mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,219
- 6,650
Nyuma ya pazia hali ya kisiasa ndani ya CHADEMA inashiria siyo "kubadili gia angani", kawaida yao, bali M/Kiti Mbowe anabadili "gia ardhini".Je, Kujitokeza kwa mara ya Kwanza kwa Mwenyekiti Taifa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe na Chama chake hicho Kumruhusu Kuhudhuria Sherehe za Uhuru wa Nchi yetu tofauti na alivyokuwa akigoma na Chama chake pia Kutomtambua Rais Dkt. Magufuli Kunaashiria nini ndani ya CHADEMA, Demokrasia ya Tanzania, Ustawi wa Kisiasa nchini na Taswira nzima ya Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwakani 2020?
ANGALIZO
Kama unajijua huna ' Critical Thinking ' ya Kutukuka acha Kutupotezea muda na waachie Werevu wachangie bakia msomaji.
Kimsingi kubadilika huku huenda kukatokana na kutambua kuwa upepo wa kisiasa, kuelekea Uchaguzi Mkuu, 2020, baada ya kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (nguzo muhimu kupata ushindi katika Uchaguzi Mkuu), unaelekea kukitupa CHADEMA nje kabisa.
Isitoshe, wimbi la viongozi wake kukihama chama si dalili njema kabisa kwa afya ya kisiasa, nchini.
Pengine, utendaji wa Serikali ya CCM, chini ya uongozi wa M/kiti wake Rais Magufuli, unaviweka katika mtihani mgumu, vyama vya siasa jinsi ya kuwashawishi wapiga kura ifikapo 2020.
Mbali na hoja hizo, kitendo cha Rais Magufuli kuwapa fursa wao kuongea na WaTz leo kwenye sherehe za Uhuru, kilikuwa ni cha "kitendawili tega". Wahusika badala ya kuwasilisha hoja zenye kugusa WaTz walitumia fursa hiyo kutetea ubinafsi katika kivuli cha kudai "demokrasia" kana kwamba nchini hakuna demokrasia.
Yafuatayo ni maneno yao Mbowe na Lipumba waliyoyasema kwenye fursa hiyo, ambauo kimsingi hayawakilishi mahitaji ya muhimu ya wapiga kura:-
Ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango, tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu Demokrasia, tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano na Mh Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa, kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia, kaliweke Taifa katika nafasi ya utengamano, Mbowe.
Natoa pongezi kwa Watanzania wote, kwa kusherehekea miaka 58 ya Uhuru, mimi nilikua naingia darasa la nne, nampongeza Rais kwa kazi aliyoifanya, namuomba ajue anajukumu la kujenga demokrasia kwenye nchi yetu kuelekea Uchaguzi 2020, Profesa Lipumba.