MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,563
Wapendwa
Ni matumaini yangu mlikuwa na weekend yenye Baraka.
Mimi wiki hii MwanajamiiOne nimeianza kwa uchungu huku machozi yakinitiririka barabarani asubuhi wakati nakuja kibaruani. Kwenye taarifa ya habari iliyotangazwa kupitia Radio One. Mama mmoja huko Morogoro aliyekamatwa kwa kosa la kumpiga vibaya Mtoto wa Mume wake (Mtoto wa kambo). Taarifa hiyo ambayo ilisema mtoto huyo mwenye umri wa miaka 3 inasemekana amepigwa hadi kuvunjwa mkono na mguu huku akiachiwa majeraha sehemu za kichwa baada ya kupigwa mateke, kuangushwa chini huku akijipigiza sakafuni na kung'atwa kwa meno mwilini.
Taarifa ilisema mtoto huyo (kwa mujibu wa majirani) amekuwa akichezea matezo hayo karibia kila siku pamoja na kufanyishwa kazi ngumu (Mtoto wa miaka 3??!!). Aliambulia kupigwa (tena kwa kuchangiwa na mama huyo na mwanae) pale anapotumwa kitu mfano mwiko akakosea (Mtoto wa Miaka 3!!).
Sitaki kusema mengi lakini kwa kifupi, kina Baba ambao mna watoto wenu ambao hamuishi na mama zao, NINAWAOMBA muwe japo na kajitabia ka kusoma alama za nyakati. Ni kweli kuwa si mama wote wa kambo ni wabaya lakini you never know just take time kuchungua mazingira.
Ningetamani kweli kujua namna ya kufanya hili liwe kweli lakini sijui, yaani nashuindwa kuwaza kabisa.
KUWENI tu MAKINI.
MBARIKIWE SANA KINA BABA NA MAMA WAZAZI/WALEZI WENYE MIOYO YA UPENDO KWA WATOTO WAO HATA KAMA HAWAJAWAZAA WAO.
Pole sana kwa uchungu Mj1,na sisi wababa tumeuchukua ushauri wako kwa uzito mkubwa_lakn ni bora zaidi pia unge wa adress wamama kwani wao ndio wafanyaji wakubwa wa vitendo hivi vya kinyama,...wewe kama mama mwenzao ungechukua nafasi hii kuwaomba waache kuwatesa watoto ambao hawaja wazaa,....ila inasikitisha na kuuma sana
Igwe ni kweli kabisa,
kwanza nakushukuru kwa kuacknowledge kuwa you have a part to play, zaidi sana akina mama wa jinsi hii sidhani hata kama hapa JF wanapitapita, lakini nina uhakika wanaume wengi walio hapa ( baadhi ) wana watoto 'wa ujanani' etc kama wewe ni mwanaume unasoma hapa, na unakaa na mwanao, naomba umwangalie vizuri ama kama sote tunajua ukatili unapofanyika tujitahidi kuripoti na kuminimize situation
juzi wakati nakuja kazini asubuhi nimepita njia panya za mwananyamala huko katikati, kukwepa foleni, njiani nikakuta mwanamke amefunga kanga moja anamtandika mtoto mdogo sana kwa kosa la kupoteza shs 200, kwavile tulikuwa tumesimama muda mrefu nikawa naangalia tu kama wengine, lakini akina mama wanaochoma mihogo hapo pembeni wakawa wanasema, 'ndio hivyo tena mtoto anapewa kipigo kwa vile si wake wakati wezi ni wanae' kwakweli sikuvumilia zaidi nilimpatia huyo mama shs 1,000 nikamwambia mwache mtoto aende shule jamani ni asubuhi unamchapa sasa hivi atachapwa tena kuchelewa, ok huyo mama aliichukua kwa kubetua midomo akaingia ndani akamwambia na uende shule mwana laana we!! kinanisikitisha kuwa majirani wanaona na watu hatuchukui hatua najua akirudi shule pengine atachapwa zaidi kwa kumdhalilisha mama mbele za watu hata sijui ?
oh my oh my !!
huu ukatili sijui utaisha lini, na sijui kwanini majirani ambao wako karibu hawaripoti vitendo hivyo, mtoto wa miaka 3 tena si wako unampigia nini jamani ? kwanini usimshawishi mumeo amrudishe kwa mama yake ?
yaani kila kukicha namshukuru Mungu kunipa uhai ili niendelee kuwaangalia wanangu, napata shida nikiwaza kuna mwanamke mwingine atawaangalia kama mimi ( yaani sio wanawake wote wabaya lakini haya mambo ya udhalilishaji yanavyoongezeka inatisha )
mwanajamii one, it has always been my intention to fund causes for abused children and housegirls, when we have time out of our busy schedule we can contribute back to the society, niPM au any interested party can PM me...tuangalie tu hata tukisaidia mmoja si haba[/QUOTE]
Nakuunga mkono mama,count me in.
