Kwanini Watanzania wengi hawasomi vitabu?

Kwanini Watanzania wengi hawasomi vitabu?

I am inspired!

Mkuu! Binafsi ni mpenzi sana wakusoma vitabu, lakini sometimes napata shida, nasahau some information nilizosoma kwenye kitabu.

Swali langu linakuja, ni kwanamna gani unaweza absorb too much information bila ya kusahau? Je kuna techniques au ni umezaliwa hivyo, au sisi wengine tuna low IQ😁
Kwanza kabisa si muhimu kukumbuka kila kitu ulichosoma. Kuna mambo mengi yanaandikwa kuchombeza narrative, unatakiwa kujua kipi ni muhimu hutakiwi kusahau, na kipi si muhimu unaweza kusahau bila kupoteza maana ya kitabu. Ikibidi hata kwa kuandika points muhimu.

Mimi napenda si tu kusoma vitabu, bali pia hata kufuatilia mazungumzo ya waandishi wa vitabu kama ya kwenye vipindi vya BBC World Service, C-SPAN, Book TV etc. Ukifuatilia mazungumzo haya utagundua kuwa hata waandishi wenyewe wa vitabu, ingawa wameviandika na ni wataalamu wa subject matter, mara nyingi hawakumbuki kila kitu walichoandika. Kumbukumbu za kiutu haziruhusu kukumbuka hivyo, ingawa kuna watu wanaweza kukumbuka mengi zaidi ya wengine, possibly kwa sababu wame specialize kwenye kitu fulani. Ni rahisi kwa profesa wa historia kukumbuka mambo mengi sana kuhusu vitabu vyake vya historia kwa sababu labda kafundisha somo hilo kwa miaka mingi na hata vitabu vyake vinatokana na notes zake za darasani.

Which brings another point, njia moja nzuri ya kukumbuka ni kufundisha, kuhadithia, kuelezea. Mimi nina tabia hiyo sana. Mara nyingi utakuta hata hapa JF huwa naelezea sana mambo ya kwenye vitabu nilivyosoma au documentaries nilizoona, inasaidia kuelimisha wengine lakini pia inanisaidia hata mimi kuweza kuelewa na kukumbuka hilo jambo vizuri, na pengine ninapokuwa naona kuna pengo, narejea kusoma nikumbuke vizuri, kama kitu ni muhimu.

Pia, kwenye mambo ya muhimu ni vizuri kusoma kwa intention, unataka kupata nini kutoka hicho kitabu? Ukisoma hivyo utakuwa unatengeneza uelewa ulio na logical consistency ambao umejiunganisha na mambo mengine.

Mimi napenda sana kusoma vitabu vya marais wa Marekani, nchi ninayoishi sasa. Nimesoma "Truman" cha David McCullough na set ya vitabu vitatu vya Lyndon B Johnson vya Robert Caro. Siwezi kukumbuka kila kitu. Kitabu cha Truman kina kurasa 1120. Vya Robert Caro viko vitatu. Siwezi kukumbuka kila kitu, lakini, leo ukiniambia habari ambayo haipo kabisa katika maisha ya Truman,kwa mfano Truman alikuwa Nazi, au alikuwa ni draft dodger, nitakataa kusema tuupime ushahidi zaidi, kwa sababu habari hiyo haipo katika account ya David McCullough.

Mimi hupenda kuunganisha facts na larger narrative ili kukumbuka, na in fact kuelewa zaidi ya kukumbuka. Ni kama unavyoweza kuelewa hesabu ukaweza kuifanya tena na tena bila kutegemea sana kukumbuka. Ila kukumbuka kila kitu kwenye kitabu cha kurasa 1120 ni vigumu na wala kitabu hakikuandikwa kwa nia hiyo.

Hata mimi pia kuna mengi sikumbuki na pengine sikumbuki hata kuwa sikumbuki mpaka ninapokuwa kwenye maongezi stimulating kuhusu hizo mada, na hapo ndipo najipima na kujua nakumbuka yapi na yapi inabidi kuyarejea.
 
Tupe hints kidogo kwa kile ulichokipata
Mkuu,

Wanaojua kuandika wanajua kuwa ni kazi kubwa kuandika kidogo kuliko kuandika mengi, kwa sababu kuandika kidogo na kukamata mambo muhimu yote ni kazi kubwa kuliko kuandika kwa urefu.

