Kitchener
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 13,823
- 27,694
Ni hoja niliyojiuliza, kwamba watu hawatakiwi kuabudu hata sehemu zingine, walau hata kukodi ukumbi ili kujifunza Neno la Mungu bila kwenda maeneo waliyozungushia utepe, kwa hiyo ile haki yao ya kuabudu imesimamishwa hadi kesi itakapoisha hata kama ni miaka 10? ndivyo katiba inavyotaka ilipotoa uhuru wa kuabudu?
Pia najua uhuru wako unaopewa na katiba hautakiwi kuvunja haki za watu wengine, nikawa najiuliza hawa watu wanaoenda kupigwa virungu leo baada ya msando kuwafukuza na kwenye ukumbi waliokodi kukusanyika kwa amani tu, vitendo vyao vimevunja haki ya nani ili pengine tuseme wasikusanyike kwani watadhuru haki za wengine?
Pia najua uhuru wako unaopewa na katiba hautakiwi kuvunja haki za watu wengine, nikawa najiuliza hawa watu wanaoenda kupigwa virungu leo baada ya msando kuwafukuza na kwenye ukumbi waliokodi kukusanyika kwa amani tu, vitendo vyao vimevunja haki ya nani ili pengine tuseme wasikusanyike kwani watadhuru haki za wengine?