Kwenye hili nahitaji ‘Critical Thinking' tafadhali kama unajijua huna au hujabarikiwa nayo usipoteze muda wako

Je, Kujitokeza kwa mara ya Kwanza kwa Mwenyekiti Taifa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe na Chama chake hicho Kumruhusu Kuhudhuria Sherehe za Uhuru wa Nchi yetu tofauti na alivyokuwa akigoma na Chama chake pia Kutomtambua Rais Dkt. Magufuli Kunaashiria nini ndani ya CHADEMA, Demokrasia ya Tanzania, Ustawi wa Kisiasa nchini na Taswira nzima ya Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwakani 2020?

ANGALIZO

Kama unajijua huna ' Critical Thinking ' ya Kutukuka acha Kutupotezea muda na waachie Werevu wachangie bakia msomaji.
Nyuma ya pazia hali ya kisiasa ndani ya CHADEMA inashiria siyo "kubadili gia angani", kawaida yao, bali M/Kiti Mbowe anabadili "gia ardhini".

Kimsingi kubadilika huku huenda kukatokana na kutambua kuwa upepo wa kisiasa, kuelekea Uchaguzi Mkuu, 2020, baada ya kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (nguzo muhimu kupata ushindi katika Uchaguzi Mkuu), unaelekea kukitupa CHADEMA nje kabisa.

Isitoshe, wimbi la viongozi wake kukihama chama si dalili njema kabisa kwa afya ya kisiasa, nchini.

Pengine, utendaji wa Serikali ya CCM, chini ya uongozi wa M/kiti wake Rais Magufuli, unaviweka katika mtihani mgumu, vyama vya siasa jinsi ya kuwashawishi wapiga kura ifikapo 2020.

Mbali na hoja hizo, kitendo cha Rais Magufuli kuwapa fursa wao kuongea na WaTz leo kwenye sherehe za Uhuru, kilikuwa ni cha "kitendawili tega". Wahusika badala ya kuwasilisha hoja zenye kugusa WaTz walitumia fursa hiyo kutetea ubinafsi katika kivuli cha kudai "demokrasia" kana kwamba nchini hakuna demokrasia.

Yafuatayo ni maneno yao Mbowe na Lipumba waliyoyasema kwenye fursa hiyo, ambauo kimsingi hayawakilishi mahitaji ya muhimu ya wapiga kura:-

Ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango, tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu Demokrasia, tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano na Mh Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa, kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia, kaliweke Taifa katika nafasi ya utengamano, Mbowe.

Natoa pongezi kwa Watanzania wote, kwa kusherehekea miaka 58 ya Uhuru, mimi nilikua naingia darasa la nne, nampongeza Rais kwa kazi aliyoifanya, namuomba ajue anajukumu la kujenga demokrasia kwenye nchi yetu kuelekea Uchaguzi 2020, Profesa Lipumba.
 
1. Mbowe amegundua kwa muda wa miaka minne toka Magufuli aingie siasa za uanaharakati hazijawasaidia zaidi ya kuwadidimiza. Hili lowasa aliwaonya mapema na prof kitila mkumbo aliwahi kuonya mapema.
2. Amegundua Magufuli hana mpango na upinzani na kadiri wanavyosusa na kumpiga mawe ndio wanazidi kujiwekea mazingira magumu kisiasa. Hivyo kujisogeza ni kujaribu kumbadilisha mentality dhidi yao na pengine kujaribu fursa iliyobakia.
3. Amegundua uungwaji wa Magufuli unazidi kuongezeka. Hili utagundua zaidi anapokuwa ziarani. Na hii ni sababu ya jitihada zake za kumkomboa mtu wa chini. Umeme wa REA, maji, vivuko, vituo vya afya kila kona, kwa saaa ofisi za serikali zinaingilika na huduma unapata.
4. Wamegundua Magufuli sio mwanasiasa wa maneno, vijembe na michakato. Ni mtu wa matokeo sasa yaani big results now. Anasema kinatekelezwa. Yupo tayari kazi ifanywe hadi usiku eg. machinjio ya vingunguti ambayo haina hata miezi miwili imefikia 60% toka atoe tamko wakati ilikuwa ardhi tupu.
Ni mengi ika yatosha kusema hayo machache.
 
