DR. MWAKABANJE
JF-Expert Member
- Nov 7, 2012
- 1,986
- 3,150
Jamani kweli huyu naibu spika Jon Ndugai kwa kauli zake leo amelewa madaraka, mapema baada ya kipindi cha maswali na majibu, akiwa katika kutangaza matangazo mbalimbali, amewalaumu wapinzani pamoja na mambo mengine anasema wamekuwa wakilalamika kuwa kiti cha spika kinaupendeleo wakati si kweli.
Anasema robo 3 ya wabunge wote ni wa CCM na robo tu ni wa upinzani lakini kwenye kipindi cha maswli na majibu utaona kabisa kuwa wapinzani ni wengi kuliko wale wa CCM, na anasema anaweza amshawishi spika wabadili utaratibu ili kila wabunge 4 wanaouliza maswali 1 tu atoke upinzani. Binafsi nadhani Ndungai anataka kuzima hoja, hoja ya wapinzani na wananchi kwa ujumla, ni kwamba maamuzi ya spika yanakuwa yanapendela upande mmoja na sio uwiano anaousema wa kuuliza maswli.
Pili ndugai afahamu kuwa watanzania tunajua wabunge wa CCM walio wengi hawaibani serikali bali kuisupport serikali kwa kila kitu hvyo huwezi ukawaona wakiuliza maswali kama wapinzani.
Vilevile Ndugai amewaponda waandishi wa habari, kuwa wanatakiwa wariport habari zao kwa ufasaha, anasema unaposema wabunge wametoka nje ya bunge wakati wabunge wametoka nje ya ukumbi tu na wapo maeneo ya bunge(hawajatoka kwenye geti la bunge0 na ameendea kwa kusema mbunge mmoja anaweza toka, wabunge kwa makundi nk. Wasiwasi wangu ni kwamba kama na wenyewe huu ni utaratibu basi ni wa kipumbavu, kwamba wabunge wanaweza wakatoka nje ya ukumbi provided kwamba hawajatoka nje ya geti!
Je, Ndunngai, anaweza akawa nje ya darasa chuoni halafu mw. alete quiz aseme alikuwepo darasani kwa kuwa hakuwa nje ya geti la chuo?
Anasema robo 3 ya wabunge wote ni wa CCM na robo tu ni wa upinzani lakini kwenye kipindi cha maswli na majibu utaona kabisa kuwa wapinzani ni wengi kuliko wale wa CCM, na anasema anaweza amshawishi spika wabadili utaratibu ili kila wabunge 4 wanaouliza maswali 1 tu atoke upinzani. Binafsi nadhani Ndungai anataka kuzima hoja, hoja ya wapinzani na wananchi kwa ujumla, ni kwamba maamuzi ya spika yanakuwa yanapendela upande mmoja na sio uwiano anaousema wa kuuliza maswli.
Pili ndugai afahamu kuwa watanzania tunajua wabunge wa CCM walio wengi hawaibani serikali bali kuisupport serikali kwa kila kitu hvyo huwezi ukawaona wakiuliza maswali kama wapinzani.
Vilevile Ndugai amewaponda waandishi wa habari, kuwa wanatakiwa wariport habari zao kwa ufasaha, anasema unaposema wabunge wametoka nje ya bunge wakati wabunge wametoka nje ya ukumbi tu na wapo maeneo ya bunge(hawajatoka kwenye geti la bunge0 na ameendea kwa kusema mbunge mmoja anaweza toka, wabunge kwa makundi nk. Wasiwasi wangu ni kwamba kama na wenyewe huu ni utaratibu basi ni wa kipumbavu, kwamba wabunge wanaweza wakatoka nje ya ukumbi provided kwamba hawajatoka nje ya geti!
Je, Ndunngai, anaweza akawa nje ya darasa chuoni halafu mw. alete quiz aseme alikuwepo darasani kwa kuwa hakuwa nje ya geti la chuo?