Learned brothers comeon!!!!!!!!!!!

Learned brothers comeon!!!!!!!!!!!

Joined
Feb 20, 2011
Posts
13
Reaction score
8
Jamani tujitokeze na tutoe ufafanuzi juu y dhana nzima ya kutojadili swala lililoko mahakamani...ongezeko la kuitumia mahakama kama kivuli inanitia kinyaa na niaibu kwa wanasheria nchini. Kwa nini katika maswala mazito mara moja tunakimbilia mahakamani na kudai tunaheshimu sana mhimili huo kwa kutozungumzia swala lililoko mahakamani? wimbi hili la kukimbilia mahakamani limeongezeka sana kipindi hiki hadi kufungua mashauri ambayo sio ya msingi kama hili la mwendawazimu halafu tunakatazwa kujadili kwa kina swala zima. Ila what i believe siku moja mahakama zetu tukufu pamoja na wanasheria weledi watatoa ufafanuzi kwa jamii ni kipindi gani na swala gani lililoko mahakamani halijadiliki? Ni hayo tu.
 
Mahakama ndiyo siraha ya mwisho kwa CCM baada ya hapo watakuwa hawana, huu ni upepo utapita tu na mahakama itarudi ktk mstari, ma-RC, MDC na baadae polisi, baadaye TISS na JWTZ, magereza, wote hawa wamechemsha na sasa wanamalizia na bunge kwa bi makinda na mahakama.Baada ya hapo tutawakamata kama kuku kwa kutumia nguvu ya umma.Wammulize ALSAAD ametumia hadi silaha za sumu lakini kilichompata jana BBC News - Syria: Hunting for President Assad's assets
 
Jamani tujitokeze na tutoe ufafanuzi juu y dhana nzima ya kutojadili swala lililoko mahakamani...ongezeko la kuitumia mahakama kama kivuli inanitia kinyaa na niaibu kwa wanasheria nchini. Kwa nini katika maswala mazito mara moja tunakimbilia mahakamani na kudai tunaheshimu sana mhimili huo kwa kutozungumzia swala lililoko mahakamani? wimbi hili la kukimbilia mahakamani limeongezeka sana kipindi hiki hadi kufungua mashauri ambayo sio ya msingi kama hili la mwendawazimu halafu tunakatazwa kujadili kwa kina swala zima. Ila what i believe siku moja mahakama zetu tukufu pamoja na wanasheria weledi watatoa ufafanuzi kwa jamii ni kipindi gani na swala gani lililoko mahakamani halijadiliki? Ni hayo tu.

Tanganyika Law Society mpo?
 
Ok. Kwa mujibu wa katiba yetu, mahakama inapaswa kuwa huru. Iweze kutoa haki bila woga wala upendeleo (without fear or favour). Hivyo dhana ya kutojadili mambo yaliyoko mahakamani ina lenga kutokuathiri mwenendo wa kesi. Hata hivyo linalozuiwa ni kujadili (kujenga hoja juu ya mwenendo wa kesi/kujadili jinsi kesi inavyoendeshwa) na siyo kuzuia mtu kutaja matukio yaliyowahi kutokea ambayo yameripotiwa mahakamani. Mfano, huwezi kumzuia mke wa msigwa asiseme mumewe amewahi pigwa. Hivyo upinzani kulaani matukio yaliyofikishwa mahakamani, mf utesaji wa ulimboka, hakuingilii uhuru wa mahakama. Tatizo ni uchama, ambapo hata AG amesahau kuwa amewahi kuwa jaji badala yake anaact kama katibu mwenezi wa shina flani la ccm!
 
Back
Top Bottom