Kwaresma na Pasaka Special Thread

SALA YAKUJIOMBEA ILI KUACHA MATENDO MAOVU
Mungu Mwenyezi, asante kwa kunipenda ingawa sijakamilika. Ninapambana na hali hii (itaje) na kadiri ninavyotaka kuacha, ninaendelea kurudi nyuma. Ninahisi aibu na uchovu. Ni Wewe pekee unayeweza kunisaidia kupambana na hali hii ili niweze kuacha. Niponye ndani na nje. Ikiwa kuna kitu chochote moyoni mwangu kinachonizuia kusonga mbele, nifunulie na unioneshe jinsi ya kukabiliana nacho. Ondoa hofu moyoni mwangu na unijaze nguvu ili niendelee kutembea katika roho na kweli. Amina.
Watakatifu Mikaeli, Gabrieli na Rafaeli malaika wakuu. Mtuombee.
 
Tusali malaika wa BWANA

Malaika wa BWANA alimpasha habari Maria naye akapata mimba kwa uwezo wa ROHO MTAKATIFU, salaam maria................
Ndimi mtumish wa BWANA nitendewe ulivyonena, salaam maria.................
Neno la MUNGU akatwaa mwili akakaa kwetu , salaam maria..........
Utuombee mzazi mtakatifu wa MUNGU tujaliwe ahadi za KRISTO
Tuombe...... Tunakuomba ee BWANA utie neema yako mioyoni mwetu ili sisi tuliojua kwa maelezo ya malaika kwamba kristo mwanao amejifanya mtu kwa mateso na msalaba wake tufikishwe utukufu na ufufuko wako. Tunaomba yote hayo kwa njia ya kristo BWANA wetu. AMINA
 
Rozary takatifu matendo ya uchungu

Siku ijumaa
Tendo la kwanza.
YESU anatoka jasho la damu, (Mariko 14:36) tumuombe MUNGU atujalie sikitiko la dhambi

Tendo la pili,
YESU anapigwa mijeledi, (Mariko 15:14-15)
Tumuombe MUNGU atujalie kuacha dhambi za uchafu

Tendo la tatu,
YESU anatiwa taji la miiba kichwani,(Mariko 15:16-17)
Tumuombe MUNGU atujalie kushinda kiburi

Tendo la nne,
YESU anachukua msalaba wake, (YOHANA 19:17-18)
Tumuombe MUNGU atujalie kuvumilia taabu

Tendo la Tano,
YESU anakufa msalabani, (yohana 19:30)
Tumuombe MUNGU atujalie kuwapenda YESU na maria
 
Hongera sana chief,pepo unayo mkononi kwa kujua kwako kufunga kwa imani yako but kama unadhani Mungu anapima kwa mzani mdogo kama huu wewe ndiye unayeshinda njaa.
Huyu anataka atuweke kwenye mashindano ya kufuturu
 
Tunaomba mafundisho zaid

Achen kukata tamaa tunaosoma ni wengi sana
 
Kesho mapema ibada ya majivu.

Tuombeane kwa Mungu azipokee toba zetu madhaifu na tabia mbovu tulizozoea kuziishi huko nyuma Kwaresma hii ikaziondoshe kwetu tubaki wasafi hata milele.
Tubun na kuiamin injili
 

Naomba kuuliza kama ifuatavyo!:!.
1️⃣ Je kwaresma ipo kwa madhehebu yote ya kikristo / kikristu au ni special kwa wakatoliki peke yao?
2️⃣ Je makanisa au madhehebu yote yanayoadhimisha kwaresma ni lazima kujichora misalaba myeusi kwenye mapaji ya uso au hili ni kwa wakatoliki peke yao?
Nauliza hivi kwa sababu siku moja nilikuwa naongea na dada mmoja msabato akasema kwenye usabato hawana sikukuu ya krismas wala pasaka ila sikukumbuka kumuuliza kuhusu kwaresma kama kwenye usababato ipo au haipo?!
 
Asante sana kwa swali zuri

Kwaresma ipo kwa ajili ya watu wote lakini si kwa kila mtu

Baadhi ya madhehebu huamisha kwaresma kwa ukubwa kama Lutheran, Anglican, catholic, Moravian na mengine mengi lakini siyo yote, madhehebu mengine hupinga kwaresma kwa sababu ambazo wanazijua wao

Kupaka MAJIVU usoni ni thehebu ya Catholic pekee ndo hupaka MAJIVU uson, Sina uhakika kama na Lutheran nao hupaka majivu

Hao watu wanaoitwa wasabato achana nao wao ni wapinga KRISTO na wako wazi wala hawajifichi
 
Mh! aisee!
Kipengele kinachosema " kwaresma ipo kwa ajili ya watu wote lakini si kwa kila mtu " sijakuelewa! " Kwa ajili ya watu wote " kivipi ?! Hadi wapagani ?! Halafu si kwa kila mtu kivipi wakati ni kwa ajili ya watu wote ?! Kitu kikiishakuwa ni kwa ajili ya watu wote si tayari kinakuwa ni kwa kila mtu ?! Watu wote ndiyo kila mtu !
 
Jumamos ya jumuiya

Masomo jumuiya ya leo
Isaya 58:9-14
Luka 5:27- 32
Zaburi 86:1-6
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…