Kwanini wapinzani hawatoi shukrani kwa Rais Kikwete?

Ng'wamapalala

JF-Expert Member
Jun 9, 2011
6,808
6,500
Mmarekani aitwaye Max de Pree aliwahi kusema, ‘’The first responsibility of a leader is to define reality. The last is to say thank you’’.

Wapinzani nchini Tanzania wamekosa fadhira kwa Rais Kikwete pamoja na kuwasaidia sana katika ukuaji wao kisiasa!

Rais Kikwete baada ya kuingia madarakani na kukuta hali ni mbaya kwa upande wa wapinzani, hakusita kumteua Ismail Jussa wa chama cha wananchi CUF kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuupa upinzani angalau uhai wa kisiasa.

Ikumbukwe kuwa, wakati Rais Kikwete anaingia madarakani mwaka 2005, Kati ya viti 182 vya Ubunge Tanzania Bara, CCM walishinda viti 175. CHADEMA walipata viti 5, TLP 1 na UDP 1 huku CUF na NCCR-Mageuzi wakiwa hawana hata mbunge mmoja. Kwa lugha nyingine, upinzani bungeni ulikuwa ni kama kutafuta sindano kwenye mchanga wa baharini.

Ni katika utawala wa Rais Kikwete ambapo upinzani umeshika kasi mpaka unahatarisha maisha ya chama kikongwe barani Africa kinachoitwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wakati wa utawala wa Rais Mkapa, upinzani kwa Tanzania Bara ulikuwa unakufa kila chaguzi kama siyo kila siku. Wakati akiingia madarakani mwaka 1995, Jumla ya kura za wapinzani kwa upande wa ubunge zilikuwa asilimia 41, mwaka 2000 zikapungua na kuwa asilimia 35 na mwaka 2005 zilipungua zaidi na kuwa asilimia 29.

Mwaka 1995, Viti vya upinzani katika Bunge la Jamhuri vinavyotokana na majimbo ya uchaguzi vilikuwa 46 kati ya viti 232, mwaka 2000 vilipungua na kuwa viti 29 kati ya viti 232, na haikuishia hapo, mwaka 2005 vikapungua zaidi na kuwa viti 26 kati ya viti 232.

Kwa upande wa Tanzania bara peke yake, mwaka 1995 wapinzani walipata viti vya ubunge 22 kati ya viti 182, na mwaka 2000 walijikuta wakipata viti 14 kati ya viti 182. Hali ilikuwa mbaya zaidi mwaka 2005 ambapo walipata viti 7 kati ya viti 182.


Utendaji wa Rais Kikwete unavifagilia kwa umakini vyama vya upinzani njia ya kuelekea Ikulu bila ya vyama hivyo kuwa na input inayoeleweka achilia mbali kuonekana kama vina nia madhubuti ya kushinda chaguzi za udiwani, ubunge na Urais.

Utendaji wa Rais Kikwete unamfanya awe ni mpinzani ndani ya CCM kutokana na matokeo ya utendaji wake ndiyo maana kuna baadhi ya wanachama wa CCM walishtuka mapema baada ya kung'amua na kutaka kutenganisha kofia ya Mwenyekiti na Rais wa Tanzania.

Kutokana na utendaji wa Rais Kikwete na serikali yake, Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010 uliwaleta bungeni CHADEMA wakiwa na wabunge 48, CUF 36, NCCR-Mageuzi 3, UDP 1 na TLP 1, Hili ni ongezeko kubwa sana kwa kipindi kifupi.

Kama hiyo haikutosha, Rais Kikwete aliwaongezea wapinzani mbunge mwingine mmoja (James Mbatia) ili wapambane vizuri na CCM!

Kwa sasa wapinzani wako kimya wanasubiri fadhira nyingine ya Rais Kikwete itakayotokana na kumteua mgombea wa Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM 2015 ambaye hachaguliki ili ahakikishe kazi iliyomleta Ikulu anaimaliza!

Rais Kikwete is on 'mission’ and he is close to pulling it off!

Wahenga walisema, the gratitude of a donkey is kicks.