Landa tuanzishe nyuzi za marejeo ya vitabu (Book Review) watu wawe wanakuja kufanya reviews za vitabu walivyosoma na kwa kupitia nyuzi hizo kuweza kufanya mazungumzo zaidi ya kuhusu mada hizo na kuchochea watu zaidi kusoma, na wao kuandika marejeo yao ya vitabu.

Hili naweza kufanya nikiwa na muda.
 
Maisha yetu hayaendani na vitabu na ni vigumu sana kutumia vitabu ktk maisha ya kitanzania na ukafanikiwa
Ebu chukua kitabu rich dady poor dady kilete ktk maisha ya kitanzania uone km kitakusaidia kutajirika na kua na mafanikio
Hicho kitabu kina maarifa ya kutosha kabisa mazingira yoyote
 
Saa hizo hizo 24 unasoma vitabu ukitaka.

Ni suala la interest

Kuna muda unaweza kuutumia kufanya vitu zaidi ya kimoja, mfano ukiwa kwenye safari kwenye basi, treni ndege au boti umepata kiti, unaweza kutumia muda huo kusoma. Ukiwa unasubiri appointment ya daktari au uko ofisi za watu unangojea kufikiwa, unaweza kusoma.

Saa 1 ya kusafiri ukiitumia kusafiri na kusoma hapo utakuwa umefanya vitu vya saa 2 ndani ya saa 1. Umesafiri kwa saa 1, lakini pia, umesoma kitabu kwa saa 1.

Siku ya masaa 24 lakini ndani ya hiyo siku unaweza kufanya mambo ya zaidi ya masaa 24, parallelly.

Kuna vitabu unaweza kuvimaliza hata kwa masaa machache tu.

Jana nimeona kuna kitabu unaweza kusoma kwa masaa matatu. That is just two footbal matches.

Siku hizi kuna mpaka audiobook kwa mtu ambaye anataka kusikiliza kitabu kinasomwa huku anafanya kitu kingine kama mazoezi au kuendesha gari.

Pia si lazima usome vyote, na si vyote vinatakiwa kusomwa mwanzo mpaka mwisho, vingine ni for reference, na hata unavyoanza kusoma si lazima kumaliza, vingine unaweza kuanza kusoma ukaona hiki hakifai ukaacha, ila kusoma muhimu.

Mwezi huu wa December tu nimemaliza kusoma vitabu vitatu

1. "Nexus: A Brief History of Information Networks from the Stone Age to AI" by Yuval Noah Harari.

2. "The Burning Earth: An Environmental History of the Last 500 Years" by Sunil Amrith

3. "The Achilles Trap: Saddam Hussein, the C.I.A., and the Origins of America's Invasion of Iraq" by Steve Coll.

Na kabla ya mwaka mpya namaliza kingine cha nne.

So niki average 4 books a month, that's 48 books a year.

Na hivi ni vitabu vikubwa, vitabu vidogo naweza kusoma zaidi ya 48 kwa mwaka.

Halafu baada ya kusoma kitabu cha a multiple Pulitzer prize winner na kuabsorb heavily researched informatio unakuja hapa JF unabishana na mtu anayesema the earth is flat!
Akhsante kwa ushauri.

Nianze kusoma vitabu ninavyovitaka kwenye mambo nayoyalenga
 
Kwanza kabisa si muhimu kukumbuka kila kitu ulichosoma. Kuna mambo mengi yanaandikwa kuchombeza narrative, unatakiwa kujua kipi ni muhimu hutakiwi kusahau, na kipi si muhimu unaweza kusahau bila kupoteza maana ya kitabu. Ikibidi hata kwa kuandika points muhimu.

Mimi napenda si tu kusoma vitabu, bali pia hata kufuatilia mazungumzo ya waandishi wa vitabu kama ya kwenye vipindi vya BBC World Service, C-SPAN, Book TV etc. Ukifuatilia mazungumzo haya utagundua kuwa hata waandishi wenyewe wa vitabu, ingawa wameviandika na ni wataalamu wa subject matter, mara nyingi hawakumbuki kila kitu walichoandika. Kumbukumbu za kiutu haziruhusu kukumbuka hivyo, ingawa kuna watu wanaweza kukumbuka mengi zaidi ya wengine, possibly kwa sababu wame specialize kwenye kitu fulani. Ni rahisi kwa profesa wa historia kukumbuka mambo mengi sana kuhusu vitabu vyake vya historia kwa sababu labda kafundisha somo hilo kwa miaka mingi na hata vitabu vyake vinatokana na notes zake za darasani.

Which brings another point, njia moja nzuri ya kukumbuka ni kufundisha, kuhadithia, kuelezea. Mimi nina tabia hiyo sana. Mara nyingi utakuta hata hapa JF huwa naelezea sana mambo ya kwenye vitabu nilivyosoma au documentaries nilizoona, inasaidia kuelimisha wengine lakini pia inanisaidia hata mimi kuweza kuelewa na kukumbuka hilo jambo vizuri, na pengine ninapokuwa naona kuna pengo, narejea kusoma nikumbuke vizuri, kama kitu ni muhimu.

Pia, kwenye mambo ya muhimu ni vizuri kusoma kwa intention, unataka kupata nini kutoka hicho kitabu? Ukisoma hivyo utakuwa unatengeneza uelewa ulio na logical consistency ambao umejiunganisha na mambo mengine.

Mimi napenda sana kusoma vitabu vya marais wa Marekani, nchi ninayoishi sasa. Nimesoma "Truman" cha David McCullough na set ya vitabu vitatu vya Lyndon B Johnson vya Robert Caro. Siwezi kukumbuka kila kitu. Kitabu cha Truman kina kurasa 1120. Vya Robert Caro viko vitatu. Siwezi kukumbuka kila kitu, lakini, leo ukiniambia habari ambayo haipo kabisa katika maisha ya Truman,kwa mfano Truman alikuwa Nazi, au alikuwa ni draft dodger, nitakataa kusema tuupime ushahidi zaidi, kwa sababu habari hiyo haipo katika account ya David McCullough.

Mimi hupenda kuunganisha facts na larger narrative ili kukumbuka, na in fact kuelewa zaidi ya kukumbuka. Ni kama unavyoweza kuelewa hesabu ukaweza kuifanya tena na tena bila kutegemea sana kukumbuka. Ila kukumbuka kila kitu kwenye kitabu cha kurasa 1120 ni vigumu na wala kitabu hakikuandikwa kwa nia hiyo.

Hata mimi pia kuna mengi sikumbuki na pengine sikumbuki hata kuwa sikumbuki mpaka ninapokuwa kwenye maongezi stimulating kuhusu hizo mada, na hapo ndipo najipima na kujua nakumbuka yapi na yapi inabidi kuyarejea.
Hii nimeelewa kabisa bila chenga!
 
Acha vitabu, hàta mabango ya barabarani hawasomi. Mtu anauliza mtaa huku kashika bango lililoandikwa jina la mtaa anaouliza.
Angalia matangazo mtandaoni yameandikwa Bei ila watu kwenye comments kila mmoja anauliza bei ya hiyo bidhaa.
Tz ndio nchi yenye watu wenye Iq ndogo sana
 
Akhsante kwa ushauri.

Nianze kusoma vitabu ninavyovitaka kwenye mambo nayoyalenga
Naam,

Unaweza kuona mtu anasoma vitabu vingi vya Project Management ukataka kuiga na wewe usome, kumbe mwenzako ni Project Manager anasoma vitu avifanyie kazi kazini kwake, wewe unasumbuka kusoma mambo ambayo kwako hayana practical use kwa sababu huna hata matumaini ya kufanya kazi hiyo.

Ni muhinu kujua muktadha, hata vitabu vya nje Marekani, Ulaya, Asia, mangapi unaweza kuyahamishia Tanzania, mangapi ni changamoto.

Naona kuna watu wengi wanasoma vitabu vya "Self Help" vilivyolengwa kwa Wamarekani au watu wa Ulaya, halafu wanataka kucopy moja kwa moja Tanzania. Wanakutana na changamito kubwa sana ya kujua yapi unawe,a kuyahamisha na yapi huwezi.
 
Back
Top Bottom