Kweli Ya kale ni dhahabu

Kweli Ya kale ni dhahabu

Kama kuna demu unampenda unamvizia akienda kukojoa akitoka tu na wewe unaenda kukojolea kale kashimo kalikochimbwa na mkojo wake, haipiti hata siku lazima utamtafuna, binafsi nilisubiri sana kutafuna mademu kiulaini lakini ikawa bila bila.

Binafc niliamini kabisa kwamba ni hatari kuwa karibu na kondoo wakati mvua inanyesha, maana radi huwa inashuka kumtafuta ili ipigane nae.

Niliamini kwamba ili vita ya nchi na nchi ipiganwe basi unachorwa mstari mreeefu sana, halafu upande huu wanasimama wanajeshi wa nchi A na upande wa pili wanasimama wanajeshi wa nchi B halafu mashine zinaanza kuunguruma pale.
Hahaa hii naikumbuka ilikuwaga ni ujinga sana aise
 
Binafsi nina kigugumizi. Siku moja utotoni mwangu, jamaa mmoja aliniudhi sana kwa kunitukania Mama yangu, basi tukapanga kupigana baada ya shule kwisha kwa ile siku. Tukaenda uchochoroni huku mie nikiwa na hasira ile mbaya, wapambe kibao walijaa kwani walikuwa wanajuwa mimi nikipigana lazima nimtoe ngebe mwenzangu, yaani sina msamaha hata kidogo na nilikuwa najulikana mpaka kuitwa 'Bud Spencer' enzi hizo. Wapambe wakachota mchanga na kutuambia tupute, nikaanza mimi kuputa...mwenzangu akawa anaogopa kwani alikuwa anajuwa muziki wangu au ni uwoga wake tu ulimzuia. Kwa kuwa nilikuwa na hasira sana, kigugumizi kikanishika na kuongea kumwambia jamaa apute mchanga siwezi. Kuangalia kando nikaona mpambe mmoja kashika kifuu anakifukia nikajuwa ni yeye ndiye kanifanya nishindwe kuongea. Ee bwana, nilimwacha yule jamaa niliyetaka kupigana naye na kumvamia mpambe, nilimtandika ile mbaya, nilimtwanga vichwa mpaka akapasuka midomo na kuvunja pua yake. Usiku nashangaa wanakuja yeye na Mama yake na polisi kuja kunikamata kunipeleka polisi. Nikaruka ukuta na kukimbilia Tandale kwa wahuni. Sikuonekana nyumbani wiki nzima kwani nilijuwa nakwenda kufungwa jela ya watoto.
Mkuu kwahy unasibitisha kifuu ukikifuka mweny kigugumiz awez kuongea
 
Mkuu kwahy unasibitisha kifuu ukikifuka mweny kigugumiz awez kuongea


Nimeshasema zamani nilipokuwa mtoto nilikuwa naamini hivyo. Imani ni sawa na dini tu, ukishaweka kitu akilini mwako basi unahisi ni ukweli kumbe ni hulka tu. Ila hata hivi sasa kama unataka kuniudhi na kunipa hasira....we jaribu kutembea na kifuu mbele yangu huku ukinionyesha kwa tambo, hapo ndipo utajuwa kwanini utotoni watu walikuwa wananiita Bud Spencer kwa ubabe wangu. Sipendi vifuu ila nazi nakula.
 
Du mvua ikinyesha tulikuwa tunaomba kufika mchana ikatike na jua liwake. Bila jua kutoka tuliambiwa hakuna chakula cha jioni. Ila ninapotoka mvua zikifika saa nane lazima zikatike na jua litoke. Hapo ndo wakati wa kuokota kumbikumbi. Tulikuwa nunaambiwa na walimu tupileke kila mmoja kumbikumbi tano.
 
Iyo namba 11 mother kanidanganya sana, nakumbuk ilivyo karibia kujifungua mdogo wangu aliniaga kuwa anaenda kununua mtoto hospital.
Nikaamin ivo, baada siku kadhaa akaja na kadogo kangu ka kike nikamwambia Mama umechagua katoto kazuri alicheka sanaa


Kasomali
 
Binafsi nina kigugumizi. Siku moja utotoni mwangu, jamaa mmoja aliniudhi sana kwa kunitukania Mama yangu, basi tukapanga kupigana baada ya shule kwisha kwa ile siku. Tukaenda uchochoroni huku mie nikiwa na hasira ile mbaya, wapambe kibao walijaa kwani walikuwa wanajuwa mimi nikipigana lazima nimtoe ngebe mwenzangu, yaani sina msamaha hata kidogo na nilikuwa najulikana mpaka kuitwa 'Bud Spencer' enzi hizo. Wapambe wakachota mchanga na kutuambia tupute, nikaanza mimi kuputa...mwenzangu akawa anaogopa kwani alikuwa anajuwa muziki wangu au ni uwoga wake tu ulimzuia. Kwa kuwa nilikuwa na hasira sana, kigugumizi kikanishika na kuongea kumwambia jamaa apute mchanga siwezi. Kuangalia kando nikaona mpambe mmoja kashika kifuu anakifukia nikajuwa ni yeye ndiye kanifanya nishindwe kuongea. Ee bwana, nilimwacha yule jamaa niliyetaka kupigana naye na kumvamia mpambe, nilimtandika ile mbaya, nilimtwanga vichwa mpaka akapasuka midomo na kuvunja pua yake. Usiku nashangaa wanakuja yeye na Mama yake na polisi kuja kunikamata kunipeleka polisi. Nikaruka ukuta na kukimbilia Tandale kwa wahuni. Sikuonekana nyumbani wiki nzima kwani nilijuwa nakwenda kufungwa jela ya watoto.
bilashaka leo wewe ndiye Scorpion!
 
*sisi vitindamimba tulikuwa tunapewa chumvi na kuinama kuirusha nyuma kupitia katikati ya miguu kwamba unazuia mvua ya mawe.

*tuliaminishwa ukimtukana mzee utaota sehemu za siri kwenye paji

*ili kuepushwa kuchelewa mtoni, mzazi alikuwa akitema mate kwenye jani na kusema mkirudi mate yamekauka mnakufa

*ukisimulia hadithi mchana, hukui au usiku hutosinzia

*....... wengine waendelee maana karibu elimu hii ilikuwa universal.
 
mtoo wa mwisho kuzaliwa aliambiwa agonoke juu ili kama kuna wingu mvua isinyeshe watu waendelee na mishe zao.
 
Back
Top Bottom