The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,425
Ukimsikiliza mkuu wa machawa mkumbo madelu akihimiza amani, unashangaa.
Kunawezekana kuwa na amani bila haki?
Je, amani inalazimishwa au inatokana na aina ya maisha ya wahusika?
Je, hawa wanolazimisha amani wanayo amani?
Wanaijua amani bila kuijua haki?
Je, amani ni nini na inasababishwa na nini?
Je, Tanzania kuna amani ya kweli au amani ya imani kama siyo ya kulazimisha?
Je, kwa mazingira yetu yaliyojaa na kutawaliwa na ubinafsi, ufisi, na ufisadi, kunaweza kuwapo amani ya kweli?
Je, kama taifa, tunataka amani au haki kwanza?
Je, kwanini watawala wa. hovyo na lazimishi wanahubiri amani na kupuuza haki?
Je, hii amani ya imani na ya pwagu na pwaguzi ya kulazimisha itadumu bila. haki?
Kipi kianze kwanza kati ya haki na amani?
Najiwazia kimya kimya.