Askofu Gwajima atunukiwa PhD (Doctor of Philosophy)

popo1986

JF-Expert Member
Jul 30, 2014
1,120
371
Leo majira ya saa kumi jioni maeneo ya ubungo katika ukumbi wa Blue Pearl..askofu Josephat Gwajima wa kanisa la ufufuo na uzima, ametunukiwa nishani ya "Doctor of philosopy in Theology...PhD", ambayo amekuwa akiisomea kupitia chuo cha Omega Global University chenye makao makuu yake South Africa...

Nnilishuhudia leo umati wa wakazi wa DSM wakielekea na kutoka pale blue pearl Hotel ubungo plaza..

shikamoo.. Bishop,Dr. J.Gwajima.:smile-big:
Leo Jumamosi hii ya Tarehe 7-03-2015, Mchungaji Kiongozi na mwanzilisha wa makanisa ya Ufufuo na Uzima Duniani, Askofu Dr. Josephat Gwajima anatunukiwa Shahada ya Falsafa (Doctor of Philosoph) PHD na Chuo Kikuu Cha Wamarekani OMEGA ambacho makao yake makuu kwa Africa yako Afrika Kusini. Mahafali hayo ambayo yamefanyika katika Ukumbi mkubwa wa Plue Pearl (Ubungo Plaza), yalihudhuriwa na maelfu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, Viongozi wa Dini na Maprofesa kutoka Chuo Kikuu cha OMEGA.

Shahada hii pia inajumuisha kazi na mchango wake kwa jamii ya Tanzania, Africa na Duniani kwa Ujumla. Machache kati ya kazi Zake

A) Askofu Dr. Josephat Gwajima, katika uchunguzi wake amegundua Injili iliyoletwa na wakoloni iliyopelekea kujengwa kwa makanisa na madhehebu mbalimbali ilikuwa na lengo la kiutawala. haikulenga hasa kujenga msingi wa Neno la Kweli lakini ililenga kuwafanya waafrika watawalike. misingi hii ambayo bado tunaitumia mpaka leo si uhalisi wa Biblia. Askofu Dr. Josephat Gwajima, amekuja na uchunguzi wake uliopelekea kuandikwa kwa kitabu "THE AFRICAN CHURCH IN AN AFRICAN PERSPECTIVE" ambacho kimetafsiriwa kwa kishwahili kama 'Kanisa la Afrika Katika Mtazamo wa Kiafrika' . Katika Kitabu hiki anaelezea misingi ya kweli ya Kibiblia katika kuanzisha na kuendeleza makanisa yetu Afrika.

B). Askofu Dr. Josephat Gwajima, ametunga kitabu maarufu 'Maombi ya Kushindana" ambacho kimetafsiriwa kwa lugha 16, nakala ya kitabu hicho ni moja kati ya nakala zinazoongoza kwa usambazaji hapa Tanzania, Kenya, Uganda, Afrika Kusini na nchi nyingine.

C).Askofu Dr. Josephat Gwajima, ametunga kitabu "Ressuraction and Life' ambacho kimetafsiriwa kwa lugha ya Kijapan, kiingereza na kikorea. kitabu hiki ni maarufu sana Nchini Japan na kinashika nafasi za juu katika usambazaji wake nchini humo.

D). Mbali na Nakala hizo lakini pia Askofu Dr. Josephat Gwajima, Ametunga Vitabu ambavyo ni maarufu hapa Tanzania na Duniani kama vifuatavyo.