Mara nyingi familia km hiyo baba huwa amekaliwa na mama (mama ndo kila kitu ndani ya nyumba na wamama hao huwa ni jst house wives.......... Thats my experience and point of view though......... Mtoto anaweza pigwa hata mbele ya baba na kunyimwa hata chakula.....
Nimejikuta nimemkumbuka Chetuntu ghafla......... sijui kale ka handsome kake katalelewa na mama wa kambo?Babu na Mjomba IGWE nimewaelewa lakini lengo na madhumuni yangu kuwalenga nyie nina maana kuwa mwanamke mwenye roho ya kishetwani kama huyu hata nikimwambia nitakuwa ninampigia mbuzi gitaa na isitoshe threads nyingi za jambo hili zilikuwa zinawalenga wao so nimejiona kama vile sina jipya la kuwaeleza wanawake wenzangu niwageukie kina Baba.
Imagine huyu alikuwa anakanywa na majirani na mashosti zake kuwa utamwuua mtoto wa watu anawajibu kama mna uchungu naye mchukueni mkamlee ninyi!! (Mtoto wa miaka 3?!!) jamani. Kitendo hiki kusema ukweli kimenifanya kwa mara ya kwanza maishani mwangu nione aibu kuzaliwa mwanamke (Sijuti). ............ Hivi kweli nawezapita kifua mbele kuwa mie ni mwanamke ilihali kuna wanawake wenye roho za kikatili kuliko wanyama?
Wewe baba mwenye mtoto wako anayeishi na mama mwingine, huwa unachukua jukumu gani kuhakikisha kuwa anapata huduma, malezi na upendo kutoka kwa mama yake wa kambo? au unaamini tu kuwa analelewa vizuri kwa kuwa tu ukirudi unamkuta/ona mama huyo anamchekea au kujifanya anamkumbatia? ni mbinu gani mtu anawezatumia ili kulijua hili??
Wapendwa
Ni matumaini yangu mlikuwa na weekend yenye Baraka.
Mimi wiki hii MwanajamiiOne nimeianza kwa uchungu huku machozi yakinitiririka barabarani asubuhi wakati nakuja kibaruani. Kwenye taarifa ya habari iliyotangazwa kupitia Radio One. Mama mmoja huko Morogoro aliyekamatwa kwa kosa la kumpiga vibaya Mtoto wa Mume wake (Mtoto wa kambo). Taarifa hiyo ambayo ilisema mtoto huyo mwenye umri wa miaka 3 inasemekana amepigwa hadi kuvunjwa mkono na mguu huku akiachiwa majeraha sehemu za kichwa baada ya kupigwa mateke, kuangushwa chini huku akijipigiza sakafuni na kung'atwa kwa meno mwilini.
Taarifa ilisema mtoto huyo (kwa mujibu wa majirani) amekuwa akichezea matezo hayo karibia kila siku pamoja na kufanyishwa kazi ngumu (Mtoto wa miaka 3??!!). Aliambulia kupigwa (tena kwa kuchangiwa na mama huyo na mwanae) pale anapotumwa kitu mfano mwiko akakosea (Mtoto wa Miaka 3!!).
Sitaki kusema mengi lakini kwa kifupi, kina Baba ambao mna watoto wenu ambao hamuishi na mama zao, NINAWAOMBA muwe japo na kajitabia ka kusoma alama za nyakati. Ni kweli kuwa si mama wote wa kambo ni wabaya lakini you never know just take time kuchungua mazingira.
Ningetamani kweli kujua namna ya kufanya hili liwe kweli lakini sijui, yaani nashuindwa kuwaza kabisa.
KUWENI tu MAKINI.
MBARIKIWE SANA KINA BABA NA MAMA WAZAZI/WALEZI WENYE MIOYO YA UPENDO KWA WATOTO WAO HATA KAMA HAWAJAWAZAA WAO.