kamsongole
Senior Member
- Apr 20, 2013
- 111
- 15
Kweli duniani hatupendani, juzi kati nimekaa na mtu wa nyanda za juu kusini tukapanga kuanzisha biashara ya kupika chakula kwenye sherehe mbalimbali.
Tukaweka mikakati kemkem na mipango mizuri, tukadhamiria kuanza kazi mara moja. Basi tukaanza kupanga nani tumshirikishe akawa anawataja watu wa kulekule.
Mimi bila hiana nikakubali, kumbe ndo najikaanga. Mara ndugu yule akaenda kuwataarifu wale ndugu juu ya mpango wetu. Nikashangaa mwenzao napigwa chini ghafla.
Mara yule hatufai tusimuweke wakati mimi ndiye nimeweka mpango mzima. Na jana tu nimetoka kuwakabidhi pesa ya chakula cha arusi ya jumapili kama katibu wa kamati hiyo.
Hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? Kweli dunia hadaa.
Tukaweka mikakati kemkem na mipango mizuri, tukadhamiria kuanza kazi mara moja. Basi tukaanza kupanga nani tumshirikishe akawa anawataja watu wa kulekule.
Mimi bila hiana nikakubali, kumbe ndo najikaanga. Mara ndugu yule akaenda kuwataarifu wale ndugu juu ya mpango wetu. Nikashangaa mwenzao napigwa chini ghafla.
Mara yule hatufai tusimuweke wakati mimi ndiye nimeweka mpango mzima. Na jana tu nimetoka kuwakabidhi pesa ya chakula cha arusi ya jumapili kama katibu wa kamati hiyo.
Hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? Kweli dunia hadaa.