Labda waje wazungu watuhesabie kura

Labda waje wazungu watuhesabie kura

MI napata wasiwasi na mambo ya kupiga na kuhesabu kura na baadae kupata matokeo halisi..maana kuna tafiti zilizofanyika hivi karibuni na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu pamoja na asasi nyingine nyingo hivi zinalalamikia kutojitokeza kwa wingi wa kutosha kwa wananchi kupiga kura. KAtika madokezo yao wamegundua kuwa wananchi hasa wale ambao ni wa kati..yaani hawana ushabiki wa vyama vya siasa ambao ni asilimia zaidi ya 75 hawapigi kura katika chaguzi mbalimbali nchini kwa sababu hawajawahi kupata matokeo sahihi ya kura zao na pia hawajaona mabadiliko kutoka kwa viongozi wanaomchagua. Hivyo basi wengi wa wapiga kura ni wanachama wa vyama vya siasa na wale wa msimamo mkali na wapingaji tu ambao ni wachache.sijajua tatizo ni kuhesabu kura ama ni nini!!
 
Back
Top Bottom