magode
JF-Expert Member
- Oct 2, 2014
- 2,204
- 3,339
Hivi mwanaume mtu mzima wa zaidi ya miaka 45,unatongoza binti mwenye miaka 16,17 au hata 22. Unakuwa umefikiria nini hasa, hivi watoto wa umri huo si watoto wako hao.
Mwanaume mwenzangu unapata wapi ujasiri wa kuvua nguo mbele ya mtoto kama huyo,kuna mzee ana zaidi ya miaka 48 ana msumbua binti anayenisaidia kazi zangu hapa,binti ana miaka 19. Kibaya zaidi huyu binti kazaliwa hapa na huyu mzee akiona.
Binti ameshaleta malalamiko kwangu zaidi ya mara 4 nikalazimika kuongea na yule mzee kirafiki,maana hata me ananizidi umri mzee yule alionyesha kunielewa na kuniomba nimtunzie heshima nami nikamuondoa shaka.
Leo binti kanionyesha message za yule mzee,nimechoka kabisaa,nimekubaliana na mawazo ya binti ya kuzipeleka hizi message kwa mkewe na watoto wake. Au nimekosea wadau.
Mwanaume mwenzangu unapata wapi ujasiri wa kuvua nguo mbele ya mtoto kama huyo,kuna mzee ana zaidi ya miaka 48 ana msumbua binti anayenisaidia kazi zangu hapa,binti ana miaka 19. Kibaya zaidi huyu binti kazaliwa hapa na huyu mzee akiona.
Binti ameshaleta malalamiko kwangu zaidi ya mara 4 nikalazimika kuongea na yule mzee kirafiki,maana hata me ananizidi umri mzee yule alionyesha kunielewa na kuniomba nimtunzie heshima nami nikamuondoa shaka.
Leo binti kanionyesha message za yule mzee,nimechoka kabisaa,nimekubaliana na mawazo ya binti ya kuzipeleka hizi message kwa mkewe na watoto wake. Au nimekosea wadau.