issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,781
- 5,205
Lema 'pasua kichwa' CHADEMA[/h] * Kauli zake zadaiwa kuudhi wenzake
* Mbunge adai zinakidhalilisha chama
* Ashangaa baadhi kumwona kama shujaa
* Ataka chama kimuwajibishe, vinginevyo...
NA STEPHEN BALIGEYA, DODOMA
KAULI za majigambo zinazotolewa na mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema (CHADEMA), kwamba ataendelea kuhamasisha maandamano usiku na mchana, zimemweka kitanzani. Hatua hiyo inatokana na baadhi ya wabunge wa CHADEMA, kudai kuwa kauli na matendo ya Lema yamekuwa yakikidhalilisha chama hicho mbele ya umma.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, mbunge mmoja wa CHADEMA, amesema kuwa anakusudia kuwasilisha malalamiko ndani ya chama hicho juu ya kauli hizo. Hata hivyo, amesema anatarajia kupata wakati mgumu wakati wa kuwasilisha hoja, hivyo kutokana na viongozi wa juu kukaa kimya bila kumchukulia Lema hatua za kumrekebisha. "Ni mtu anayeshangaza sana, taswira yetu mbele ya jamii imechafuka, lakini jambo la kusikitisha viongozi wa juu wako kimya na wengine wanamchukulia kama shujaa," alisema mbunge huyo.
Ameongeza kuwa ni ngumu kwa viongozi na wabunge wa CHADEMA kujivua lawama za kuwa chama kisichojali maendeleo ya Watanzania na badala yake kuhamasisha fujo. "Kweli unaamua kuropoka mbele ya umma kwamba tutaandamana usiku na mchana, mpaka kieleweke, hivi tujiulize anataka kieleweke kitu gani wakati uchaguzi umekamilika?" alihoji.
Pia, ameeleza kushangazwa kwake na baadhi ya wabunge wenzake wa chama hicho kujigamba mbele ya Bunge kuwa vyama vingine navyo viitishe maandamano kama vitapata watu. "Huu ni upofu wa kisiasa, hivi unaweza kusema CCM wakiamua kufanya maandamano hawapati watu, na je, unataka kusema CUF wakiandamana hawapati watu? Waache kujidanganya," aliongeza.
Alisema iwapo vyama vingine vitakuwa na sera ya maandamano kama Chadema inavyotaka iwe, hakuna shaka nchi itakosa mwenyewe, kwani lazima kila mwananchi ana mapenzi na chama fulani, hivyo kusema hawatapata watu ni hadaa tupu.
"Hivi kama sisi tuna watu wengi kiasi hicho, tulishindwa nini kupata viti 50 ikilinganishwa na vile ilivyopata CCM? Pamoja na udhaifu tunaozungumzia, lakini ukweli unabaki kuwa CCM ndiyo chama chenye watu wengi na siku kikiamua kujibu mapigo patakuwa hapatoshi.
"Unajua siku ile tunajadili Muswada wa Katiba hapa Dodoma, aliamua kwenda kuhamasisha wanafunzi wa UDOM na kuwapa sh. 5,000 kila aliyekubali kuungana na fujo zake," aliongeza mbunge huyo.
Alisema pamoja na Mkuu wa Mkoa Dodoma, Dk. James Msekela, kueleza wanafunzi kuwa anajua mgomo na fujo zao yupo mwanasiasa (mbunge) nyuma, Lema alijitokeza papo hapo na kusema yeye ndiye aliyewafuata.
Kwa maelezo hayo, mbunge huyo anasema imefikia hatua watu wenye akili timamu wanaona kwamba, CHADEMA kinaongozwa na watu wasio na uchungu na Watanzania kutokana na matendo yanayoendelea.
"Tumekuwa tukiwasema viongozi wa CCM ambao kila kukicha wanakemeana, lakini kwetu hata kumuonya Lema juu ya kauli zake tumeshindwa na badala yake heshima ya chama inazidi kushuka," alisema.
Juzi jioni akichangia kwenye bajeti ya serikali kwa mwaka 2011/12, Lema alisema CHADEMA kitaendelea kuandamana usiku na mchana ili mradi taa ziwekwe barabarani.
"Tena nataka niwaambie kuwa mimi ndiye niliyezuia maiti Tarime wasizikwe na mwenzangu Tundu Lissu akaja kupigilia msumari wa mwisho," alijigamba Lema.
Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Lugola, alisema mbunge huyo amezoea kuzuia maiti wasizikwe, hivyo kuna siku atazuia hata maiti za watu wengine ambazo hazijatokana na vurugu kama za Tarime.
"Lema, kuna siku ukimaliza kugombea maiti wa Nyamongo, utagombea maiti wanaotokana na vifo vya kawaida, kwani itakuwa mazoea hivyo kuwa vigumu kuacha," alisema Lugola.
