Lema mwanasiasa Bora wa Mwaka 2011

Lema mwanasiasa Bora wa Mwaka 2011

Ni ukweli usiopingika kuwa Godbless Lema amekuwa ni mwanasiasa mwenye kuibua mijadala mingi hapa nchini, ndani na nje ya bunge. Kwa uchache utaungana nami kukumbuka hotuba ya waziri kivuli wa mambo ya ndani aliyoitoa bungeni ilivyovuta hisia za watanzania wengi. Bila kusahau tamko lake lililopinga mwafaka uliofikiwa kati ya madiwani wa CCM na Chadema Arusha na kupelekea madiwani hao kufukuzwa Chadema.

Ni hivi majuzi tu ametoa waraka wake kuhusu kufukuzwa Kafulila unavyojadiliwa hadi leo hii. Ukiachilia mbali misukosuko yake na harakati za kuwasaidia wananchi wa jimbo lake la Arusha mjini hadi kupelekea kuwekwa rumande kwa wiki mbili, vile vile tumejulishwa Lema amepata tuzo yamwanasiasa bora na jasiri kijana kutoka blog moja nchini na kuwashinda wanasiasa wengine machachari waliotamba mwaka jana kina Zitto, January na Mnyika anayeibukia kwa sasa. Kwa vigezo hivi sina budi kabisa kusema GL amekuwa mwanasiasa bora wa Mwaka huu tunaomaliza wa 2011, nafikiri utakubaliana nami.



Luteni,

Je unajuwa ni kuwa jimbo lake la Arusha mjini halina hata Kilometer moja ya Lami.

Je Lema ameshaweka lami japo hata Km Moja tokea aingie madarakani? Je maendeleo gani aliyowaletea wapiga kura wake? mpaka awe mwanasiasa bora?
 
Naona bado unachanganya mambo Mkuu. Hayo unayoyataja yalikuwa kwenye Ilani ya Uchaguzi katika Jimbo la Arusha kwa upande wa CDM. Lakini inapaswa uelewe kwamba CCM wamecheza rafu kwenye uchaguzi wa Meya na kwa mantiki hiyo Ilani inayotekelezwa si ya LEMA (CDM) tena bali ni ile aliyokuwa anainadi Batilda Buriani kwa niaba ya Chama chake kwa Jimboa la Arusha! Nasisitiza, tusipotoshe hoja!

Naomba kueleweshwa, ina maana huu mgogoro wa umeya ukidumu kwa miaka mingine 4 ndo kusema ahadi nyingi za mbunge hazitatekelezwa? Nadiriki kusadiki kwamba wakati huku CDM wakiendekeza mgogoro huku wakisusia vikao vya madiwani, wenzao kule wanatekeleza ahadi zao kwenye kata zao. sijui CDM watawaambia nini wapiga kura wao mwaka 2015. Ingalikuwa bora kutumia akili na weledi mkuu kumaliza tatizo la umeya kwa faida ya wananchi wa Arusha.
Kumbuka hapa ni mafahali CCM na CDM wanagombana kwa maslahi yao na wanaoumia ni wananchi.
 
Luteni,

Je unajuwa ni kuwa jimbo lake la Arusha mjini halina hata Kilometer moja ya Lami.

Je Lema ameshaweka lami japo hata Km Moja tokea aingie madarakani? Je maendeleogani aliyowaletea wapiga kura wake? mpaka awe mwanasiasa bora?
Si kweli, nafikiri wewe hujafika Arusha ukitoka Oman usiishie Kibandamaiti tu njoo A-town ujionee maendeleo.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Godbless Lema amekuwa ni mwanasiasa mwenye kuibua mijadala mingi hapa nchini, ndani na nje ya bunge. Kwa uchache utaungana nami kukumbuka hotuba ya waziri kivuli wa mambo ya ndani aliyoitoa bungeni ilivyovuta hisia za watanzania wengi. Bila kusahau tamko lake lililopinga mwafaka uliofikiwa kati ya madiwani wa CCM na Chadema Arusha na kupelekea madiwani hao kufukuzwa Chadema.

