Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,169
- 48,451
Hii nukuu ya kunionya mimi toka kwa huyu Mwana JF mwenzetu imenishagaza sana. Imenishangaza kwa kuwa inaonesha kwenye nchi hii kuwa na mawazo tofauti na CCM ni jambo la hatari sana.Halafu ' mkidudeliwa ' na ' kunyalandaliwa ' na ' wanaojulikana ' mnakimbilia ' Kulialia ' na kuomba misaada ili mponyeke.
Lakini mawazo kama ya huyu mwana JF mwenzetu yako kwa watanzania wengi sana kiasi kwamba yanaleta swali la msingi ni kwa nini watanzania wanahofia kitakachowapata baada ya kuipinga CCM?
Mitaani inasemwa ukiipinga CCM kwenye nyumba yako kunaweza kupitishwa Barabara na nyumba yako kubomolewa, wafanyakazi wa Umma inadaiwa watafukuzwa kazi, kwa wanafunzi wa vyuo wanaambiwa watanyimwa mikopo, kwa wanasiasa wanaambiwa kitawapata kama kilichompata Lissu na mengi mengi sana.
Lakini CCM yenyewe inajinasibu kama ni chama kinacholinda amani na kupenda amani kwa watanzania. Kama CCM ni chama cha kupenda na kulinda amani ni kwa nini watanzania wenzao wanakiona kuwa kinaweza kuwapatliza kama wakipingana nacho?