Siasa za tanzania ni hovyo sana binafsi kuanzia leo simwamini tena mbowe ni pandikizi la ccm linalotuchora wapinzani wa kweli
 
ANGALIZO langu la katika huu Uzi ulilisoma na Kuliewa vyema? Kuna Watu hapa Jamvini huwa mnanilazimisha niwajibu hovyo.
Usiwatishe watu kwamba utajibu ovyo mkuu hapa si gerezani hili ni jukwaa huru na kuna taratibu zake... ndio maana wanachangia watakavyo na si utakavyo. Ikiwa hupendi maoni tofauti kwanini uweke uzi hapa jukwaani?
Huu ni mfano mbaya ingelikuwa una madaraka nadhani ungefanya makubwa kuliko hiki kitisho!!! Ruksa kupovuka na kuonesha utovu wako wa adabu mkuu...
 
Mbowe, Lowassa, Sumaye, na kundi lao ni waumini wa dini zinazohubiri kusamehe wamekuwa wakihubiri kusamehe, ng'ambo ya pili naye Mfalme anahubiri kusamehe, hivyo basi imefika mahali wote wamejitambua kuwa wanachokuhubiri sicho wanachokitenda, yawezekana dhamira zimewasuta wakaamua kutazama maslahi ya nchi badala ya mizozo na kuumizana.
Kama wameona vema kufanya hivyo na wakatekeleza maridhiano basi watambue mitaani kuna vidonda vingi vya chuki na mdororo wa mahusiano baina ya mtu na mtu hata kuaminiana kumepungua na upendo wa watanzania tuliosifiwa nao ulikuwa shakani. Na tuombe yatimie...
 
Nimewatazama akina sugu, na Lema wakati mbowe anaenda jukwani. Nyuso zao japo ile kamera haikuwamulika sana, walionekana ni watu ambao wapo pale Kwa amri.

Mbowe kajitahidi kuficha hisia kaongea kiume fulani chenye uchungu moyoni, pale wameenda Kwa amri.

Angalia wakati mheshimiwa anatoka, nao wamejivuta Kwa shida kumpa mkono.

Kama siyo amri wameitikia mwaliko kwamba no way out, tumeshikwa, kesi kila kona.

But si Kwa mapenzi wameenda pale.
Rubbish.
 
Asante sana Genta, huu uzi ni mfano mzuri wa tabia za wapenda na wapigania demokrasia, haki, utu, kuheshimiana na usawa katika nchi yetu. Wanapambana kila siku kuikosoa serikali na taasisi nyingine kutotenda haki wakati wenyewe hawawezi kuishi demokrasia, haki na yote wayapiganiayo.

Tabia hiyo pia ndio inayomfanya Mbowe hii leo ashiriki sherehe za Uhuru na kuomba suluhu.

Hats kabla ya kuja Lowasa, tayari CDM kulikuwa na kilio cha ndani kuwa tufanye siasa, proper siasa badala ya uanaharakati. Arusha walikuwa na malalamiko juu ya siasa za uchonganishi, za vurugu na zenye kutia hasira za lema kuwa zinaua chama. CDM haikusikia,

Zitto alipozikataa siasa za jinsi hiyo na kina Mwigamba na kuja na kauli nchi kwanza chama baadae, wasimamizi wakuu wa siasa za harakati, zenye kutia hasira, siasa za kujenga mpasuko wakamshughulikia.

