Kwanini wanawake ndio huonekana kikwazo?

Kwanini wanawake ndio huonekana kikwazo?

A man with one idea

Senior Member
Joined
Jul 18, 2022
Posts
125
Reaction score
269
Habari za leo ndugu zangu! Ningependa mnisadie kwanini Kwenye suala la kutembelea ndugu, hasa wale wenye uwezo wa kifedha.

Mama wa familia ndio huonekana kikwazo cha Mahala pale kutofikika hasa ndugu wale wa upande wa mwanaume( unakuta mtu anakwambia siwezi kabisa kwenda kwa ndugu yule! Ukiuliza kwanini? Anakwambia yule mke wake sio!) Je hili usababishwa na nini?

Ni kweli wanawake wengi huwa kikwazo kwa ndugu wengi kutoka upande wa Baba kutofikika pale kwake!?
 
Naona inategemea familia na familia, wengine ndio, wengine sio...

Japo wanasema wanawake kwa maneno hawajambo...
 
Shida tu ndo zinatupeleka kwa ndugu tuvumilie tu kama kuna ulazima wa kwenda kwa ndugu
 
Habari za leo ndugu zangu! Ningependa mnisadie kwanini Kwenye suala la kutembelea ndugu ,Hasa wale wenye uwezo wa kifedha...
Changamoto za kifamilia daiwa huwa zinatofautiana kati ya familia na familia.

Changamoto nilizonazo mimi, siyo lazima zifanane na za kwako. Kwamba kwanini wanawake huonekana kikwazo, hilo ni suala mtambuka.
 
Ke wote ni sawa kiakili lakini hawafanani kitabia.

Je wajua ni kipi shetani aliongea na Ever/Hawa bustanini Eden kabla ya kumpatia Adam tunda ale?
 
Changamoto za kifamilia daiwa huwa zinatofautiana kati ya familia na familia.

Changamoto nilizonazo mimi, siyo lazima zifanane na za kwako. Kwamba kwanini wanawake huonekana kikwazo, hilo ni suala mtambuka.
Ooh nimekuelewa.lengo langu pia nielewe Zaidi hili swala.
 
Tulieni majumbani mwenu acheni kushika watu uchawi
 
Back
Top Bottom