Source: UHURU
* Mbunge adai zinakidhalilisha chama
* Ashangaa baadhi kumwona kama shujaa
* Ataka chama kimuwajibishe, vinginevyo...
NA STEPHEN BALIGEYA, DODOMA
KAULI za majigambo zinazotolewa na mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema (CHADEMA), kwamba ataendelea kuhamasisha maandamano usiku na mchana, zimemweka kitanzani. Hatua hiyo inatokana na baadhi ya wabunge wa CHADEMA, kudai kuwa kauli na matendo ya Lema yamekuwa yakikidhalilisha chama hicho mbele ya umma.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, mbunge mmoja wa CHADEMA, amesema kuwa anakusudia kuwasilisha malalamiko ndani ya chama hicho juu ya kauli hizo. Hata hivyo, amesema anatarajia kupata wakati mgumu wakati wa kuwasilisha hoja, hivyo kutokana na viongozi wa juu kukaa kimya bila kumchukulia Lema hatua za kumrekebisha. "Ni mtu anayeshangaza sana, taswira yetu mbele ya jamii imechafuka, lakini jambo la kusikitisha viongozi wa juu wako kimya na wengine wanamchukulia kama shujaa," alisema mbunge huyo.
Ameongeza kuwa ni ngumu kwa viongozi na wabunge wa CHADEMA kujivua lawama za kuwa chama kisichojali maendeleo ya Watanzania na badala yake kuhamasisha fujo. "Kweli unaamua kuropoka mbele ya umma kwamba tutaandamana usiku na mchana, mpaka kieleweke, hivi tujiulize anataka kieleweke kitu gani wakati uchaguzi umekamilika?" alihoji.
Pia, ameeleza kushangazwa kwake na baadhi ya wabunge wenzake wa chama hicho kujigamba mbele ya Bunge kuwa vyama vingine navyo viitishe maandamano kama vitapata watu. "Huu ni upofu wa kisiasa, hivi unaweza kusema CCM wakiamua kufanya maandamano hawapati watu, na je, unataka kusema CUF wakiandamana hawapati watu? Waache kujidanganya," aliongeza.
Alisema iwapo vyama vingine vitakuwa na sera ya maandamano kama Chadema inavyotaka iwe, hakuna shaka nchi itakosa mwenyewe, kwani lazima kila mwananchi ana mapenzi na chama fulani, hivyo kusema hawatapata watu ni hadaa tupu.
"Hivi kama sisi tuna watu wengi kiasi hicho, tulishindwa nini kupata viti 50 ikilinganishwa na vile ilivyopata CCM? Pamoja na udhaifu tunaozungumzia, lakini ukweli unabaki kuwa CCM ndiyo chama chenye watu wengi na siku kikiamua kujibu mapigo patakuwa hapatoshi.
"Unajua siku ile tunajadili Muswada wa Katiba hapa Dodoma, aliamua kwenda kuhamasisha wanafunzi wa UDOM na kuwapa sh. 5,000 kila aliyekubali kuungana na fujo zake," aliongeza mbunge huyo.
Alisema pamoja na Mkuu wa Mkoa Dodoma, Dk. James Msekela, kueleza wanafunzi kuwa anajua mgomo na fujo zao yupo mwanasiasa (mbunge) nyuma, Lema alijitokeza papo hapo na kusema yeye ndiye aliyewafuata.
Kwa maelezo hayo, mbunge huyo anasema imefikia hatua watu wenye akili timamu wanaona kwamba, CHADEMA kinaongozwa na watu wasio na uchungu na Watanzania kutokana na matendo yanayoendelea.
"Tumekuwa tukiwasema viongozi wa CCM ambao kila kukicha wanakemeana, lakini kwetu hata kumuonya Lema juu ya kauli zake tumeshindwa na badala yake heshima ya chama inazidi kushuka," alisema.
Juzi jioni akichangia kwenye bajeti ya serikali kwa mwaka 2011/12, Lema alisema CHADEMA kitaendelea kuandamana usiku na mchana ili mradi taa ziwekwe barabarani.
"Tena nataka niwaambie kuwa mimi ndiye niliyezuia maiti Tarime wasizikwe na mwenzangu Tundu Lissu akaja kupigilia msumari wa mwisho," alijigamba Lema.
Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Lugola, alisema mbunge huyo amezoea kuzuia maiti wasizikwe, hivyo kuna siku atazuia hata maiti za watu wengine ambazo hazijatokana na vurugu kama za Tarime.
"Lema, kuna siku ukimaliza kugombea maiti wa Nyamongo, utagombea maiti wanaotokana na vifo vya kawaida, kwani itakuwa mazoea hivyo kuwa vigumu kuacha," alisema Lugola.
Source: UHURU