Lowasa, baada ya CDM kushindwa uchaguzi akaja na mawazo ya kukijenga chama imara. Wazo likiwa lile like, kufanya siasa proper na kuachana na siasa za kiharakati, siasa za kukosoa zaidi kuliko kujenga mipango mbadala na kuuza sera. Lowasa nae akaonekana ameishiwa na bado ni CCM.
Akiwa ndani ya CDM akakosewa heshima na vijana wenye damu ya kiharakati wenye kuweza kusema lolote iwe laivu au kwenye mitandao. CDM kikawa chama cha Kambale kama alivyojionea mzee wangu Juma Duni Haji. Kila mtu ana mamlaka, hakuna utaratibu, hakuna heshima ili mradi tu uwe mwanaharakati na uwe na hamu ya kukamatwa utiwe jela. Sifa kubwa ya CDM ikawa uwezo wa kumtemea mtu mbovu, kuwa tayari kwenda jela au kupigwa na polisi.

Hali ilivyozidi ikabidi mwenyekiti aseme, gharama ya mahakamani, kuwekeana dhamana na mambo kama hayo ikawa kubwa. Chama kinachopigania demokrasia kikawa tayari kutoheshimu haki za watu na utawala wa sheria. Chuki iliyopandwa miongoni mwao ikawa kali kiasi cha kuwa tayari kuiuza nchi kwa maadui wetu eti kisa tu CCM iko madarakani.

Tabia hiyo ya CDM ikalelewa na kuota mizizi. Bahati mbaya sana mazoea yalipojenga tabia, ikatokea nguvu ya kuwashikisha adabu na kuikomesha tabia hiyo. Tabia ilivyodhibitiwa vilivyo wale waliokuwa wanazikataa siasa za uanaharakati na kukuosoa tu wakaanza kuikacha CDM. Utekelezaji wa madai na urekebishaji wa makosa ukaiacha CDM haina hoja ya kisiasa. Watakosoa nini tena? CDM mara ikageuka, ikaanza kuwatetea iliyokuwa inawatuhumu, wananchi wakawashangaa, CDM ikazidi kupoteza muelekeo, dhamira yao haikueleweka miongoni mwa wananchi.

Madai ya CDM kuwa wasanii yakashika. Ikaonekana yale mamilioni aliyokuwa akipewa Mbowe na akina Kinana na Mkono yakapata uhalali, Majibu ya kuwa na uhusiano nje ya siasa na kufahamiana yakashindwa kujibu swali mipaka ya kufahamianà akina Mbowe na akina Kinana. Inawezekana ushamba was jamaa ndio ukazidisha chuki ya Mbowe kwa awamu iliyokataa kumdekeza na kumhonga ikazidi. Wabunge vijana wa Mbowe wakazidisha matusi kwa viongozi was kitaifa na nchi kiujumla.

Uchaguzi was ndani was CDM umekuwa dalili ya kuthibitisha ugonjwa was kuwepo makundi yanayosigana juu ya namna chama kinavyoendeshwa.

Kundi harakati na vurugu linaelekea kushinda kushika nafasi, lakini kundi siasa proper limeshinda kwa kuwaeleza na kuwaelekeza watanzania nini hasa kinaendelea ndani ya chadema.

Mbowe anafahamu madhara na nguvu ya kundi hili ndani ya chama chake. Anawafahamu wanaopinga siasa za namna hiyo waliokuwepo kabla ya mafuriko ambao bado wapo lakini hawaridhiki na anawafamu wana mafuriko ambao bado wapo lakini hawaridhiki.

Wale waliokuwepo kabla ya mafuriko ambao mioyo yao haipo kabisa CCM, kuna uwezekano mkubwa wakamfuata Zitto Zitto Act na wale wengine wakarudi nyumbani kwao.

Ajenda kwenye siasa za Tanzania kwa sasa ni sumu haijaribiwi kwa kuonjwa. Hizi ni tuhuma nzito kutolewa na mtu aliwahi kuwa mwenyekiti wa usalama wa Taifa.

Tuhuma za kumuua Chacha Wangwe, kujaribu kumdhuru Zitto, kumpa nafssi ya personal assistant Saanane kisha kumpoteza kutokana na misimamo take na mawasiliano take na Dr Slaa na hata wasiwasi wa kushiriki katika jaribio LA kutaka umuondoa Lissu sio tuhuma kubwa kama kumtia hofu aliyekuwa mwandamizi wa nchi anayelindwa na nchi.