MSINGI WA KIROHO
KANUNI YA KUJENGA KANISA LA MAELFU (MEGA CHURCH)
GHARAMA YA KUJENGA KANISA LA MAELFU
NENO NI MUNGU NA MUNGU NI NENO
USHINDI KWA DAMU YA YESU
SILAHA ZA VITA VYETU
VIFUNGO VYA ROHONI, MWILINI NA NAFSINI.
HATARI YA NDOTO
MAOMBI YA KUBOMOA MADHABAHU
SHERIA MBILI ZA ROHONI
JINSI YA KUTUNZA MUUJIZA WAKO
MASHETANI KATIKATI YA UZAO WA WANAADAMU
KIBALI KILICHO IBIWA
FUMBO LA MAUTI
KULOGA KWA KUPIGA MAFUNDO
MICHORO YA GIZA
MIMI SI KAMA WALE
USINGIZI WA KICHAWI
DAMU INENAYO MEMA
VIKAO VYA UHARIBIFU
BARAKA KATIKA MAPAMBANO
NGUVU YA MSALABA
UBATIZO WA KIBIBLIA
MKATE WA KILA SIKU
SERIKALI YA MASHETANI
MAOMBI YA KUGHAIRISHA MABAYA YALIYOPANGWA YAMPATE MTU
MAJESHI YA WAFU
SHERIA ISHIRINI ZA UONGOZI


E). Askofu Dr. Josephat Gwajima, amekuwa mstari wa mbele kukemea kwa uwazi propaganda za Udini zinazojipenyeza kwenye misingi ya Dola hili la Kidemokrasia.

F). Askofu Dr. Josephat Gwajima, Pia Amekemea kwa Uwazi serikali ya nchi hii pale ilipokwenda kinyume na maadili ya uongozi bora na misingi ya haki kama vuguvugu la Ugonjwa wa Dengu, Mauaji ya Albino na kuwakemea watawala wanaokwenda kinyume na maadili ya utumishi wao. pia amekuwa mstari wa mbele kuipongeza serikali kwenye hatua zake za kuwaletea maendeleo wananchi wake.

G).Askofu Dr. Josephat Gwajima, ametembelea na kufanya mikutano zaidi ya nchi 38 za Afrika, Marekani, Canada, nchi zote za Ulaya zinazounda shirikisho la Umoja wa Ulaya, Uingereza, japan, Korea, China, na katika mikutano yake yote hiyo imekuwa ikihudhuriwa na maelfu ya watu ambayo inapatikana Youtube.

Kila la Heri Askofu Dr. Josephat Gwajima.



255718104333-1370316994.jpg
IMG-20150307-WA0231.jpg
IMG-20150307-WA0240.jpg
IMG-20150307-WA0241.jpg
IMG-20150307-WA0237.jpg

 
mkuu aliwai kusoma maswala haya haya ya Theology kabla hawajamkabidhi nilisikia wakisoma wasifu wake kuanzia level ya certificate hadi juu......wenzetu wapo serious
 
Hii habari hapa chini inaweza kulisaidia jukwaa kuelewa juu ya hiki kinachoitwa "Omega Global University".

Aya ya mwisho inatupa picha ya aina ya "Phd" aliyotunukiwa mtumishi wa Mungu.



Mayor Mdaka´s honorary "doctorate" under scrutiny
News - Date: 19 February 2010

Written by: News Correspondent / Viewed: 2856




The mayor of the Vhembe District Municipality, Cllr Falaza Mdaka, was recently awarded an honorary doctor’s degree by the Omega Global University, but many people have asked the question whether it is worth the paper it’s written on.

The Witbank-based “university” awarded the honorary degree to Cllr Mdaka for “his perpetual effort to make the lives of other people better.” The ceremony took place a fortnight ago and other people who have been honoured in this way include well-known choral master Shalati Joseph Khosa of Phalaborwa, Tinyiko Elphas Khosa, who started New Era College years ago, and Gabriel Ngomane, a businessman from Mpumalanga.

The term “honorary doctorate” normally refers to a very prestigious title conferred upon an outstanding individual by an institute of higher education. In South Africa, this is normally awarded by one of the registered universities. In the University of Johannesburg’s Charter for Honorary Degrees, an honorary doctoral degree is described as:

“… an academic award that entitles the honoured person to bear the doctoral title honoris causa in recognition of his/her outstanding academic contributions that do not however meet the requirements set in the University Rules or the Act for the conferment of a doctoral degree as a result of the successful completion of a recognized programme of study of the University.”

In certain cases, doctoral titles are also conferred upon people based on their contributions to the community. Again in the case of the University of Johannesburg, it is stated that such an award “… is based on relevant outstanding intellectual contributions and/or relevant outstanding contributions to public life.”

The universities in South Africa are also very conservative in as far as the awarding of such degrees is concerned. Recipients of such degrees include former president Nelson Mandela and Archbishop Desmond Tutu. The charter also stresses this fact by stating: “A conservative awards policy is followed, in order to emphasize the extraordinary and inherent value of the awards.”

The Omega Global University is not listed as a registered South African University. On their website, this institution invites people to apply for an honorary doctor’s degree. It states that “Omega Global University offers honorary Doctorate degrees to deserving candidates based on their life experience.” To qualify for such a degree, you also only need “at least 5 years of work or life experience relevant to (the) desired major.” Interested parties can also apply online for such a degree.
 
Leo Jumamosi hii ya Tarehe 7-03-2015, Mchungaji Kiongozi na mwanzilisha wa makanisa ya Ufufuo na Uzima Duniani, Askofu Dr. Josephat Gwajima anatunukiwa Shahada ya Falsafa (Doctor of Philosoph) PHD na Chuo Kikuu Cha Wamarekani OMEGA ambacho makao yake makuu kwa Africa yako Afrika Kusini. Mahafali hayo ambayo yamefanyika katika Ukumbi mkubwa wa Plue Pearl (Ubungo Plaza), yalihudhuriwa na maelfu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, Viongozi wa Dini na Maprofesa kutoka Chuo Kikuu cha OMEGA.

Shahada hii pia inajumuisha kazi na mchango wake kwa jamii ya Tanzania, Africa na Duniani kwa Ujumla. Machache kati ya kazi Zake

A) Askofu Dr. Josephat Gwajima, katika uchunguzi wake amegundua Injili iliyoletwa na wakoloni iliyopelekea kujengwa kwa makanisa na madhehebu mbalimbali ilikuwa na lengo la kiutawala. haikulenga hasa kujenga msingi wa Neno la Kweli lakini ililenga kuwafanya waafrika watawalike. misingi hii ambayo bado tunaitumia mpaka leo si uhalisi wa Biblia. Askofu Dr. Josephat Gwajima, amekuja na uchunguzi wake uliopelekea kuandikwa kwa kitabu "THE AFRICAN CHURCH IN AN AFRICAN PERSPECTIVE" ambacho kimetafsiriwa kwa kishwahili kama 'Kanisa la Afrika Katika Mtazamo wa Kiafrika' . Katika Kitabu hiki anaelezea misingi ya kweli ya Kibiblia katika kuanzisha na kuendeleza makanisa yetu Afrika.

B). Askofu Dr. Josephat Gwajima, ametunga kitabu maarufu 'Maombi ya Kushindana" ambacho kimetafsiriwa kwa lugha 16, nakala ya kitabu hicho ni moja kati ya nakala zinazoongoza kwa usambazaji hapa Tanzania, Kenya, Uganda, Afrika Kusini na nchi nyingine.

C).Askofu Dr. Josephat Gwajima, ametunga kitabu "Ressuraction and Life' ambacho kimetafsiriwa kwa lugha ya Kijapan, kiingereza na kikorea. kitabu hiki ni maarufu sana Nchini Japan na kinashika nafasi za juu katika usambazaji wake nchini humo.

D). Mbali na Nakala hizo lakini pia Askofu Dr. Josephat Gwajima, Ametunga Vitabu ambavyo ni maarufu hapa Tanzania na Duniani kama vifuatavyo.


  1. MSINGI WA KIROHO
  2. KANUNI YA KUJENGA KANISA LA MAELFU (MEGA CHURCH)
  3. GHARAMA YA KUJENGA KANISA LA MAELFU
  4. NENO NI MUNGU NA MUNGU NI NENO
  5. USHINDI KWA DAMU YA YESU
  6. SILAHA ZA VITA VYETU
  7. VIFUNGO VYA ROHONI, MWILINI NA NAFSINI.
  8. HATARI YA NDOTO
  9. MAOMBI YA KUBOMOA MADHABAHU
  10. SHERIA MBILI ZA ROHONI
  11. JINSI YA KUTUNZA MUUJIZA WAKO
  12. MASHETANI KATIKATI YA UZAO WA WANAADAMU
  13. KIBALI KILICHO IBIWA
  14. FUMBO LA MAUTI
  15. KULOGA KWA KUPIGA MAFUNDO
  16. MICHORO YA GIZA
  17. MIMI SI KAMA WALE
  18. USINGIZI WA KICHAWI
  19. DAMU INENAYO MEMA
  20. VIKAO VYA UHARIBIFU
  21. BARAKA KATIKA MAPAMBANO
  22. NGUVU YA MSALABA
  23. UBATIZO WA KIBIBLIA
  24. MKATE WA KILA SIKU
  25. SERIKALI YA MASHETANI
  26. MAOMBI YA KUGHAIRISHA MABAYA YALIYOPANGWA YAMPATE MTU
  27. MAJESHI YA WAFU
  28. SHERIA ISHIRINI ZA UONGOZI

E). Askofu Dr. Josephat Gwajima, amekuwa mstari wa mbele kukemea kwa uwazi propaganda za Udini zinazojipenyeza kwenye misingi ya Dola hili la Kidemokrasia.

F). Askofu Dr. Josephat Gwajima, Pia Amekemea kwa Uwazi serikali ya nchi hii pale ilipokwenda kinyume na maadili ya uongozi bora na misingi ya haki kama vuguvugu la Ugonjwa wa Dengu, Mauaji ya Albino na kuwakemea watawala wanaokwenda kinyume na maadili ya utumishi wao. pia amekuwa mstari wa mbele kuipongeza serikali kwenye hatua zake za kuwaletea maendeleo wananchi wake.

G).Askofu Dr. Josephat Gwajima, ametembelea na kufanya mikutano zaidi ya nchi 38 za Afrika, Marekani, Canada, nchi zote za Ulaya zinazounda shirikisho la Umoja wa Ulaya, Uingereza, japan, Korea, China, na katika mikutano yake yote hiyo imekuwa ikihudhuriwa na maelfu ya watu ambayo inapatikana Youtube.

Kila la Heri Askofu Dr. Josephat Gwajima.

pic 2.jpg

photo 1.JPG

 
Baada ya kutunukiwa PhD ya Theology....na Chancellor wa chuo kikuu cha south Africa OMEGA GLOBAL UNIVERSITY hizi ni baadhi ya pic zake askofu Josephat Gwajima mzee wa misukule
 

Attachments

  • IMG-20150308-WA0001.jpg
    IMG-20150308-WA0001.jpg
    124.3 KB · Views: 1,094
  • IMG-20150308-WA0000.jpg
    IMG-20150308-WA0000.jpg
    117.4 KB · Views: 1,148
  • IMG-20150307-WA0202.jpg
    IMG-20150307-WA0202.jpg
    95.4 KB · Views: 1,100
  • IMG-20150307-WA0236.jpg
    IMG-20150307-WA0236.jpg
    111.8 KB · Views: 983
  • IMG-20150307-WA0239.jpg
    IMG-20150307-WA0239.jpg
    82.5 KB · Views: 1,051
daa kwa kweli huyu jamaa sio mchezo huyu anamaanisha huyu.
 
wenzetu wanafanya vitu vinavyoonekana, sisi tumekazania kufanya mambo ya aibu aibu tu.. !!tunang'ang'ania mambo ya kipuuzi yasiyutupatia ugali.. Hongereni kwa kweli.. mahakama ya Kadhi italeta nini!!!??.. badala ya kujikita kwenye elimu, Utunzi wa vitabu, tunang'ang'ania mambo ya aibu.. ai inatia Khisiran sana..
 
Hajapata mgao wa Rugemarila huyu? Anaonekana yupo poa. Tatizo kuzaa na wake za watu.
 
A weke CV yake tuone mtiririko wa elimu! Huu ni ujanja ujanja


UOTE=weed;12088627]amen amen amen!ila hatijaua kama kabla ya kusoma hiyo PhD aliwahi kusoma hata degree??[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom