Applicant
JF-Expert Member
- Feb 12, 2020
- 1,962
- 1,746
Siamini kilichotokoea jana, kuna mwanamke amenizungusha sana mwezi wa3 huu, nikaona labda nitumie Nguvu ya Shilingi ya Kitanzania mambo yatakaa sawa, nikamualika Lunch akakubali, nikaona nisiongee sana, nikaziachia chips mayai na kuku ziongee, nikaiachia Saint Anna wine iongee, Nikayaachia maji ya Kilimanjaro ya Baridi yaongee.
Sikutaka kuongea kabisa siku hiyo maana nilishaongea sana bila mafanikio, Nikaamua niiachie pesa ya kitanzania iongee, baada ya kula tukiwa tunapiga story nikaweka Laki5 mezani nikamwabia hiyo itamsaidia kimatumizi.
Cha ajabu nayo alikataa, nikajua labda anaona aibu nikachukua pochi yake nimuwekee ndio akawa mkaliii "HUWEZI KUNIRUBUNI NISHAKWAMBIA SIPO TAYARII! " akaita bodaboda akaondoka zake na laki5 akaiacha.
Kuna wanawake wa ajabu sana.
Sikutaka kuongea kabisa siku hiyo maana nilishaongea sana bila mafanikio, Nikaamua niiachie pesa ya kitanzania iongee, baada ya kula tukiwa tunapiga story nikaweka Laki5 mezani nikamwabia hiyo itamsaidia kimatumizi.
Cha ajabu nayo alikataa, nikajua labda anaona aibu nikachukua pochi yake nimuwekee ndio akawa mkaliii "HUWEZI KUNIRUBUNI NISHAKWAMBIA SIPO TAYARII! " akaita bodaboda akaondoka zake na laki5 akaiacha.
Kuna wanawake wa ajabu sana.