Kweli Ya kale ni dhahabu

Kweli Ya kale ni dhahabu

ARGAN MARA

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2016
Posts
1,135
Reaction score
2,940
ENZI ZA UTOTO TULIAMINI KWAMBA...
Kwa Wahenga tu si Kwa KIzazi cha Video Game

1. Ukiweka SINDANO kwenye RELI (aidha ya kirungu au ya kushonea) Basi TRENI ikipita itapinduka...

2. Ukila TUNDA lenye mbegu mfano chungwa, Bungo au Ubuyu, tulijitahidi tusimeze MBEGU, maana tukiamini kuwa ukimeza mbegu Mti wa ilo tunda utaota kichwani.

3. Tukiamni kuwa ukinyooshea kidole KABURI, basi kidole chako KITAOZA.

4. Ukiona Kuku wakipigana UKICHOMEKA KISU chini ardhini watapigana mpaka mmoja afe.

5. Mtu mwenye KIGUGUMIZI akiongea UKAFUNIKA KIFUU basi hataweza kuongea na atabakia anagugumia mpaka ukifunue.

6. Ukikutana na ALBINO temea mate KIFUANI/KITOVUNI kwako usipofanya hivyo nawe utakuja KUZAA kama huyo.

7. Tuliamini pia Albino HAWAFI, bali wanapotea tu Kimiujiza.

8. Ukihadithia HADITHI MCHANA basi utaota MKIA

9. Siku JUA likiwaka na MVUA kunyeesha basi sikuo hiyo SIMBA jike porini anazaa!
Na kama kuna mpira siku hiyo na Yanga anacheza basi matokeo yatakuwa sare.

10. Siku UKING'OA JINO tupa juu ya PAA la nyumba KUNGURU akilichukua jino lako ndio litaota jingine.

11. Watoto wote WANANUNULIWA hospitali au Wanaokotwa BAHARINI.

12. KONDOO ukimfunga kitambaa chekundu anapigana na radio iliyokua karibu yake.

13. Tuliamini kuwa wagonjwa wote wa akili (Vichaa na wendawazimu) kabla ya kuugua walikuwa ni WASOMI WAKUBWA SANA.

14. Ukiwa unanyonyoa KUKU/BATA usizungumze, ukizungumza tu MANYOYA yanarudi upya.

15. Tukiamini kuwa MAJAMBAZI ni Watu wenye sura ZINAZOTISHA, kama sura haitishi, basi sio Jambazi.

16. Ukitaka KUPIGANA na mwenzio ili kupata uhakika, unachora MSTARI na kumwambia ...KAMA WEWE MWAMBA VUKA HUO MSTARI, kitendo cha yeye kuvuka tu, ni ndundi tu, hakuna kuuliza mara ya pili.

Kama pembeni kuna mashabiki wapambe, watachota mchanga mkononi na kukwambia kama kweli unataka kupigana puta mchanga huu, kisha aliyekupa mchanga atakunja ngumi na kukwambia tia kidole hapa (Katikati ya kiganja chake), kitendo hicho tulikichukulia kama tusi kubwa sana na mtu kama kama kafanya hivyo basi kweli kadhamiria ugomvi na mtazipiga tu.

17. Kama unaangalia mpira na ukaona timu yako inataka kufungwa au ni pira wa penati, basi tuliamini UKIZIBANA SEHEMU ZAKO BINAFSI yule mpigaji penati atakosa na kupiga nje au juu au kipa atadaka.

18. Kama umekaa na UMENYOOSHA MIGUU, ikatokea mtu AMEKURUKA, basi atatakiwa arudi na kukuruka tena, hasipo fanya hivyo atasababisha yule aliyerukwa kutokukua yaani hato ongezeka kimo atabakia kuwa andunje.

19. kama mmekaa na mmoja wenu KASIMAMA, tuliokaa wote tuliamini yule aliyekaa atakuwa ANATUNYONYA DAMU.
Utasikia tu mtu analalamika, ebu kaa chini usitunyonye damu.