Ni hivi majuzi tu ametoa waraka wake kuhusu kufukuzwa Kafulila unavyojadiliwa hadi leo hii. Ukiachilia mbali misukosuko yake na harakati za kuwasaidia wananchi wa jimbo lake la Arusha mjini hadi kupelekea kuwekwa rumande kwa wiki mbili, vile vile tumejulishwa Lema amepata tuzo yamwanasiasa bora na jasiri kijana kutoka blog moja nchini na kuwashinda wanasiasa wengine machachari waliotamba mwaka jana kina Zitto, January na Mnyika anayeibukia kwa sasa. Kwa vigezo hivi sina budi kabisa kusema GL amekuwa mwanasiasa bora wa Mwaka huu tunaomaliza wa 2011, nafikiri utakubaliana nami.

MAGWANDA at work.
 
Sidhani kwangu mimi lema hes the guy who keep sticking his nose where it doesn't belong...! hadi mambo ya NCCR anayaingilia yeye ...na waraka katoa kabisa .. mbana anahangaika sana hivi....! wanasiasa bora huwa wapo kimya saana wanafanya mambo kimya na yakaonekana... Mh january makamba nendeni jimboni kwako mkajionee mambo anayoyafanya na anayotarajia kuyafanya ...
 
Sidhani kwangu mimi lema hes the guy who keep sticking his nose where it doesn't belong...! hadi mambo ya NCCR anayaingilia yeye ...na waraka katoa kabisa .. mbana anahangaika sana hivi....! wanasiasa bora huwa wapo kimya saana wanafanya mambo kimya na yakaonekana... Mh january makamba nendeni jimboni kwako mkajionee mambo anayoyafanya na anayotarajia kuyafanya ...
Hao si wanasiasa ni wafanyabiashara.
 
Luteni,
Je Lema ameshaweka lami japo hata Km Moja tokea aingie madarakani? Je maendeleo gani aliyowaletea wapiga kura wake? mpaka awe mwanasiasa bora?

Jamani tutofautishe kazi za Mbunge, kazi za Serikali Kuu na kazi za Halmashauri! Lema kama Lema si kazi yake kuweka Lami. Hiyo ni kazi ya taasisi husika ambazo kwa sasa zipo chini ya Uongozi wa CCM!

 
Vigezo vingine vya kizuzu ndivyo vilivyotufikisha hapa hadi tukampata kiongozi tuliye naye ndani ya taifa letu hivi sasa....Sijui watanzania tuna tatizo la kugeuza priorities upside-down au ni nini hasa ! Sijui ubora wa mbunge unajikita katika logic zipi hasa,labda kama tunaangalia quantity ya matukio.

Anyways tunafuata vigezo vile vile wanavyotumia hata wasomi wa hovyo(wasomi wanao-compromise taaluma zao ili kujikomba kwa mkuu wa nchi hata kumpatia udaktari wa falsafa) katika mazingira tatanishi.Naona dalili ya great thinkers kutumia vigezo kama vile vilivyotumika kumpa JK uongozi wa juu 2005 hadi kufikia 80%,naona tunatumia vigezo vile vile vilivyotupatia akina maji marefu bungeni ....pengine vigezo vilivyotupatia akina Lusinde.Tuna safari ndefu
Ben

Ok mkuu hivi ni vigezo vya kizuzu lakini angalau mimi nimeviona unaweza kutupavigezo vyako vya kisomi,
 
Mkuu Ben.

Kama Lema ni mwanasiasa bora wa mwaka 2011 hakuna haja ya kushangaa kwanini Tanzania ni masikini wa kutupwa pamoja na kuwa na utajiri mkubwa wa Madini,Ardhi kubwa,Mito mikubwa,mabwawa na maziwa kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji,malihasili mbuga za wanyama na nk.

Tunampataje kiongozi bora ?.

[1] Maandamano yasiyo na maana ?.

[2] Kususa dhamana ?.

[3] Kuombea maiti ifufuke ?.

[4] Kupigiwa kura na mashabiki kwenye blog ambayo mtu mmoja anaweza kupiga kura mara 100,000,000 ?.

Mitanzania mijitu ya ajabu kweli ndiyo maana mlidanganywa na maaskofu Kikwete chaguo la Mungu mkaingia kichwa kichwa mkamchagua kwa 80% ?.
Yote uliyotaja kasoro no. 3 ni siasa.
 
Nadiriki kusadiki kwamba wakati huku CDM wakiendekeza mgogoro huku wakisusia vikao vya madiwani, wenzao kule wanatekeleza ahadi zao kwenye kata zao. sijui CDM watawaambia nini wapiga kura wao mwaka 2015. Ingalikuwa bora kutumia akili na weledi mkuu kumaliza tatizo la umeya kwa faida ya wananchi wa Arusha.

