Lalamiko langu kwa shule za Tanzania kulazimisha wanafunzi kusoma masomo ya Dini

ASIWAJU

JF-Expert Member
Nov 18, 2022
1,939
1,625
Habari za saa nyote natumai ni njema, moja kwa moja wacha niende katika jambo lililonifanya niandike lalamimiko langu.

Lalamiko langu linaenda kwa shule za msingi na upili katika taifa letu la Tanzania kuhusu suala la ulazimishaji wa vipindi vya dini kwa wanafunzi tena kwa kuwachapa viboko wale wote waliogoma kuhudhuria vipindi hivyo.

Imefika wakati dini kuonekana ni jambo la lazima kwa mwanafunzi wakati katiba ya taifa letu haielezi hilo.

: Kwanini uongozi wa shule mbalimbali za misingi na upili kwa hapa nchini zimefanya dini kuwa kipindi cha lazima pasipo kujali uhuru wa mtu kuwa muumini wa dini au la ?

Dini ni suala la hiari lakini hapa taifani kwetu katika shule za misingi na upili dini imechukuliwa kama ni suala lazima.

: Kwanini uhuru wa kimaamuzi wa wenye dini umezingatiwa lakini wa wasio na dini umefunikwa kwa viboko vikali na adhabu kali kutoka katika viongozi/ walimu wa shule ?

Mimi mwenyewe mleta lalamiko nilipata kuwa muathirika wa hili swala wakati wa uanafunzi wangu jambo lililo niletea kero kubwa kwangu.

: Kwanini wanafunzi wasiotaka kujishughulisha na masuala ya kidini wasipewe uhuru wao wa kufanya hivyo ? Kwanini iwe ni lazima kwa wanafunzi wote kushiriki vipindi hivyo ?

Ni hilo tu lalamiko langu kwa shule za Tanzania kuhusu lazimisho la kushiriki vipindi vya dini kwa wanafunzi pasipo kuzingatia uhuru wao wa kimaamuzi, ningependa kuona shule zote za taifa letu zikiji rekebisha kuhusu hili swala.
 
Awatoto walazimishwe dini. Kuna vitu vinapozwa makali na dini, waende tu
Kwa nini uhuru binafsi hau zingatiwi na kwa nini iwe ni lazima kushiriki hivyo vipindi tena kwa viboko na adhabu usipo fanya hivyo ?
 
Solution ni kumuhamishia shule isiyokua na vipindi vya dini
Shule nyingi za kiserikali zimetawaliwa na hivyo vipindi kwa hiyo ni swala gumu kutekelezeka hilo jambo, kwa nini isiwe kwa shule za kiserikali kujirekebisha ? Maana hili taifa letu ni la wote wenye kupendezwa na dini na wale wasiopendezwa nazo.
 
Kwani wewe huna dini? Huoni kuwa ndiyo mwanzo mzuri wa malezi kwa mtoto? Unazani watafundishwa wakiwa watu wazima? Kwa viboko hapana inatakiwa kuongea na wazazi wao ili waongee na watoto wao.
 
Kwani wewe huna dini? Huoni kuwa ndiyo mwanzo mzuri wa malezi kwa mtoto? Unazani watafundishwa wakiwa watu wazima? Kwa viboko hapana inatakiwa kuongea na wazazi wao ili waongee na watoto wao.
Kwa nini iwe ni swala la lazima wakati imani ni swala la mtu binafsi ?
 
Unakutana na wanafunzi wametoka kwenye familia za kidini wanaanza kuweka ratiba za maombi ya mfungo kila kidato,kila siku saa 4 kuna maombi, n.k.

kiongozi wangu wa maombi alikuwa anasema malengo yake ni kupata one ya 7 halafu alikuwa active sana kwenye mambo ya kidini kufunga,kuhubiri bila kusahau maombi ya saa 4 ila mwisho necta alipata div 3 ya mwishoni.
 
Ubaya zaidi ni kwamba uongozi wa shule huwa hawana control ya kile kinachofundishwa mule.
 
Hawa ndo wazazi wanaolea watoto. Kuna shida gani mtoto wako akifundishwa mambo mema? Kama kupendana na wenzake, kumuamini Muumba wake etc! Au kuna wazazi ni wachawi haya mafundisho yanawasumbua. Usijali mtoto akirudi nyumbani ataendelea kuruka na nyungo.

Subiri akirudi nyumbani utaendelea kumfundisha kuhusu upanya road. Si wako umemzaa
 
Ukifika miaka 18 ndio unakuwa na UHURU wa kuchagua aina ya maisha uitakayo, sababu bado wewe ni mtoto upo chini ya uangalizi ukiachwa ujikuze utakuwa panyaroad kisha utakuwa kero kwa Jamii na ni hatari kwa maisha yako utauwawa.
 
Back
Top Bottom