20. Watoto wa Kike walikuwa wanaweka mdudu (Fukufuku) kwenye manyonyo yao, wakiamini kuwa yatakuwa makubwa... Yule mdudu ilikuwa ukimuimbia, sikumbuki vizuri ule wimbo, ila ulikuwa kama hivi... Fukufuku toka nitakupa maji ya sukari... au Fukufuku toka baba yako kaja... (Na ajabu wale wadudu ukiwaimbia walikuwa wanatoka).

21. Kuna ndege wa Pwani, tukiwajua kwa jina la Yangeyange (Bata Maji) walikuwa weupe, wakiruka tukiwaimbia... Yangeyange tupe kucha nyeupe... Tukiamini kuwa kwa kuimba uko tutakuwa na kucha Nyeupe.

Ongeza Mengine Unayo Yakumbuka...
FB_IMG_1557191453603.jpeg
 
ENZI ZA UTOTO TULIAMINI KWAMBA...
Kwa Wahenga tu si Kwa KIzazi cha Video Game

1. Ukiweka SINDANO kwenye RELI (aidha ya kirungu au ya kushonea) Basi TRENI ikipita itapinduka...

2. Ukila TUNDA lenye mbegu mfano chungwa, Bungo au Ubuyu, tulijitahidi tusimeze MBEGU, maana tukiamini kuwa ukimeza mbegu Mti wa ilo tunda utaota kichwani.

3. Tukiamni kuwa ukinyooshea kidole KABURI, basi kidole chako KITAOZA.

4. Ukiona Kuku wakipigana UKICHOMEKA KISU chini ardhini watapigana mpaka mmoja afe.

5. Mtu mwenye KIGUGUMIZI akiongea UKAFUNIKA KIFUU basi hataweza kuongea na atabakia anagugumia mpaka ukifunue.

6. Ukikutana na ALBINO temea mate KIFUANI/KITOVUNI kwako usipofanya hivyo nawe utakuja KUZAA kama huyo.

7. Tuliamini pia Albino HAWAFI, bali wanapotea tu Kimiujiza.

8. Ukihadithia HADITHI MCHANA basi utaota MKIA

9. Siku JUA likiwaka na MVUA kunyeesha basi sikuo hiyo SIMBA jike porini anazaa!
Na kama kuna mpira siku hiyo na Yanga anacheza basi matokeo yatakuwa sare.

10. Siku UKING'OA JINO tupa juu ya PAA la nyumba KUNGURU akilichukua jino lako ndio litaota jingine.

11. Watoto wote WANANUNULIWA hospitali au Wanaokotwa BAHARINI.

12. KONDOO ukimfunga kitambaa chekundu anapigana na radio iliyokua karibu yake.

13. Tuliamini kuwa wagonjwa wote wa akili (Vichaa na wendawazimu) kabla ya kuugua walikuwa ni WASOMI WAKUBWA SANA.

14. Ukiwa unanyonyoa KUKU/BATA usizungumze, ukizungumza tu MANYOYA yanarudi upya.

15. Tukiamini kuwa MAJAMBAZI ni Watu wenye sura ZINAZOTISHA, kama sura haitishi, basi sio Jambazi.

16. Ukitaka KUPIGANA na mwenzio ili kupata uhakika, unachora MSTARI na kumwambia ...KAMA WEWE MWAMBA VUKA HUO MSTARI, kitendo cha yeye kuvuka tu, ni ndundi tu, hakuna kuuliza mara ya pili.

Kama pembeni kuna mashabiki wapambe, watachota mchanga mkononi na kukwambia kama kweli unataka kupigana puta mchanga huu, kisha aliyekupa mchanga atakunja ngumi na kukwambia tia kidole hapa (Katikati ya kiganja chake), kitendo hicho tulikichukulia kama tusi kubwa sana na mtu kama kama kafanya hivyo basi kweli kadhamiria ugomvi na mtazipiga tu.

17. Kama unaangalia mpira na ukaona timu yako inataka kufungwa au ni pira wa penati, basi tuliamini UKIZIBANA SEHEMU ZAKO BINAFSI yule mpigaji penati atakosa na kupiga nje au juu au kipa atadaka.