Ndugu yangu kumbuka kwamba kutekeleza ahadi ulizowaahidi wapiga kura sio kigezo pekee cha kuchaguliwa tena!
 
Mkuu TUMBIRI,

Godbless Lema ni mbunge ana wajibu mkubwa wa kutuondoa kwenye umasikini kama wewe Tumbiri ulivyo na nafasi ya Baba / Mama haijalishi kama umeshika madaraka ya kisiasa au lah.Lema ni mbunge kachaguliwa na wananchi wengi ambao walitegemea atatekeleza mambo yote aliyoahidi wakati akiomba kura.Zipo ahadi nyingi labda tuzichukue zile alizotoa kupitia mchakato majimboni kwakuwa kila mtanzania alizisikia.

[1] Alisema atajenga Hospital tatu !.Nina uhakika ukimuuliza akuonyeshe walau kiwanja kimoja kwaajili ya ujenzi wa hiyo Hospital anaweza kuanzisha maandamano ya kupinga kuulizwa alichoahidi.

[2] Alisema atajenga Machinga Complex nakumbuka mmoja wa washindani wake alitoa tahadhari kwa wananchi kuchunguza baadhi ya ahadi za wagombea kwakuwa ahadi nyingine ni vigumu kutekelezwa na mbunge Lema akasema anajua fedha zitatoka wapi.Leo hii ukimuuliza mipango ya machinga complex imefikia wapi atakuuliza mbona Kikwete katoa ahadi kibao utekelezaji zero.
Mzee Ngongo kazi za mbunge ni zipi inawezekana unachanganya kazi za serikali na halimashauri za miji.
 
Jamani tutofautishe kazi za Mbunge, kazi za Serikali Kuu na kazi za Halmashauri! Lema kama Lema si kazi yake kuweka Lami. Hiyo ni kazi ya taasisi husika ambazo kwa sasa zipo chini ya Uongozi wa CCM!



Tumbiri.

Naomba ujue siku zote wananchi hawataki malumbano bali wanataka maendeleo. Na Mbunge ndio mwenye dhima kubwa sana katika kuchochea maendeleo ya jimbo lake akishirikiana na wananchi wake. Kwani ni yeye anawawakilisha wapiga kura wake ndani ya chombo kikuu cha kutunga sheria na kupatisha bajeti ya nchi.

sasa tuweke wazi je amewasaidia nini wananchi wake?
 


kwa hiyo luten kwako wewe mwanasiasa bora ni yule ambaye ni VUVUZELA ...
Siasa na uanasiasa ni kazi ya kumobilize watu kujiletea maendeleo yao wenyewe, sasa wewe ukianza kujenga barabara au hospitali kimya kimya kwa kutumia hela zako hiyo si siasa ni biashara unawekeza ili baadae uvune na ndicho kinachowashinda wanasiasa wengi tanzania kama kina RA.
 
Ndugu yangu kumbuka kwamba kutekeleza ahadi ulizowaahidi wapiga kura sio kigezo pekee cha kuchaguliwa tena!

Watakuchagua tu kama watakuelewa, isije ikaja semwa ya Heri ya Misri kuliko kuishi hapa Jangwani. angalizo tu mkuu, wananchi wa huku kwetu Maganjo wanasema hapendwi mbunge bali maendeleo.
 
Si kweli, nafikiri wewe hujafika Arusha ukitoka Oman usiishie Kibandamaiti tu njoo A-town ujionee maendeleo.


Feedback,

Tunaijua vizuri sana Arusha na nimepita mwezi huu mwanzoni nikitokea mwanza. lakini tuweke wazi . Je manispaa ya Arusha mjini ina barabara ya Lami? Tutajie basi ni bara gani hiyo la Lami inayomilikiwa na manispaa ya Arusa mjini? Kumbuka kuna barabara zinazomilikiwa na TANROAD.

sasa tubainishie na unitakie barabara zinazomilikiwa na manispaa ya arusha mjini yenye lami?

nasubiri jibu hapa.
 
Luteni,

Je unajuwa ni kuwa jimbo lake la Arusha mjini halina hata Kilometer moja ya Lami.

Je Lema ameshaweka lami japo hata Km Moja tokea aingie madarakani? Je maendeleo gani aliyowaletea wapiga kura wake? mpaka awe mwanasiasa bora?
Mzee mimi naishi Arusha wewe unaishi wapi.
 
Back
Top Bottom