Mbowe hapa anafanya mawili, kusahulisha tuhuma zake na pili kujaribu kunasua chama chake. Kujifanya kaachana na siasa za ulaghai na utapeli, siasa za harakati na vurugu, siasa za kudhuriana na kupotezana na kujifanya muungwana, siasa za Lazaro Nyalandu.

Lema, Jacob, Halima Mdee na viongozi wake, au genge lake kama alivyoliita Sumaye si wa siasa hizo, kamwe hawawezi kubadilika na hawataki kubadilika lakini wamelazimishwa kuigiza kubadilika na upepo wa kutoaminika na kutokukubalika tena, Mbowe anajaribu kubadili gia kuwatoa kwenye matope. So rahisi kufanikiwa katika siasa za Magufuli
Kweli umeandika gazeti, sasa ni ipi relation kati ya hiki ulichokiandika hapa kuhusu yanayotokea ndani ya CDM na kilichotokea leo?!

Halafu habari ya Zitto na wengineo sijui imekuja vipi hapa!, kama unamuona ana vision, vipi hiyo ACT yake inaendeleaje?!

Siasa zetu zinalazimisha uanaharakati, huwezi kulazimisha hoja kwenye mazingira ambayo polisi wanatumika kukibeba chama tawala. Utaenda vipi kulinda kura kwa hoja ulizoandika kwenye daftari? Hao wazee uliowataja Lowassa na Sumaye hawakujua ugumu wa kuwa mpinzani tz, mpk walivyoingia ndani ndio wakajionea, Tumemsikia Sumaye analalamika kanyan'ganywa mashamba, hayo ndio malipo ya kuwa mpinzani tz. Mbowe kaharibiwa mali zake zote, ndio malipo yakuwa mpinzani tz.

Hili suala la sumu haijaribiwi kwa kuionja linakuzwa na wajinga tu, hivi hufahamu kama huo ni msemo tu, ni sawa na angesema kina cha maji hakijaribiwi kwa kuingiza mguu, wacheni kupotosha watu, kamuua Chacha Wangwe kama una shahidi si upeleke polisi?, kupotea kwa Saanane kama unaushahidi peleka polisi, sio kuropoka tu.

Unazungumzia CDM kutaka kuiuza nchi, nchi gani hiyo?, na ninani waliotaka kuuziwa hebu wataje hapa tuwajue, sema na bei waliyokubaliana, kichwa chako kimejaa pumba nyingi sana!
 
1. Mbowe amegundua kwa muda wa miaka minne toka Magufuli aingie siasa za uanaharakati hazijawasaidia zaidi ya kuwadidimiza. Hili lowasa aliwaonya mapema na prof kitila mkumbo aliwahi kuonya mapema.
2. Amegundua Magufuli hana mpango na upinzani na kadiri wanavyosusa na kumpiga mawe ndio wanazidi kujiwekea mazingira magumu kisiasa. Hivyo kujisogeza ni kujaribu kumbadilisha mentality dhidi yao na pengine kujaribu fursa iliyobakia.
3. Amegundua uungwaji wa Magufuli unazidi kuongezeka. Hili utagundua zaidi anapokuwa ziarani. Na hii ni sababu ya jitihada zake za kumkomboa mtu wa chini. Umeme wa REA, maji, vivuko, vituo vya afya kila kona, kwa saaa ofisi za serikali zinaingilika na huduma unapata.
4. Wamegundua Magufuli sio mwanasiasa wa maneno, vijembe na michakato. Ni mtu wa matokeo sasa yaani big results now. Anasema kinatekelezwa. Yupo tayari kazi ifanywe hadi usiku eg. machinjio ya vingunguti ambayo haina hata miezi miwili imefikia 60% toka atoe tamko wakati ilikuwa ardhi tupu.
Ni mengi ika yatosha kusema hayo machache.
Mbona hamruhusu mikutano ya hadhara kama mnajiamini anakubalika, ccm wanazunguka nchi nzima kina Polepole na Bashiru kufanya shughuli za kisiasa, vipi kwa CDM na upinzani kwa ujumla, waruhusuni na wao muone kama kweli mnakubalika.
 
