Lengo ni kuingo'a CCM au kuleta maendeleo?

Lengo ni kuingo'a CCM au kuleta maendeleo?

Zitto Kabwe siku hizi 'kaishiwa' kabisa.
Sio kama enzi zile ambapo asingeweza kuvumilia ufisadi ndani ya serikali.
Siku hizi kabaki kushambulia Chadema tu.
Sijamsikia akizungumzia ufisadi wa wazi kabisa kama huu hapa chini....
Katika ufisadi huu, Zitto 'alifumba macho' kabisa, hakuonekana wala kutoa tamko....

Bandari watumia bilioni 9.6 kikao cha siku moja! - Taarifa News

Siku hizi kamekuwa ni ka shock absorber ka ma ccm.

Hakana tofauti na mrema.

Kako tayari kujidhalilisha ili kudhibiti mchakato wa katiba mpya.
 
Let say umeenda hospitali ukaambiwa una kansa kwenye kidole inabidi kikatwe ili kansa isije kuenea mwili mzima.. halafu una muuliza dokta "hivi lengo lako ni kunikata kidole au kuzuia kansa isienee?

kuzuia kansa hapo ni kukata kidole... na hakuna maendeleo kabla ya ccm haijang'olewa..
 
Wameunganaje kama hawapatani? Walitokaje bungeni kwa pamoja kama hawapatani? Endelea kusubiri uone inawezekanaje. "ADUI WA ADUI YAKO NI RAFIKI YAKO"

Soma hii hapa chini
Hali si shwari kati ya CUF na Chadema, kutokana na vyama hivyo sasa kuamua kuoneshana ubabe hadharani.
Hatua hiyo inatishia usalama wa Watanzania kisiasa, kutokana na vitendo ambavyo vinadaiwa kufanywa au kusababishwa na wafuasi wa vyama vya siasa katika mikutano ya hadhara.
Na kama hali hii itaacha iendelee huku nchi ikielekea katika uchaguzi mkuu mwaka 2015, kuna hatari ya wananchi kudhuriana na kufanya mfumo wa siasa ya vyama vingi nchini kuonekana balaa kwa Taifa.
Baada ya vurugu kutokea katika mikutano ya Chadema chini ya Operesheni Sangara na kusababisha vifo vya watu wawili Morogoro na Iringa hivi karibuni, sasa kumezuka mtafaruku baina ya chama hicho na CUF.
Jana CUF iliituhumu Chadema na kuihadharisha, kuwa falsafa yake ya ‘ngangari' iliyokuwa ikiendeshwa dhidi ya Polisi inaweza kuhamishiwa dhidi ya Chadema na kusababisha ikose pa kukaa.
Tamko la CUF linatokana na kile ilichodai kwamba wafuasi wake walipondwa mawe na wale wa Chadema walipokuwa wakiendelea na shughuli za kutangaza mikutano inayoendelea mjini Arusha.
"CUF inatoa onyo kali kwa viongozi wa Chadema, kwamba hali hii ikiendelea, wajue hawataweza kufanya shughuli zao sehemu yoyote Tanzania, kwani uwezo wa kuwafanya tutakavyo tunao na kwa sababu wameanza tunaweza kumaliza," Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Haki za Binadamu wa CUF, Abdul Kambaya alisema hayo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.
Taarifa hiyo iliendelea kumnukuu: "Ile ngangari kwa Polisi tunaweza kuwahamishia wao na wakose pa kukaa, ila hatupendi tufike huko na kama wana busara na ni wanasiasa kweli wenye nia ya kutumia hoja badala ya vurugu kumkomboa Mtanzania, watafakari hilo."
Kwa mujibu wa Kambaya, CUF inaona Chadema kama chama kisichoweza siasa za ustahimilivu, haijiamini na ni changa kisiasa. "Hii inadhirishwa na kutoelewa maana ya demokrasia na uhuru wa Mtanzania kuamua kujiunga na chama chochote atakacho.
"Bado hawajakomaa kisiasa kama CUF ilivyokomaa kisiasa hatudhuru chama chochote kinapofanya siasa maeneo yoyote hapa nchini," alisisitiza.
CUF inatuhumu viongozi wa Chadema Arusha kushawishi wafuasi wao kuwaponda mawe wafuasi wake wanaoendelea na mikutano ya kisiasa tangu mwanzoni mwa wiki hii.
Kambaya alimtuhumu Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Godbless Lema kwamba juzi akihutubia wafuasi wa chama chake kwenye viwanja vya stendi ya Nduruma alisema ‘CUF wametuvamia' na kuwasihi kwa usemi wa ‘kamata mwizi men' uanze kutekelezwa.
Kwa mujibu wa taarifa ya CUF, vijana wao walipondwa mawe jana wakiwa mtaa wa Kilombero kata ya Levorosi. Inasema kutokana na vurugu hizo, gari la matangazo la CUF lilipondwa na mwanachama mmoja aliyetajwa kwa jina la Athumani Abdulrahman kujeruhiwa jicho na kwamba taarifa ziko Polisi.
Chama hicho kilisisitiza, kwamba kitaendelea na siasa Arusha hususan Operesheni Mchakamchaka na mikutano. "Kama wao ni wababe kweli na wanatumia hoja ya vurugu, waendelee na mipango yao ya hujuma na tutawafundisha siasa, kwani bado hawajakomaa," ilisisitiza taarifa ya Kambaya.
Gazeti hili lilimtafuta Lema ambaye alipata kuwa mbunge wa Arusha Mjini kabla ya Mahakama Kuu kubatilisha ubunge wake, kwa ajili ya kujibu shutuma za kushawishi vijana kuwafanyia vurugu wana CUF, lakini hakupatikana.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa alipotafutwa kujibu shutuma hizo za CUF dhidi ya chama chake, alisema yuko mkoani Mwanza hafahamu suala hilo. Alimtaka mwandishi kuwasiliana na viongozi wa chama walioko Arusha.
Aidha, Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene alisema hana taarifa ya suala hilo na akaomba apewe muda apate ukweli kabla ya kutoa majibu juu ya shutuma hizo za CUF.
chanzo: HATARI!! WAFUASI CUF, CHADEMA WAONESHANA UBABE MIKUTANONI... - ziro99blog
 
Wewe kwa mawazo yako unafikiri watanzania wataweza kupata maendeleo bila kung'oka CCM?

