 3 na 76, Madaraka Selemani dk. 32 na Emanuel Gabriel dk. 83.
YANGA: Sekilojo Chambua dk 16.

NB: Katika mechi hii, Mtani nusura aweke mpira kwapani na hii ni baada ya Madaraka Selemani "Mzee wa Kiminyio" kupachika goli maridadi kabisa kuwahi kushuhudiwa katika Uwanja wa Uhuru, na hii ilikua ni dk. ya 32.

Japo katika miaka 4 iliyopita, Mnyama katetereka kweli kweli.. ila Historia haioneshi kama alishawahi kuadhibiwa kwa vipigo vizito kama huyo "Jamaa".

Naimani Msimu huu "ni zamu yetu'' tunaenda kuongeza kumbukumbu nyingine "mujarabu" katika vitabu vyetu vya HISTORIA.
 
Najua kuna Wakuu "sana" watakuja na swali kama hili..

Swali: Sasa hizo historia zinawasaidia nini kwa sasa?

Wahenga wanawajibu;
"If you don't know history, then you don't know anything. You are a leaf that doesn't know it is part of a tree."
 
kilimbamula.

Yanga SC amekuwa akiwapo dozi simba pakubwa sana.

Hii inathibitishwa na ukweli wa kwamba.
- Simba SC mpaka sasa anadaiwa idadi ya MAGOLI ya kufungwa na Yanga SC....

- Simba SC mpaka saaa inadaiwa idadi ya MECHI za kufungwa na Yanga SC.....



92 - idadi ya mechi (mpaka msimu 2015/16) ambazo Yanga SC imekutana na Simba SC tangu kuanzishwa kwa LigiKuu Tanzania mwaka 1965.

189 - idadi ya magoli yaliyofungwa tangu Yanga SC na Simba SC zianze kukutana ligi ilipoanza mwaka 1965 mpaka mwaka 2015/16.

101 -idadi ya magoli ambayo Yanga SC imeifunga Simba SC, Magoli 13 zaidi ya waliyofungwa na Simba SC. tangu ligi iasisiwe 1965

13 - Simba SC wanatakiwa wafunge magoli 13 dhidi ya Yanga SC bila kuruhusu goli ili wafikie idadi sawa ya magoli waliyofungwa na Yanga SC.

35 - mechi ambazo Yanga SC imeshinda dhidi ya Simba SC kati ya mechi 92 walizopata kukutana. Imepoteza 22, sare 35.

13 - Simba SC inatakiwa ishinde mechi kumi dhidi ya Yanga bila kupoteza ili kufikia idadi ya mechi ambazo Yanga SC imeifunga Simba.
 
Vile vile kuna mwaka half time mkakataa kurudi uwanjani nayo pia muiweke katika kumbukumbu zenu.
 
Wahenga walishawahi kunena;
"If you don't know history, then you don't know anything. You are a leaf that doesn't know it is part of a tree."

Wanamsimbazi wenzangu, hebu tukumbushane baaadhi ya kumbukumbu mujarabu, ili tusiwe kama jani walilokua wanalizungumzia wahenga.

LiGI KUU.
1. Miaka 39, Siku 15 zilizopita [July 19, 1977]!!
Simba S.C v Yanga S.C 6-0
WAFUNGAJI:
SIMBA; Abdallah King Kibadeni Mputa dk. 10, 42 na 89 [hii rekodi yake haijavunjwa mpaka sasa], Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73.
YANGA; Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

2. Miaka 22, Siku 31 zilizopita [July 2, 1994]!!
Simba S.C v Yanga S.C 4-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: George Magere Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani "Mzee wa Kiminyio" na Dua Saidi.
YANGA; Constantine Kimanda.

3. Miaka 4, Siku 84 tu zilizopita [May 6, 2012]
Simba S.C v Yanga S.C 5-0
WAFUNGAJI:
SIMBA: Emmanuel Anorld Okwi dk 1 na 52, Felix Sunzu dk 47, Juma Kaseja dk 66 na Patrick Mutesa Mafisango dk 73.

BONUS: KOMBE LA TUSKER.
Miaka 12, Siku 125 zilizopita [March 31, 2002]!!
Simba S.C Vs Yanga S.C 4-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: Mark Sirengo dk. 3 na 76, Madaraka Selemani dk. 32 na Emanuel Gabriel dk. 83.
YANGA: Sekilojo Chambua dk 16.

NB: Katika mechi hii, Mtani nusura aweke mpira kwapani na hii ni baada ya Madaraka Selemani "Mzee wa Kiminyio" kupachika goli maridadi kabisa kuwahi kushuhudiwa katika Uwanja wa Uhuru, na hii ilikua ni dk. ya 32.

Japo katika miaka 4 iliyopita, Mnyama katetereka kweli kweli.. ila Historia haioneshi kama alishawahi kuadhibiwa kwa vipigo vizito kama huyo "Jamaa".

Naimani Msimu huu "ni zamu yetu'' tunaenda kuongeza kumbukumbu nyingine "mujarabu" katika vitabu vyetu vya HISTORIA.

Aisee we jamaa una akili sana ilibidi ukaishi Maracana
 
Asante sana kwa historia ila hii hapo chini vipi au haituhusu?
ImageUploadedByJamiiForums1470246455.798768.jpg
 
Usizungumzie historia tu,na leo mmechapwa kagoli kamoja huko Morogoro na timu ya Manispaa ya Kinondoni(KMC FC) mpaka mkataka kupigana,ongeza ni na hiyo kwenye historia ya mwakani
Vile vile kuna mwaka half time mkakataa kurudi uwanjani nayo pia muiweke katika kumbukumbu zenu.
Ilikua mwaka 1992 kwenye ligi ya Muungano wa mchangani hawakurudi uwanjani kipindi cha pili kwani walijua zitakua nyingi alikua kishapigwa goli mbili kwa kamoja kao.
.
 
Usizungumzie historia tu,na leo mmechapwa kagoli kamoja huko Morogoro na timu ya Manispaa ya Kinondoni(KMC FC) mpaka mkataka kupigana,ongeza ni na hiyo kwenye historia ya mwakani

Ilikua mwaka 1992 kwenye ligi ya Muungano wa mchangani hawakurudi uwanjani kipindi cha pili kwani walijua zitakua nyingi alikua kishapigwa goli mbili kwa kamoja kao.
.
na nyie je 2010 pale taifa hamkuleta tim kabisa
 
na nyie je 2010 pale taifa hamkuleta tim kabisa
Si afadhali sisi hatukuja kabisa,kuliko nyie mmekuja mmepigwa mkaweka mpira kwapani, hakuna jambo la aibu kwenye mpira kama kuweka mpira kwapani,na bado mtapigwa sana msimu ujao,umesikia ya Moro lakini? pole mzee mzima.
 

Leo Katika Historia:

Mnamo tar 3-08-2016,majira ya saa 10:30 Jioni.

Timu ya Simba SC imefungwa bao 1 na timu ya KMC (Vijana wa Mtaani/Manispaa)
 
Usizungumzie historia tu,na leo mmechapwa kagoli kamoja huko Morogoro na timu ya Manispaa ya Kinondoni(KMC FC) mpaka mkataka kupigana,ongeza ni na hiyo kwenye historia ya mwakani

Ilikua mwaka 1992 kwenye ligi ya Muungano wa mchangani hawakurudi uwanjani kipindi cha pili kwani walijua zitakua nyingi alikua kishapigwa goli mbili kwa kamoja kao.
.
Shukran kwa kujazia nyama sembo nadhani aliisahau hii natumaini ataiweka pia.
 
Back
Top Bottom