Je, Kujitokeza kwa mara ya Kwanza kwa Mwenyekiti Taifa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe na Chama chake hicho Kumruhusu Kuhudhuria Sherehe za Uhuru wa Nchi yetu tofauti na alivyokuwa akigoma na Chama chake pia Kutomtambua Rais Dkt. Magufuli Kunaashiria nini ndani ya CHADEMA, Demokrasia ya Tanzania, Ustawi wa Kisiasa nchini na Taswira nzima ya Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwakani 2020?

ANGALIZO

Kama unajijua huna ' Critical Thinking ' ya Kutukuka acha Kutupotezea muda na waachie Werevu wachangie bakia msomaji.
Wewe mwenyewe sio critical thinker....but anyway ngoja nitulie nitakupa nondo.
 
Tukio la leo lina maana nyingi, BINAFSI niainishe CHACHE.

1. Tukio hili linatokea wakati Mh. Lowassa na Mh. Sumaye tayari wamejiweka pembeni ndani ya CHADEMA.

✓ Sasa inawezekana CHADEMA wanajaribu kumuonyesha Mh Raisi kuwa watu hawa wawili walikuwa wakiwachonganisha CHADEMA, CCM na SERIKALI.

2. Tukio hili pia linatokea wakati CHADEMA wanakaribia kufanya Mkutano Mkuu kwa ajili ya kuchagua Viongozi wakuu wa Chama.

✓Implication yake inaweza kuwa, kwamba Mh. Mbowe na Kamati Kuu wameamua kushiriki SHEREHE HIZI ZA UHURU ili kumnyima CREDIT mpinzani wa Mh. Mbowe.

3. Msuguano wa kisiasa, wakati tukio hili linatokea kuna msuguano mkubwa wa Kisiasa.

✓ Inawezekana CHADEMA wameamua kushiriki ikiwa ni sehemu ya mbinu yao kujiimarisha kichama kwa WANANCHI.

4. Inawezekena pia CHADEMA wametumia siku ya leo kuwasilisha kilio Chao.

✓ Ukisikiliza vizuri hotuba ya Mh. Mbowe kuna ujumbe mzito sana ndani yake. Ujumbe huu umewasilishwa mbele ya Mabalozi wa Nchi mbalimbali pamoja na Viongozi mbalimbali wa Vyama na Serikali.


CHADEMA kuhudhuria Maadhimisho ya leo ni SPECIAL MISSION.
Hii ndio critical thinker sasa.
 
Sababu za Chadema kuazimia kuhudhuria kwa maoni yangu ni kama zifuatazo;

1. Hoja za Chadema kukosa nguvu.
Hii ni kutokana na Chadema wenyewe kuanza kukosa uhalali wa kuhoji suala zima la demokrasia.
Wengi walikuwa na hamu kuona jinsi Chadema kinavyokuwa mstari wa mbele kuonesha demokrasia ya kweli lakini umekuwa kinyume chake.Sababu zipo na mifano ipo wazi.
Hoja kama ya kupinga ufisadi imekufa na siyo agenda ya Chadema tena.CCM wameiteka na tunaona wanavyoifanyia kazi kwa spidi kama askari wa miavuli.

2. Kuonekana wazi kwa maendeleo ya miundo mbinu kama barabara,reli,nishati na kuimarika kwa usafiri wa anga na maji.Hii inafanya iwe vigumu sana kuwashawishi wananchi wasione na waanze kufikiri chama mbadala.Pamoja na kuwepo ugumu wa maisha lakini dalili zilizopo zinawapa matumaini wananchi wakiamini huenda huu ni mwanzo tu na hali itakaa sawa.

3. Kuimarika kwa nidhamu ya kazi serikalini ikiwa ni pamoja na kupungua sana kwa uonevu,kutotoa haki kwa waliopewa dhamana,na urasimu usiokuwa na sababu.Hata kama kuna sehemu bado hazijakaa sawa lakini ile hali ya mh.Magufuli kuchukua hatua za haraka kukemea na kuonya mara agunduapo 'madudu' ya jinsi hiyo yanafanywa,kunawafanya wananchi wawe na matumaini sana.Na zaidi pale wananchi wanapoona safu aliyonayo ikiongozwa na mh.Kassim Majaliwa jembe jingine hatari sana.