Kwa hiyo lengo kuu ni kwanza kutimiza azma ya kuitoa CCM madarakani, ili lengo la pili kuu, la kuwapatia maisha bora ya kikwelikweli watanzania, lipate kutimia!
 
Wewe kwa mawazo yako unafikiri watanzania wataweza kupata maendeleo bila kung'oka CCM?

Kwa hiyo lengo kuu ni kwanza kutimiza azma ya kuitoa CCM madarakani, ili lengo la pili kuu, la kuwapatia maisha bora ya kikwelikweli watanzania, lipate kutimia!
Vyma vya upinzani mbona vinachechemea?
 
Nawasalimia wana bodi.
Nimefuarahi sana vyama vya upinzani kuungana. Ni hatua moja ya maendeleo kisiasa.

View attachment 198919
Lakini pamoja na kuungana inapaswa kila kitu kuwekwa wazi ili kieleweke ni nini makubaliano halisi. Maana kunaugomvi mwingi umewahi kutoka hapo nyuma. Mfano mwaka jana 2013 kumekuwa na ugomvi baina ya CUF na CHADEMA:-



Kwa kweli inayaka moyo sana.
Ila pointi yangu ni kwamba je huu muungano wa vyama hivi ni wa kudumu au wa mda? kama ni wa kudumu kwa nini kila kitu kisiwekwe hadharani ili kila mmoja akaelewa.

Je lengo la hivi vya ni kung'oa CCM au kuleta maendeleo kwa wananchi?
Kama ni kimoja ni jinsi gani sasa watafikia lengo lao wakati bodo kuna watu wanavidonda vinauma havijapona na hatujaona wakisameheana?

Kukubaliana viongozi haitoshi maana huku mitaani wanachama wa CUF na CHADEMA hawapendani bado hawajaaelezwa ule utofauti uliojitokeza umeishaje? Maswali ni mengi sana.

Hivi chukulia wewe ni mwanachama wa CUF halafu wenje ndiye mgombea na unalazimishwa umchague wakati alikuita shogha!!! inakuja akilini kweli?

Mimi ninataka kujua huu umoja ni wa namna gani?

Halafu ikumbukwe mwaka 2010 baada ya kuunda kambi ya upinzani Mbowe alikataa kuwahusisha wenzake kwenye kambi ya upinzani na akataka yeye tu ndiye mpakwa mafuta. Na ikumbukwe kuwa CHADEMA sasa inapumulia oxygen kwa hiyo inatafuta kick kupitia kwa wazoefu wa siasa kama akina Lipumba na Mbatia watu waliozoea kugalaganzwa vibaya ili kujificchia aibu.

Na wana JF wekeni alini huu umoja baada ya 2015 kila mmoja ataanza kumlaumu mwenzake ndiye aliye sababisha kushindwa vibaya. Na ndio itakuwa mwisho wa CDM, CUF na NCCR.

MOU haijakaa vizuri kwani haijaeleza toauti zinamalizwaje? imejikita katika madaraka tu. Haina sera yoyote zaidi ya kujikita kwenye madaraka.

Lipumba hataki uongozi mdogo anataka mkubwa ndio mnataka agombee uraisi? Itakuwa ngumi mbaya ya usoni. Slaa je? itakuwaje. Hapa patachimbika Lipumba hatakubali hata siku moja.


Wapinzani siwaelewi kabisa lengo lenu, maana vuguvugu la utofauti ni kubwa mno.

Lengo no yote 2 yaani kuitoa CCM kwenye usukani na maendeleo kufuatia . Kazi kubwa na ngumu sana ni kuitoa CCM pale maendeleo ni mepesi maana , Tanzania ni tajiri hivyo inawezekana kwa kila kitu baada ya CCM kuwa nje .
 
Wakara wa SHETANI mwaka huu mna kazi.

LENGO KUU LA UKAWA ni kuiondoa CCM madarakani, SIMPLE AND CLEAR!

CCM ikishaondoka madarakani mambo mengine kama maendeleo yatafuata baadaye, maana CCM ndiyo kikwazo cha maendeleo yetu.
 
Huwezi kuleta maendeleo kama ccm iko madarakani. Cha kwanza ni kuing'oa ccm madarakani ndipo maendeleo yatapatikana
 
Wakara wa SHETANI mwaka huu mna kazi.

LENGO KUU LA UKAWA ni kuiondoa CCM madarakani, SIMPLE AND CLEAR!

CCM ikishaondoka madarakani mambo mengine kama maendeleo yatafuata baadaye, maana CCM ndiyo kikwazo cha maendeleo yetu.
Kwani UKAWA ndio nini?
 
WE MTOA MADA, NAKUJIBU KAMA IFUATAVYO:- ISIPONG'OKA CCM MAENDELEO ITAKUWA NDOTO KATIKA NCHI HII.
Ccm ni PAKA maendeleo ni PANYA, ILI PANYA AISHI LAZIMA PAKA AONDOLEWE TENA KWA NGUVU KAMA ILE YA MISRI, LIBYA n.k
 
Back
Top Bottom