Kwanini wanawake hawafuti namba za simu

Kwanini wanawake hawafuti namba za simu

Mbishi 4 real

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
640
Reaction score
655
Kwa kawaida tunapokua tumeingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanawake huwaga tunapeana namba zetu zote za simu za mitandao tofauti tofauti ili ikitokea mpenzi wako kakukosa hewani kwenye namba flani basi awe na uwezo wa kukupata kwa namba nyingine ambayo inawezekana isifahamike na watu wengi lakini mpenzi wako hawezi kukosa kukupatia hiyo namba.

Inapotokea mmeachana asilimia kubwa ya wanaume ndio wanaoongoza kwa kufuta namba za wapenzi wao walioamua kuachana nao, mara nyingi huwa tunawaelekeza kabisa wanawake kwamba "futa namba zangu zote za simu" ili tu kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza.

Suala hili limekua tofauti kidogo kwa upande wa wanawake ambapo unaweza kumwambia afute namba zako za simu akakujibu "sawa" lakini asifanye kama vile ambavyo umemtaka afanye.Wanawake walio wengi wana uwezo wa kukariri namba za simu kwa haraka sana kuliko kitu chochote na hata kama akizifuta bado atakua na uwezo wa kukutumia sms na kukupigia pindi anapojiskia kufanya hivyo hata kama ulishamkataza.

Hii inatokana na nini ? je ni upendo wa dhati alionao juu yako hata kama umemuacha au ni ulimbukeni tu wamapenzi ?

Karibuni tuambizane
 
wanawake huwa ni wavumilivu pia hawapendi shari walio wengi ila sie wanaume huwa tuna amua kwa hasira na ubabe mwingi

2yrs nimeachana na mtu siku moja akanitafuta mpaka nikashangaa, ila baada ya hapo nikafuta tena alipo nitafuta nikauliza we nani? naona alichukia mpaka leo ajanicheki japo najua atanicheki tu ni suala la muda.
 
Hadi umewaza hivo yashakutokea sio?

Kazi ndogo sana hiyo mkuu! Unauliza tatizo ni nini? Wakati umejijibu mwenyewe hapo !

Basi mkiachana sajiri namba mpya uone kama atakupata,

Kazi kwisha
 
Kwa kawaida tunapokua tumeingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanawake huwaga tunapeana namba zetu zote za simu za mitandao tofauti tofauti ili ikitokea mpenzi wako kakukosa hewani kwenye namba flani basi awe na uwezo wa kukupata kwa namba nyingine ambayo inawezekana isifahamike na watu wengi lakini mpenzi wako hawezi kukosa kukupatia hiyo namba.

Inapotokea mmeachana asilimia kubwa ya wanaume ndio wanaoongoza kwa kufuta namba za wapenzi wao walioamua kuachana nao, mara nyingi huwa tunawaelekeza kabisa wanawake kwamba "futa namba zangu zote za simu" ili tu kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza.

Suala hili limekua tofauti kidogo kwa upande wa wanawake ambapo unaweza kumwambia afute namba zako za simu akakujibu "sawa" lakini asifanye kama vile ambavyo umemtaka afanye.Wanawake walio wengi wana uwezo wa kukariri namba za simu kwa haraka sana kuliko kitu chochote na hata kama akizifuta bado atakua na uwezo wa kukutumia sms na kukupigia pindi anapojiskia kufanya hivyo hata kama ulishamkataza.

Hii inatokana na nini ? je ni upendo wa dhati alionao juu yako hata kama umemuacha au ni ulimbukeni tu wamapenzi ?

Karibuni tuambizane
Ni kwasababu wanajua ulivyo mdhaifu na anauwezo wa kukufanya urudi kwake ila tu itachukua muda kidogo..
Ndio maana anauwezo wa kukufwata kimitego japo umemuacha na ukalal naye akakutegeshea na mimba
 
Maswala ya kugombn mpk kufkia hatua ya kulazmishana kufta namb ni utoto, haya maisha duara waweza umlazmishe afute siku si siku ukahtaj mawasiliano nae zaid ya awali, hamna kitu sipend kama bifu
 
Inshort kuachana sio bifu.Huwezi jua dunia duara eX wako anaweza kuja kuwa msaada kwako utapoanguka ukakosa wa kukuinua.
 
Mm namba za wapenzi wangu zpo kchwan so ata nkfuta kwa sm haisaidii
 
Mm nafuta namba ya nn kunijazia phonebook angu
 
kuna siku unashika ka kimeo kako unakagua # gani haijaonesha ushirikiano kwa muda basi una zi r.i.p namba za kutosha

naona wanawake hawana huo utaratibu ndo maana wanatutafuta hata baada ya maachano yetu.
 
Wajnga ndo wanabak nazo,asa umeachana nae namba ake ya nn??me na delete kila ktu hta kama kuna pct nazo,nafuta
 
mapenzi sio beef...kunakuachwa,so inatakiwa kukubali hali zote nina x wangu wengi tu ambao tunapiga story na kuongea as friend.kufuta number ni hasira tu zakiume
 
Kwani hua mnaachana kwa vita mkuu??? kabisa eti unamwambia "fuuuuta namba yangu na usinitafute"mapenz ya O level hayo.Kuachana sio ugomv kwamba hamuwezi kusalimiana wala kusemeshana milele
 
Back
Top Bottom