4. Faida za Chadema kuhudhuria ni nyingi na zinafanya wananchi waone kwamba kumbe ni wastaarabu licha ya kukutana na changamoto nyingi katika utendaji wao kisiasa.Hasara ya wao kutohudhuria ingekuwa kubwa zaidi kwani wananchi wengi hawaguswi sana na maumivu wanayoyapata wao Chadema na hivyo wangebaki wakiwashangaa tu kwa nini wanasusia ili hali Rais akitekeleza mambo mengi ya kimaendeleo na yanaonekana.

5. Mh.John Pombe Magufuli licha ya mambo ya maendeleo,ameonesha kuwa yeye ni binadamu mwenye huruma na mwenye msamaha.
Kuna mambo kama ya kusamehe wafungwa ambao walihukumiwa kunyongwa tangu enzi za Utawala wa awamu ya kwanza hadi leo yameleta hisia sana kwa wananchi na kumuona mtu huyu ni mwenye moyo wa pekee sana.
Kwa mambo kama hayo amejipatia wafuasi wengi sana na hivyo wanamchukulia kama mzazi hata kama atateleza katika kauli,watanzania wengi walishamsamehe pia
Pumba
 
Asante sana Genta, huu uzi ni mfano mzuri wa tabia za wapenda na wapigania demokrasia, haki, utu, kuheshimiana na usawa katika nchi yetu. Wanapambana kila siku kuikosoa serikali na taasisi nyingine kutotenda haki wakati wenyewe hawawezi kuishi demokrasia, haki na yote wayapiganiayo.

Tabia hiyo pia ndio inayomfanya Mbowe hii leo ashiriki sherehe za Uhuru na kuomba suluhu.

Hats kabla ya kuja Lowasa, tayari CDM kulikuwa na kilio cha ndani kuwa tufanye siasa, proper siasa badala ya uanaharakati. Arusha walikuwa na malalamiko juu ya siasa za uchonganishi, za vurugu na zenye kutia hasira za lema kuwa zinaua chama. CDM haikusikia,

Zitto alipozikataa siasa za jinsi hiyo na kina Mwigamba na kuja na kauli nchi kwanza chama baadae, wasimamizi wakuu wa siasa za harakati, zenye kutia hasira, siasa za kujenga mpasuko wakamshughulikia.

Lowasa, baada ya CDM kushindwa uchaguzi akaja na mawazo ya kukijenga chama imara. Wazo likiwa lile like, kufanya siasa proper na kuachana na siasa za kiharakati, siasa za kukosoa zaidi kuliko kujenga mipango mbadala na kuuza sera. Lowasa nae akaonekana ameishiwa na bado ni CCM.
Akiwa ndani ya CDM akakosewa heshima na vijana wenye damu ya kiharakati wenye kuweza kusema lolote iwe laivu au kwenye mitandao. CDM kikawa chama cha Kambale kama alivyojionea mzee wangu Juma Duni Haji. Kila mtu ana mamlaka, hakuna utaratibu, hakuna heshima ili mradi tu uwe mwanaharakati na uwe na hamu ya kukamatwa utiwe jela. Sifa kubwa ya CDM ikawa uwezo wa kumtemea mtu mbovu, kuwa tayari kwenda jela au kupigwa na polisi.

Hali ilivyozidi ikabidi mwenyekiti aseme, gharama ya mahakamani, kuwekeana dhamana na mambo kama hayo ikawa kubwa. Chama kinachopigania demokrasia kikawa tayari kutoheshimu haki za watu na utawala wa sheria. Chuki iliyopandwa miongoni mwao ikawa kali kiasi cha kuwa tayari kuiuza nchi kwa maadui wetu eti kisa tu CCM iko madarakani.