Wapinzani toeni angalau shukrani kwa Rais Kikwete!
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Ametusaidia sana kikwete katika harakati zetu za kuwatafutia neema watanzania!
 
Nimeipenda hii mada! Na itakua vizuri zaidi rais ahakikishe ccm haipati mgombea urais mwaka huu maana hali ni mbaya sana kwao!
 
rais kikwete alipaswa kushukuriwa na wapinzani kwa kutuleteakatiba mpya. bahati mbaya ametuacha njia panda....

sio katiba tu,naona asilimia kubwa wapinzani wameiendesha serikali sana sema wingi na udikteta wa c.c.m kwa kauli walizokaririshwa za 'ndiyo na hapana' zimewapa uhai mfu,hivo ni jukumu la wote kushikana mkono wa shukrani kwani uhai wa upande mmoja hutegemea uwepo wa upande mwingine
 
Anaweza akaongeza msaada mkubwa zaidi kwa maana hakukutana barabarani na El,na ukizingatia kauli ya EL nini nilichofamys ambushed mwenyekiti(jk) hujui
 
Sijawahi kuona upuuzi kama huu uliyoletwa hapa. Yeye ni Nani mpaka upinzani ukue au ufe? MUNGU PEKEE KWA MUJIBU WA MAANDIKO NDIYE ANAYESTAHILI KUSHUKURIWA NA SI VINGINEVYO.
 
Kikwete si mtu wa kupewa shukrani bali lawama tu mpaka ajiue. Atapata shukrani only akiwafunga Mkapa, Daniel Yona, Mama Makinda, na majambazi wengine wa CCM.
 
Kikwete ni rais niliyetokea kumkubali sana TZ kwa uongozi wake hakika kazi mzuri aliyoifanya imeonekana tuliofundwa na wazazi wetu tunamshukuru ila kwa wale wasiojielewa endeleeni kumtukana ila neema huijui mpaka ikutoke. Mungu akupe maisha marefu na yenye afya ameen
 
mleta mada we ni mnafiki na mzandiki na mchawi unaeishi,umetoa takwimu za miaka na asilimia ya kura za upinzani ulipofika 2010 umeacha hujasema,so kikwete alipigia kampeni upinzani
 
Naona unacho unachokifahamu dhifi ya Rais Jakaya Kikwete, sisi wengine hatukijui.
 
Pamoja na kwamba udhaifu wa kiongozi unaweza ukachangia kuupaisha upinzani nadhani watanzania wameamuwa kufanya mabadiliko baada ya kuchoshwa na CCM.

Kwani kuna baadhi ya maaeneo CCM wamefanya mambo mazuri tu,ya kimaendeleo lakini pamoja na hayo,CCM bado wamekataliwa bila kujali mambo mazuri walioyafanya.


Kwani wakati mwingine hata kitu kizuri kinachowafanyia wananchi mambo mazuri huwa kinachokwa na wananchi,hivyo hufika wakati ambao wananchi huamuwa kufanya mabadiliko bila kujali mazuri yaliyofanywa na kile kilichopo madarakani kwa wakati huo.

Kinachotakiwa ni kuwa na kiasi,si kwamba eti kwa vile chama fulani kimeongoza vizuri,kimewafanyia wananchi mazuri kwa kushirikina na kiongozi aliyeko madarakani kwa wakati huo basi ndio kiendelee kukaa madarakani milele na milele wakati ni kipindi cha demokrasia,basi huo utakuwa ni utawala wa kifalme ambao ili kumuondoa kiongozi aliyeko madarakani wananchi wanatakiwa wafanye kama kile walichomfanya Gaddaf.
 
Mmarekani aitwaye Max de Pree aliwahi kusema, ‘’The first responsibility of a leader is to define reality. The last is to say thank you’’.

Wapinzani nchini Tanzania wamekosa fadhira kwa Rais Kikwete pamoja na kuwasaidia sana katika ukuaji wao kisiasa!

Rais Kikwete baada ya kuingia madarakani na kukuta hali ni mbaya kwa upande wa wapinzani, hakusita kumteua Ismail Jussa wa chama cha wananchi CUF kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuupa upinzani angalau uhai wa kisiasa.

