Kwanini wengi hukiogopa kifo /kufa?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,617
Reaction score
860,794
nimerejea kwenye mfululizo wetu ule wa makala zinazohusiana na kiama kifo kuzimu makaburini na hata mochwari
Ndani za hizo makala kuna nyingine ni za kutiana moyo na kuondoana hofu huku nyingine zikielezea dhana mbalimbali na nyingine zikiwa ni masimulizi ya kweli
Nia yangu si kuleta hofu wala kumtisha mtu bali kupandikiza mbegu ya uzoevu katika vitu visivyozoeleka.... Hasa kifo
Hofu ya wengi kwenye kifo ni hii
Kwamba hatutaonana na wapendwa wetu tena
Kwamba miili yetu hii itaharibika na kuoza kabisa
Kwamba hatuna hakika na huko tuendako
Kwamba je ni kweli kuna pepo jehanam au rebirth/reincarnation?
Kwamba tunaachana na starehe za dunia hii na mali zote tulizochuma?
Lakini kubwa zaidi ni ule upweke kile kiza na zile kilo za mchanga ndani chini ya kaburi pekeyako kabisa .....na zile hari za kifo mwili unapotengana na roho I mean yale mateso yake zile dakika na sekunde za mwisho
Mbali ya hayo yote ni zile fikra za wale wapendwa wetu waliotangulia huko, kwamba wako wapi sasa na wanafanya nini huku ukionyeshwa mapicha ya marehemu Waliobaki mifupa tuu.....
Usimlaumu anayeogopa kifo ndani ya kaburi lililofunikwa kuna siri nyingi tusizozijua
 
Uzuri wa kifo ni kuwa
Pale ambapo kifo kipo binadamu hayupo na pale ambapo binadamu yupo kifo hakipo, ukifa unakuwa haupo so hakuna haja ya kuogopa, na unaogopa kwa kuwa upo.
Wala haina haja ya kutishana, kifo ni moja ya ugunduzi bora kabisa kuwahi tokea ulimwenguni, kinatoa chance ya kizazi kimoja kurithisha dunia kizazi kingne.
 
Kifo ni fumbo tata na imepelekea binaadam wengi kujaribu kulifumbua kupitia iman au mapokeo lakini imebaki ni fumbo gumu sababu hakuna alie rudi kutoa ushuhuda na hata ukiona misimamo yetu kwa imani zetu ni kujaribu kupata ahueni tu kwa fumbo hili sijui paradiso au jehanamu ni kujaribu tu kutafsiri kitu ambacho hatuwezi mpaka tuwe hiyo hali tu ndo tutapata uhalisia
 
Kifo! Sidhani kama nakiogopa.
Huwa nina kauli moja inayonipa ujasiri "kama siku zako zimefik utakufa tu hata kama umejificha uvunguni "
 
Mkuu watu wanaogopa kifo sababu wengi wao ni watu waovu kwaiyo wanajua wakifa tu ni mwendo wa kipondo mwanzo mwisho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…