Tabia hiyo ya CDM ikalelewa na kuota mizizi. Bahati mbaya sana mazoea yalipojenga tabia, ikatokea nguvu ya kuwashikisha adabu na kuikomesha tabia hiyo. Tabia ilivyodhibitiwa vilivyo wale waliokuwa wanazikataa siasa za uanaharakati na kukuosoa tu wakaanza kuikacha CDM. Utekelezaji wa madai na urekebishaji wa makosa ukaiacha CDM haina hoja ya kisiasa. Watakosoa nini tena? CDM mara ikageuka, ikaanza kuwatetea iliyokuwa inawatuhumu, wananchi wakawashangaa, CDM ikazidi kupoteza muelekeo, dhamira yao haikueleweka miongoni mwa wananchi.

Madai ya CDM kuwa wasanii yakashika. Ikaonekana yale mamilioni aliyokuwa akipewa Mbowe na akina Kinana na Mkono yakapata uhalali, Majibu ya kuwa na uhusiano nje ya siasa na kufahamiana yakashindwa kujibu swali mipaka ya kufahamianà akina Mbowe na akina Kinana. Inawezekana ushamba was jamaa ndio ukazidisha chuki ya Mbowe kwa awamu iliyokataa kumdekeza na kumhonga ikazidi. Wabunge vijana wa Mbowe wakazidisha matusi kwa viongozi was kitaifa na nchi kiujumla.

Uchaguzi was ndani was CDM umekuwa dalili ya kuthibitisha ugonjwa was kuwepo makundi yanayosigana juu ya namna chama kinavyoendeshwa.

Kundi harakati na vurugu linaelekea kushinda kushika nafasi, lakini kundi siasa proper limeshinda kwa kuwaeleza na kuwaelekeza watanzania nini hasa kinaendelea ndani ya chadema.

Mbowe anafahamu madhara na nguvu ya kundi hili ndani ya chama chake. Anawafahamu wanaopinga siasa za namna hiyo waliokuwepo kabla ya mafuriko ambao bado wapo lakini hawaridhiki na anawafamu wana mafuriko ambao bado wapo lakini hawaridhiki.

Wale waliokuwepo kabla ya mafuriko ambao mioyo yao haipo kabisa CCM, kuna uwezekano mkubwa wakamfuata Zitto Zitto Act na wale wengine wakarudi nyumbani kwao.

Ajenda kwenye siasa za Tanzania kwa sasa ni sumu haijaribiwi kwa kuonjwa. Hizi ni tuhuma nzito kutolewa na mtu aliwahi kuwa mwenyekiti wa usalama wa Taifa.

Tuhuma za kumuua Chacha Wangwe, kujaribu kumdhuru Zitto, kumpa nafssi ya personal assistant Saanane kisha kumpoteza kutokana na misimamo take na mawasiliano take na Dr Slaa na hata wasiwasi wa kushiriki katika jaribio LA kutaka umuondoa Lissu sio tuhuma kubwa kama kumtia hofu aliyekuwa mwandamizi wa nchi anayelindwa na nchi.

Mbowe hapa anafanya mawili, kusahulisha tuhuma zake na pili kujaribu kunasua chama chake. Kujifanya kaachana na siasa za ulaghai na utapeli, siasa za harakati na vurugu, siasa za kudhuriana na kupotezana na kujifanya muungwana, siasa za Lazaro Nyalandu.

Lema, Jacob, Halima Mdee na viongozi wake, au genge lake kama alivyoliita Sumaye si wa siasa hizo, kamwe hawawezi kubadilika na hawataki kubadilika lakini wamelazimishwa kuigiza kubadilika na upepo wa kutoaminika na kutokukubalika tena, Mbowe anajaribu kubadili gia kuwatoa kwenye matope. So rahisi kufanikiwa katika siasa za Magufuli
Pumba.
 