18. Kama umekaa na UMENYOOSHA MIGUU, ikatokea mtu AMEKURUKA, basi atatakiwa arudi na kukuruka tena, hasipo fanya hivyo atasababisha yule aliyerukwa kutokukua yaani hato ongezeka kimo atabakia kuwa andunje.

19. kama mmekaa na mmoja wenu KASIMAMA, tuliokaa wote tuliamini yule aliyekaa atakuwa ANATUNYONYA DAMU.
Utasikia tu mtu analalamika, ebu kaa chini usitunyonye damu.

20. Watoto wa Kike walikuwa wanaweka mdudu (Fukufuku) kwenye manyonyo yao, wakiamini kuwa yatakuwa makubwa... Yule mdudu ilikuwa ukimuimbia, sikumbuki vizuri ule wimbo, ila ulikuwa kama hivi... Fukufuku toka nitakupa maji ya sukari... au Fukufuku toka baba yako kaja... (Na ajabu wale wadudu ukiwaimbia walikuwa wanatoka).

21. Kuna ndege wa Pwani, tukiwajua kwa jina la Yangeyange (Bata Maji) walikuwa weupe, wakiruka tukiwaimbia... Yangeyange tupe kucha nyeupe... Tukiamini kuwa kwa kuimba uko tutakuwa na kucha Nyeupe.

Ongeza Mengine Unayo Yakumbuka...View attachment 1090095
daaa leo mkuu umenikumbusha habari njema kabisa,,sisi watoto wa udongo tumekuelewa sana mkuu
 
Binafsi nina kigugumizi. Siku moja utotoni mwangu, jamaa mmoja aliniudhi sana kwa kunitukania Mama yangu, basi tukapanga kupigana baada ya shule kwisha kwa ile siku. Tukaenda uchochoroni huku mie nikiwa na hasira ile mbaya, wapambe kibao walijaa kwani walikuwa wanajuwa mimi nikipigana lazima nimtoe ngebe mwenzangu, yaani sina msamaha hata kidogo na nilikuwa najulikana mpaka kuitwa 'Bud Spencer' enzi hizo. Wapambe wakachota mchanga na kutuambia tupute, nikaanza mimi kuputa...mwenzangu akawa anaogopa kwani alikuwa anajuwa muziki wangu au ni uwoga wake tu ulimzuia. Kwa kuwa nilikuwa na hasira sana, kigugumizi kikanishika na kuongea kumwambia jamaa apute mchanga siwezi. Kuangalia kando nikaona mpambe mmoja kashika kifuu anakifukia nikajuwa ni yeye ndiye kanifanya nishindwe kuongea. Ee bwana, nilimwacha yule jamaa niliyetaka kupigana naye na kumvamia mpambe, nilimtandika ile mbaya, nilimtwanga vichwa mpaka akapasuka midomo na kuvunja pua yake. Usiku nashangaa wanakuja yeye na Mama yake na polisi kuja kunikamata kunipeleka polisi. Nikaruka ukuta na kukimbilia Tandale kwa wahuni. Sikuonekana nyumbani wiki nzima kwani nilijuwa nakwenda kufungwa jela ya watoto.
 
Kama kuna demu unampenda unamvizia akienda kukojoa akitoka tu na wewe unaenda kukojolea kale kashimo kalikochimbwa na mkojo wake, haipiti hata siku lazima utamtafuna, binafsi nilisubiri sana kutafuna mademu kiulaini lakini ikawa bila bila.

Binafc niliamini kabisa kwamba ni hatari kuwa karibu na kondoo wakati mvua inanyesha, maana radi huwa inashuka kumtafuta ili ipigane nae.

Niliamini kwamba ili vita ya nchi na nchi ipiganwe basi unachorwa mstari mreeefu sana, halafu upande huu wanasimama wanajeshi wa nchi A na upande wa pili wanasimama wanajeshi wa nchi B halafu mashine zinaanza kuunguruma pale.
 
Kama kuna demu unampenda unamvizia akienda kukojoa akitoka tu na wewe unaenda kukojolea kale kashimo kalikochimbwa na mkojo wake, haipiti hata siku lazima utamtafuna, binafsi nilisubiri sana kutafuna mademu kiulaini lakini ikawa bila bila.

Binafc niliamini kabisa kwamba ni hatari kuwa karibu na kondoo wakati mvua inanyesha, maana radi huwa inashuka kumtafuta ili ipigane nae.

Niliamini kwamba ili vita ya nchi na nchi ipiganwe basi unachorwa mstari mreeefu sana, halafu upande huu wanasimama wanajeshi wa nchi A na upande wa pili wanasimama wanajeshi wa nchi B halafu mashine zinaanza kuunguruma pale.
Iyo haya ya mwisho, nimecheka sana
Wamarekani wao walikua wanachora mstari mpaka Afghanistan
 
4. Ukiona Kuku .........

23. Ukisikia milio ya watu wakigegedana CHOMEKA KISU kwenye mgomba, kikiingia chote watanasianaa adi ukichomoe mgegedo nao unachomokaa
 
Iyo namba 11 mother kanidanganya sana, nakumbuk ilivyo karibia kujifungua mdogo wangu aliniaga kuwa anaenda kununua mtoto hospital.
Nikaamin ivo, baada siku kadhaa akaja na kadogo kangu ka kike nikamwambia Mama umechagua katoto kazuri alicheka sanaa
 
N
ENZI ZA UTOTO TULIAMINI KWAMBA...
Kwa Wahenga tu si Kwa KIzazi cha Video Game

1. Ukiweka SINDANO kwenye RELI (aidha ya kirungu au ya kushonea) Basi TRENI ikipita itapinduka...

2. Ukila TUNDA lenye mbegu mfano chungwa, Bungo au Ubuyu, tulijitahidi tusimeze MBEGU, maana tukiamini kuwa ukimeza mbegu Mti wa ilo tunda utaota kichwani.

3. Tukiamni kuwa ukinyooshea kidole KABURI, basi kidole chako KITAOZA.

4. Ukiona Kuku wakipigana UKICHOMEKA KISU chini ardhini watapigana mpaka mmoja afe.

5. Mtu mwenye KIGUGUMIZI akiongea UKAFUNIKA KIFUU basi hataweza kuongea na atabakia anagugumia mpaka ukifunue.

6. Ukikutana na ALBINO temea mate KIFUANI/KITOVUNI kwako usipofanya hivyo nawe utakuja KUZAA kama huyo.

7. Tuliamini pia Albino HAWAFI, bali wanapotea tu Kimiujiza.

8. Ukihadithia HADITHI MCHANA basi utaota MKIA

9. Siku JUA likiwaka na MVUA kunyeesha basi sikuo hiyo SIMBA jike porini anazaa!
Na kama kuna mpira siku hiyo na Yanga anacheza basi matokeo yatakuwa sare.

10. Siku UKING'OA JINO tupa juu ya PAA la nyumba KUNGURU akilichukua jino lako ndio litaota jingine.

11. Watoto wote WANANUNULIWA hospitali au Wanaokotwa BAHARINI.

12. KONDOO ukimfunga kitambaa chekundu anapigana na radio iliyokua karibu yake.

13. Tuliamini kuwa wagonjwa wote wa akili (Vichaa na wendawazimu) kabla ya kuugua walikuwa ni WASOMI WAKUBWA SANA.

14. Ukiwa unanyonyoa KUKU/BATA usizungumze, ukizungumza tu MANYOYA yanarudi upya.

15. Tukiamini kuwa MAJAMBAZI ni Watu wenye sura ZINAZOTISHA, kama sura haitishi, basi sio Jambazi.

16. Ukitaka KUPIGANA na mwenzio ili kupata uhakika, unachora MSTARI na kumwambia ...KAMA WEWE MWAMBA VUKA HUO MSTARI, kitendo cha yeye kuvuka tu, ni ndundi tu, hakuna kuuliza mara ya pili.

Kama pembeni kuna mashabiki wapambe, watachota mchanga mkononi na kukwambia kama kweli unataka kupigana puta mchanga huu, kisha aliyekupa mchanga atakunja ngumi na kukwambia tia kidole hapa (Katikati ya kiganja chake), kitendo hicho tulikichukulia kama tusi kubwa sana na mtu kama kama kafanya hivyo basi kweli kadhamiria ugomvi na mtazipiga tu.

17. Kama unaangalia mpira na ukaona timu yako inataka kufungwa au ni pira wa penati, basi tuliamini UKIZIBANA SEHEMU ZAKO BINAFSI yule mpigaji penati atakosa na kupiga nje au juu au kipa atadaka.

18. Kama umekaa na UMENYOOSHA MIGUU, ikatokea mtu AMEKURUKA, basi atatakiwa arudi na kukuruka tena, hasipo fanya hivyo atasababisha yule aliyerukwa kutokukua yaani hato ongezeka kimo atabakia kuwa andunje.

19. kama mmekaa na mmoja wenu KASIMAMA, tuliokaa wote tuliamini yule aliyekaa atakuwa ANATUNYONYA DAMU.
Utasikia tu mtu analalamika, ebu kaa chini usitunyonye damu.

20. Watoto wa Kike walikuwa wanaweka mdudu (Fukufuku) kwenye manyonyo yao, wakiamini kuwa yatakuwa makubwa... Yule mdudu ilikuwa ukimuimbia, sikumbuki vizuri ule wimbo, ila ulikuwa kama hivi... Fukufuku toka nitakupa maji ya sukari... au Fukufuku toka baba yako kaja... (Na ajabu wale wadudu ukiwaimbia walikuwa wanatoka).

21. Kuna ndege wa Pwani, tukiwajua kwa jina la Yangeyange (Bata Maji) walikuwa weupe, wakiruka tukiwaimbia... Yangeyange tupe kucha nyeupe... Tukiamini kuwa kwa kuimba uko tutakuwa na kucha Nyeupe.

Ongeza Mengine Unayo Yakumbuka...View attachment 1090095
Nyingine ni hii. Kama ikatokea umechelewa kurudi Nyumbani basi ili usiulizwe au kuchapwa ulitakiwa kuokota mkaa au jiwe na ikiwa una karibia nyumbani unalilisha kwa nyuma na usiangalie nyuma mpaka utakapoingia ndani.
 
Kama umefanya kosa, unachomeka chelewa kwenye nywele ili usipigwe nyumbani. Au unatandaza vijiti mlangoni, akikanyaga tu anasahau.
 
daaa mkuuu mbavuuu zanguu
Binafsi nina kigugumizi. Siku moja utotoni mwangu, jamaa mmoja aliniudhi sana kwa kunitukania Mama yangu, basi tukapanga kupigana baada ya shule kwisha kwa ile siku. Tukaenda uchochoroni huku mie nikiwa na hasira ile mbaya, wapambe kibao walijaa kwani walikuwa wanajuwa mimi nikipigana lazima nimtoe ngebe mwenzangu, yaani sina msamaha hata kidogo na nilikuwa najulikana mpaka kuitwa 'Bud Spencer' enzi hizo. Wapambe wakachota mchanga na kutuambia tupute, nikaanza mimi kuputa...mwenzangu akawa anaogopa kwani alikuwa anajuwa muziki wangu au ni uwoga wake tu ulimzuia. Kwa kuwa nilikuwa na hasira sana, kigugumizi kikanishika na kuongea kumwambia jamaa apute mchanga siwezi. Kuangalia kando nikaona mpambe mmoja kashika kifuu anakifukia nikajuwa ni yeye ndiye kanifanya nishindwe kuongea. Ee bwana, nilimwacha yule jamaa niliyetaka kupigana naye na kumvamia mpambe, nilimtandika ile mbaya, nilimtwanga vichwa mpaka akapasuka midomo na kuvunja pua yake. Usiku nashangaa wanakuja yeye na Mama yake na polisi kuja kunikamata kunipeleka polisi. Nikaruka ukuta na kukimbilia Tandale kwa wahuni. Sikuonekana nyumbani wiki nzima kwani nilijuwa nakwenda kufungwa jela ya watoto.
 
Back
Top Bottom