vibertz
JF-Expert Member
- Mar 15, 2022
- 3,091
- 5,785
yanga kuwa na uhitaji na mzize ni sawa na mzazi asiyeweza kumtunza mwanae...
halafu anakataa mwanawe kuchukuliwa na kulelewa na mtu mwenye uwezo...
mzize hajaamua kubaki yanga, amelazimika abaki ndio maaana amewaambia muongeze mshahara...
angeamua kwaa maapenzi yake, asingetaka maboresho ya mkataba.
Mkuu unaelewa unachoongea kweli? Mtu asiyetaka kubakia huwa hana nia wala haja ya kuomba maboresho ya mshahara bali anashinikiza kuondoka ili akapate changamoto sehemu nyingine. Mtu anayeomba kuboreshewa mshahara maanake ameridhia kubakia kwa masharti na vigezo.
Hilo la mfano wako wa mzazi asiyeweza kumtunza mwanae sijui umewaza nini? Matunzo kwa mtoto ni malezi na kumfundisha yaliyo bora na mazuri. Thamani na ubora wa Mzize mnaouona sasa umepandishwa na nani kama sio walimu waliopo Yanga? Sasa unasemaje kuwa hakutunzwa wakati leo mchezaji anaonekana lulu kutokana na matunzo bora aliyoyapata.