1. Mbowe amegundua kwa muda wa miaka minne toka Magufuli aingie siasa za uanaharakati hazijawasaidia zaidi ya kuwadidimiza. Hili lowasa aliwaonya mapema na prof kitila mkumbo aliwahi kuonya mapema.
2. Amegundua Magufuli hana mpango na upinzani na kadiri wanavyosusa na kumpiga mawe ndio wanazidi kujiwekea mazingira magumu kisiasa. Hivyo kujisogeza ni kujaribu kumbadilisha mentality dhidi yao na pengine kujaribu fursa iliyobakia.
3. Amegundua uungwaji wa Magufuli unazidi kuongezeka. Hili utagundua zaidi anapokuwa ziarani. Na hii ni sababu ya jitihada zake za kumkomboa mtu wa chini. Umeme wa REA, maji, vivuko, vituo vya afya kila kona, kwa saaa ofisi za serikali zinaingilika na huduma unapata.
4. Wamegundua Magufuli sio mwanasiasa wa maneno, vijembe na michakato. Ni mtu wa matokeo sasa yaani big results now. Anasema kinatekelezwa. Yupo tayari kazi ifanywe hadi usiku eg. machinjio ya vingunguti ambayo haina hata miezi miwili imefikia 60% toka atoe tamko wakati ilikuwa ardhi tupu.
Ni mengi ika yatosha kusema hayo machache.
Pumba
 
1. Tindu lissu risasi 38
2. Viongozi wa chadema wanasota mahakamani kila siku
3. Wanaharakati wa chadema wanatekwa/kuuwawa
4. Marufuku mikutanao ya hadhara
5. Sheria mpya ya vyama vya siasa lengo kukandamiza upinzani
7. Viongozi wa upinzani kufilisiwa
8. Rafu chaguzi za mtaa
9. Madiwani wa upinzani kuhamia CCM

Uchaguzi mkuu unakuja.......

1. Vyombo vya ulinzi na usalama vipo chini ya makada wa ccm (wakuu wilaya na mkoa)
2. Tume ya Uchaguzi NEC ipo chini ya Rais

Hapo unatokaje kwa mfano MARIDHIANO NI LAZIMA KWA USTAWI WA UPINZANI.
Point
 
Nyuma ya pazia hali ya kisiasa ndani ya CHADEMA inashiria siyo "kubadili gia angani", kawaida yao, bali M/Kiti Mbowe anabadili "gia ardhini".

Kimsingi kubadilika huku huenda kukatokana na kutambua kuwa upepo wa kisiasa, kuelekea Uchaguzi Mkuu, 2020, baada ya kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (nguzo muhimu kupata ushindi katika Uchaguzi Mkuu), unaelekea kukitupa CHADEMA nje kabisa.

Isitoshe, wimbi la viongozi wake kukihama chama si dalili njema kabisa kwa afya ya kisiasa, nchini.

Pengine, utendaji wa Serikali ya CCM, chini ya uongozi wa M/kiti wake Rais Magufuli, unaviweka katika mtihani mgumu, vyama vya siasa jinsi ya kuwashawishi wapiga kura ifikapo 2020.

Mbali na hoja hizo, kitendo cha Rais Magufuli kuwapa fursa wao kuongea na WaTz leo kwenye sherehe za Uhuru, kilikuwa ni cha "kitendawili tega". Wahusika badala ya kuwasilisha hoja zenye kugusa WaTz walitumia fursa hiyo kutetea ubinafsi katika kivuli cha kudai "demokrasia" kana kwamba nchini hakuna demokrasia.

Yafuatayo ni maneno yao Mbowe na Lipumba waliyoyasema kwenye fursa hiyo, ambauo kimsingi hayawakilishi mahitaji ya muhimu ya wapiga kura:-

Ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango, tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu Demokrasia, tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano na Mh Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa, kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia, kaliweke Taifa katika nafasi ya utengamano, Mbowe.

Natoa pongezi kwa Watanzania wote, kwa kusherehekea miaka 58 ya Uhuru, mimi nilikua naingia darasa la nne, nampongeza Rais kwa kazi aliyoifanya, namuomba ajue anajukumu la kujenga demokrasia kwenye nchi yetu kuelekea Uchaguzi 2020, Profesa Lipumba.
Pumba
 
Back
Top Bottom