Infopaedia
JF-Expert Member
- Oct 28, 2011
- 1,231
- 1,496
Wataalamu wanatumbia watoto huwa wana-act katika intelligent level baada ya ku-reason kulingana na mazingira na anachokielewa. Majibu ya watoto huwa yanafikirisha ama kushangaza. Juzi juzi nilipiga simu nyumbani nikawa naongea na dogo ana umri wa miaka mitano. Nikamuuliza unafanya nini, akajibu anaangalia mpira. Nikamuuliza nani na nani wanacheza, akajibu Iran na Spain (of course baada ya kuambiwa na mama yake). Nikamuuliza we unashabikia timu gani, akajibu Iran. Nikamuuliza dada yake yuko timu gani, akasema Spain. Nikamuuliza na kaka yako nae anashabikia timu gani, akaniambia hapana kwasababu team ziko mbili tu. Dah! nilicheka sana huku nawaza. Kweli watoto hawapendi maswali ya kijinga.
Hebu tupe kisa kimoja kama ulishawahi kukutana na majibu ya kushangaza ya watoto.
Hebu tupe kisa kimoja kama ulishawahi kukutana na majibu ya kushangaza ya watoto.