KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 10,569
- 21,075
P
Watu wengi huteseka kiroho na kimwili kwa matatizo mbalimbali huku wengine wakidhani kurogwa wengine wakidhani wameibiwa ama kuchafuliwa nyota lakini watu wengi husahau juu ya laana ambazo zimetokana na koo zao ama wazazi wao
Kama watangulizi wetu ama ndugu zetu ama wazazi wetu kuna makosa walifanya huko nyuma na basi haya ndiyo huathiri hadi watoto wetu kiroho na kimwili kwa maana haya makosa hugeuka kuwa maagano ndani yetu na hutusumbua sisi na maisha yetu
Ikiwa wazazi wetu walifanya kosa la kiroho basi hilo kosa huja hadi kwa watoto na kuathiri katika maisha yao, moja ya makosa ambayo yanabakia hadi pale yanapovunjwa ni kama agano la damu ambalo hilo linahusisha chale, kafara, kuna hirizi za maagano na kuna makosa mengine ambayo hubakia katika mnyororo ndani yetu na yasipovunjwa hugeuka kama kiumbe mbaya na katali sana asiye na huruma na huyo kiumbe huja kumaliza famili na kizazi kijacho.
Makosa kama vile kwenda kwa mganga kumroga mwenzako bila sababu yoyote basi kosa hilo hugeuka na kuwa agano kwa maana nafsi ya mtendewa huanza kulia na kusononeka hivyo yale masononeko yake ni kama agano la damu ambalo taratibu hukua ndani yako na mwishowe utadaiwa na ikiwa haupo duniani basi kizazi chako watadaiwa tu.
Kuna watu wanakwenda kwa wataalam na kwenda kuondoa uhai wa fulani ama unakwenda kumfunga fulani kisa wivu ama tamaa ya kidunia basi kumbuka yale yote unayoyafanya ni kama kioo ndani yako kinamulika na kuyatunza ambapo baadaye hugeuka na kuwa agano ambalo litakusumbua wewe na kizazi chako
Unapokwenda kwa mtaalam kuchanjwa chale kumbuka ni kama kufanya ibada ya kafara na ibada ya kafara lazima utoe sadaka takatifu na hii sadaka takatifu ni damu basi tambua kwa kuchanjwa chale kwako ni ibada kamili ya kafara wewe ni sawa na aliyetoa kafara ya mtu hivyo taratibu unajenga agano ambalo litakusumbua wewe ama kizazi chako na hili ndilo huwasumbua watu wengi maana wazazi wao walifanya haya maagano huko nyuma hivyo lazima wajitoe katika maagano hayo ndipo nafsi zao zitulie...
Maagano ni sawa na makubaliano au mkataba na maagano yapo ya aina nyingi sana kuanzia kafara, chale, punyeto, kujichua, kuuza nafsi ya mwenzako,kumfunga mwenzako, kumroga yote ni maagano
Kuchepuka nje ya ndoa nako ni agano kamili ambalo itabidi lisafishwe kikamilifu na ujitoe katika hiyo kamba
Mara nyingi unasikia watu wanalalamika kuhusu tabia za watoto "huyu mtoto tabia kaichukua wapi, mbona baba na mama yake au ukoo wao hawako hivyo?". Chanzo cha tabia za ajabuajabu za watoto ni matokeo ya michepuko iliyofanya maagano na watu/koo zingine zenye laana. Laana na matatizo yanayoletwa na agano la damu katika familia havihitaji mtu kuchepuka na kuzaa nje ya ndoa, bali tu kuhusiana katika mapenzi!
Iko hivi kukutana kimwili na mtu mwenye maagano ya damu basi tambua na wewe ni sehemu ya maagano kwa maana ndigi ni kwamba mtu mchafu kiroho ukikutana naye na wewe ni sehemu ya huo uchafu
Maagano yanayofanywa na watu kwa njia ya kukutana kimwili na mtu mwenye maagano huenda vizazi hadi vizazi yaani kutoka kizazi hadi kizazi hubebwa na viashilia vilivyopo katika damu, mfano DNA hivyo hii ni hatari sana na inatisha na haya ndiyi huwasumbua watu wengi sana
Maagano ya kukutana kimwili na mtu mwenye maagano ya damu hii inawaathiri sana watoto na sio wahusika maana watoto ndo muunganiko wa damu mbili.
Ukifanya ngono na mtu mwenye mapepo huwa yanahamia pia kwako na kufanya agano nawe na kuathiri nyota yako.
Kumbuka kwamba nyota zina athari ya moja kwa moja katika maisha yetu na yeyote asiyefuata nyota yake hawezi kamwe kusonga mbele kwa maana anaishi nje ya asili yake
Watu wengi huteseka kiroho na kimwili kwa matatizo mbalimbali huku wengine wakidhani kurogwa wengine wakidhani wameibiwa ama kuchafuliwa nyota lakini watu wengi husahau juu ya laana ambazo zimetokana na koo zao ama wazazi wao
Kama watangulizi wetu ama ndugu zetu ama wazazi wetu kuna makosa walifanya huko nyuma na basi haya ndiyo huathiri hadi watoto wetu kiroho na kimwili kwa maana haya makosa hugeuka kuwa maagano ndani yetu na hutusumbua sisi na maisha yetu
Ikiwa wazazi wetu walifanya kosa la kiroho basi hilo kosa huja hadi kwa watoto na kuathiri katika maisha yao, moja ya makosa ambayo yanabakia hadi pale yanapovunjwa ni kama agano la damu ambalo hilo linahusisha chale, kafara, kuna hirizi za maagano na kuna makosa mengine ambayo hubakia katika mnyororo ndani yetu na yasipovunjwa hugeuka kama kiumbe mbaya na katali sana asiye na huruma na huyo kiumbe huja kumaliza famili na kizazi kijacho.
Makosa kama vile kwenda kwa mganga kumroga mwenzako bila sababu yoyote basi kosa hilo hugeuka na kuwa agano kwa maana nafsi ya mtendewa huanza kulia na kusononeka hivyo yale masononeko yake ni kama agano la damu ambalo taratibu hukua ndani yako na mwishowe utadaiwa na ikiwa haupo duniani basi kizazi chako watadaiwa tu.
Kuna watu wanakwenda kwa wataalam na kwenda kuondoa uhai wa fulani ama unakwenda kumfunga fulani kisa wivu ama tamaa ya kidunia basi kumbuka yale yote unayoyafanya ni kama kioo ndani yako kinamulika na kuyatunza ambapo baadaye hugeuka na kuwa agano ambalo litakusumbua wewe na kizazi chako
Unapokwenda kwa mtaalam kuchanjwa chale kumbuka ni kama kufanya ibada ya kafara na ibada ya kafara lazima utoe sadaka takatifu na hii sadaka takatifu ni damu basi tambua kwa kuchanjwa chale kwako ni ibada kamili ya kafara wewe ni sawa na aliyetoa kafara ya mtu hivyo taratibu unajenga agano ambalo litakusumbua wewe ama kizazi chako na hili ndilo huwasumbua watu wengi maana wazazi wao walifanya haya maagano huko nyuma hivyo lazima wajitoe katika maagano hayo ndipo nafsi zao zitulie...
Maagano ni sawa na makubaliano au mkataba na maagano yapo ya aina nyingi sana kuanzia kafara, chale, punyeto, kujichua, kuuza nafsi ya mwenzako,kumfunga mwenzako, kumroga yote ni maagano
Kuchepuka nje ya ndoa nako ni agano kamili ambalo itabidi lisafishwe kikamilifu na ujitoe katika hiyo kamba
Mara nyingi unasikia watu wanalalamika kuhusu tabia za watoto "huyu mtoto tabia kaichukua wapi, mbona baba na mama yake au ukoo wao hawako hivyo?". Chanzo cha tabia za ajabuajabu za watoto ni matokeo ya michepuko iliyofanya maagano na watu/koo zingine zenye laana. Laana na matatizo yanayoletwa na agano la damu katika familia havihitaji mtu kuchepuka na kuzaa nje ya ndoa, bali tu kuhusiana katika mapenzi!
Iko hivi kukutana kimwili na mtu mwenye maagano ya damu basi tambua na wewe ni sehemu ya maagano kwa maana ndigi ni kwamba mtu mchafu kiroho ukikutana naye na wewe ni sehemu ya huo uchafu
Maagano yanayofanywa na watu kwa njia ya kukutana kimwili na mtu mwenye maagano huenda vizazi hadi vizazi yaani kutoka kizazi hadi kizazi hubebwa na viashilia vilivyopo katika damu, mfano DNA hivyo hii ni hatari sana na inatisha na haya ndiyi huwasumbua watu wengi sana
Maagano ya kukutana kimwili na mtu mwenye maagano ya damu hii inawaathiri sana watoto na sio wahusika maana watoto ndo muunganiko wa damu mbili.
Ukifanya ngono na mtu mwenye mapepo huwa yanahamia pia kwako na kufanya agano nawe na kuathiri nyota yako.
Kumbuka kwamba nyota zina athari ya moja kwa moja katika maisha yetu na yeyote asiyefuata nyota yake hawezi kamwe kusonga mbele kwa maana anaishi nje ya asili yake