Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,323
Ni ukweli usiopingika kuwa Godbless Lema amekuwa ni mwanasiasa mwenye kuibua mijadala mingi hapa nchini, ndani na nje ya bunge. Kwa uchache utaungana nami kukumbuka hotuba ya waziri kivuli wa mambo ya ndani aliyoitoa bungeni ilivyovuta hisia za watanzania wengi. Bila kusahau tamko lake lililopinga mwafaka uliofikiwa kati ya madiwani wa CCM na Chadema Arusha na kupelekea madiwani hao kufukuzwa Chadema.
Ni hivi majuzi tu ametoa waraka wake kuhusu kufukuzwa Kafulila unavyojadiliwa hadi leo hii. Ukiachilia mbali misukosuko yake na harakati za kuwasaidia wananchi wa jimbo lake la Arusha mjini hadi kupelekea kuwekwa rumande kwa wiki mbili, vile vile tumejulishwa Lema amepata tuzo yamwanasiasa bora na jasiri kijana kutoka blog moja nchini na kuwashinda wanasiasa wengine machachari waliotamba mwaka jana kina Zitto, January na Mnyika anayeibukia kwa sasa. Kwa vigezo hivi sina budi kabisa kusema GL amekuwa mwanasiasa bora wa Mwaka huu tunaomaliza wa 2011, nafikiri utakubaliana nami.
Luteni,
Je unajuwa ni kuwa jimbo lake la Arusha mjini halina hata Kilometer moja ya Lami.
Je Lema ameshaweka lami japo hata Km Moja tokea aingie madarakani? Je maendeleo gani aliyowaletea wapiga kura wake? mpaka awe mwanasiasa bora?