Ikumbukwe kuwa, wakati Rais Kikwete anaingia madarakani mwaka 2005, Kati ya viti 182 vya Ubunge Tanzania Bara, CCM walishinda viti 175. CHADEMA walipata viti 5, TLP 1 na UDP 1 huku CUF na NCCR-Mageuzi wakiwa hawana hata mbunge mmoja. Kwa lugha nyingine, upinzani bungeni ulikuwa ni kama kutafuta sindano kwenye mchanga wa baharini.

Ni katika utawala wa Rais Kikwete ambapo upinzani umeshika kasi mpaka unahatarisha maisha ya chama kikongwe barani Africa kinachoitwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wakati wa utawala wa Rais Mkapa, upinzani kwa Tanzania Bara ulikuwa unakufa kila chaguzi kama siyo kila siku. Wakati akiingia madarakani mwaka 1995, Jumla ya kura za wapinzani kwa upande wa ubunge zilikuwa asilimia 41, mwaka 2000 zikapungua na kuwa asilimia 35 na mwaka 2005 zilipungua zaidi na kuwa asilimia 29.

Mwaka 1995, Viti vya upinzani katika Bunge la Jamhuri vinavyotokana na majimbo ya uchaguzi vilikuwa 46 kati ya viti 232, mwaka 2000 vilipungua na kuwa viti 29 kati ya viti 232, na haikuishia hapo, mwaka 2005 vikapungua zaidi na kuwa viti 26 kati ya viti 232.

Kwa upande wa Tanzania bara peke yake, mwaka 1995 wapinzani walipata viti vya ubunge 22 kati ya viti 182, na mwaka 2000 walijikuta wakipata viti 14 kati ya viti 182. Hali ilikuwa mbaya zaidi mwaka 2005 ambapo walipata viti 7 kati ya viti 182.


Utendaji wa Rais Kikwete unavifagilia kwa umakini vyama vya upinzani njia ya kuelekea Ikulu bila ya vyama hivyo kuwa na input inayoeleweka achilia mbali kuonekana kama vina nia madhubuti ya kushinda chaguzi za udiwani, ubunge na Urais.

Utendaji wa Rais Kikwete unamfanya awe ni mpinzani ndani ya CCM kutokana na matokeo ya utendaji wake ndiyo maana kuna baadhi ya wanachama wa CCM walishtuka mapema baada ya kung'amua na kutaka kutenganisha kofia ya Mwenyekiti na Rais wa Tanzania.

Kutokana na utendaji wa Rais Kikwete na serikali yake, Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010 uliwaleta bungeni CHADEMA wakiwa na wabunge 48, CUF 36, NCCR-Mageuzi 3, UDP 1 na TLP 1, Hili ni ongezeko kubwa sana kwa kipindi kifupi.

Kama hiyo haikutosha, Rais Kikwete aliwaongezea wapinzani mbunge mwingine mmoja (James Mbatia) ili wapambane vizuri na CCM!

Kwa sasa wapinzani wako kimya wanasubiri fadhira nyingine ya Rais Kikwete itakayotokana na kumteua mgombea wa Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM 2015 ambaye hachaguliki ili ahakikishe kazi iliyomleta Ikulu anaimaliza!

Rais Kikwete is on 'mission’ and he is close to pulling it off!

Wahenga walisema, the gratitude of a donkey is kicks.

Wapinzani toeni angalau shukrani kwa Rais Kikwete!

Akili zako zinahitaji kuongezewa mbolea kwani zimedumaa
 
JK kuna mambo mengi tutamkumbuka nayo binafsi nimempenda kwa kuwa karibu na watu,baadhi ya watendaji mmemuangusha
 
kukua kwa upinzani ni kawaida tu!!ukuna kitu kinachokua ghafla.mawazo yako 0000000000..tunakua kwa kasi ata angebana tungejua la kufanya...
 
Hivi ni kweli kwamba, wakati Kikwete akiingia madarakani Cuf na Nccr walikuwa hawana hata Mbunge mmoja?

Akili zako zinakutosha mwenyewe...!!!!

BACK TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom