Kwanini wanandoa wa kiafrika sio romantic

Kwanini wanandoa wa kiafrika sio romantic

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,709
Reaction score
9,030
Ndoa nyingi ni kwa ajili tu ya kulala na kuamka, kulea watoto na kuzeeka pamoja mpaka kifo. Wanandoa wengi ni mara chache sana kupeana busu na kukumbatiana wanapopata habari njema. Mume humuwekea mkewe chakula mdomoni pale tu mke anapokuwa mgonjwa akawa hawezi kujilisha.

Ukimuona mwanaume anamfungulia mlango mkewe basi ujue mlango huo ni mbovu au una kasoro. Kitu pekee kinachomfanya mwanaume wa kiafrika kuigusa shingo ya mkewe ni pale mke huyo anapolalamika kuwa ana homa. Hatoigusa tena mpaka atakapopata homa nyingine. Muda pekee ambao atambeba mkewe mikononi mwake ni pale anapojifungua. Ukiwaona wamekaa nje wakati wa usiku, usifikiri wanaenziana. Wanasubiri tu harufu ya dawa waliyopulizia ndani iishe.

Wanawake wengi wanawanunulia zawadi waume zao pale tu mume anapokuwa mgonjwa hospitalini. Muda pekee ambao wanakimbia pamoja ni pale inapotokea hatari na kila mtu akawa anakimbia. Muda pekee wanaokaa pamoja jioni ni pale wanapotaka kwenda kupeleka malalamiko kwa wazazi wa mtu aliyempiga mtoto wao au aliyempa mimba binti yao.

Muda pekee wanaokoga pamoja ni pale wote wanapochelewa kwenda kazini. Muda pekee ambao mke huyatazama kwa ukaribu macho ya mumewe ni pale jicho la mume linapopatwa na uchafu.

Kwa bahati mbaya, Waafrika wana mawazo kuwa kila mwanaume romantic na mbembezi anakuwa ametawaliwa na mke. Hapo wataanza kueneza umbea. Tubadilike.... Mabadiliko yanaanza na WEWE.
 
mkuu mila na tamaduni zetu ndizo ninafanya hiki kitu.

Ila na pesa wakati mwingine ina matter kwa kiasi kikubwa
 
Ndoa nyingi ni kwa ajili tu ya kulala na kuamka, kulea watoto na kuzeeka pamoja mpaka kifo. Wanandoa wengi ni mara chache sana kupeana busu na kukumbatiana wanapopata habari njema. Mume humuwekea mkewe chakula mdomoni pale tu mke anapokuwa mgonjwa akawa hawezi kujilisha.

Ukimuona mwanaume anamfungulia mlango mkewe basi ujue mlango huo ni mbovu au una kasoro. Kitu pekee kinachomfanya mwanaume wa kiafrika kuigusa shingo ya mkewe ni pale mke huyo anapolalamika kuwa ana homa. Hatoigusa tena mpaka atakapopata homa nyingine. Muda pekee ambao atambeba mkewe mikononi mwake ni pale anapojifungua. Ukiwaona wamekaa nje wakati wa usiku, usifikiri wanaenziana. Wanasubiri tu harufu ya dawa waliyopulizia ndani iishe.

Wanawake wengi wanawanunulia zawadi waume zao pale tu mume anapokuwa mgonjwa hospitalini. Muda pekee ambao wanakimbia pamoja ni pale inapotokea hatari na kila mtu akawa anakimbia. Muda pekee wanaokaa pamoja jioni ni pale wanapotaka kwenda kupeleka malalamiko kwa wazazi wa mtu aliyempiga mtoto wao au aliyempa mimba binti yao.

Muda pekee wanaokoga pamoja ni pale wote wanapochelewa kwenda kazini. Muda pekee ambao mke huyatazama kwa ukaribu macho ya mumewe ni pale jicho la mume linapopatwa na uchafu.

Kwa bahati mbaya, Waafrika wana mawazo kuwa kila mwanaume romantic na mbembezi anakuwa ametawaliwa na mke. Hapo wataanza kueneza umbea. Tubadilike.... Mabadiliko yanaanza na WEWE.
wacha umagharibi mamboleo!
 
Hii ni kweli mkuu tunaishi kwa mazoea hata kukumbatiana usiku ni shida,sasa ndoa itakuwa na furaha kweli?Njia pekee ya kutatua changamoto za maisha na kupata maendeleo ni kuwa na furaha katika ndoa na sio kuishi kama dada na kaka.
 
Aya yote yanakuja kulingana na kipato cha familia nyingi kuwa chini , na wakati mwingine mmoja kati yao anahisi huyu nishaweka ndani so hata ile nguvu ya ushawishi au care inakuwa ndogo maana anajua hawezi kwenda mahali yoyote pale, tofauti na mchepuko wake wa nje ambao anajitahidi kuujenga kuwa karbu nae
[HASHTAG]#mtazamo[/HASHTAG]
 
Hahaaa. Mbali na yote hayo bado zinadumu na maisha yanaendelea.

Ni ukweli tu kwamba tangia mwanzo wa mahusiano hakuwagi na hivyo vitu kama vipo ni vichache kati ya hivyo na hiyo ndio sababu hivyo inapofika ndani ya ndoa ndio vinakufa kabisa.
 
Ndoa nyingi ni kwa ajili tu ya kulala na kuamka, kulea watoto na kuzeeka pamoja mpaka kifo. Wanandoa wengi ni mara chache sana kupeana busu na kukumbatiana wanapopata habari njema. Mume humuwekea mkewe chakula mdomoni pale tu mke anapokuwa mgonjwa akawa hawezi kujilisha.

Ukimuona mwanaume anamfungulia mlango mkewe basi ujue mlango huo ni mbovu au una kasoro. Kitu pekee kinachomfanya mwanaume wa kiafrika kuigusa shingo ya mkewe ni pale mke huyo anapolalamika kuwa ana homa. Hatoigusa tena mpaka atakapopata homa nyingine. Muda pekee ambao atambeba mkewe mikononi mwake ni pale anapojifungua. Ukiwaona wamekaa nje wakati wa usiku, usifikiri wanaenziana. Wanasubiri tu harufu ya dawa waliyopulizia ndani iishe.

Wanawake wengi wanawanunulia zawadi waume zao pale tu mume anapokuwa mgonjwa hospitalini. Muda pekee ambao wanakimbia pamoja ni pale inapotokea hatari na kila mtu akawa anakimbia. Muda pekee wanaokaa pamoja jioni ni pale wanapotaka kwenda kupeleka malalamiko kwa wazazi wa mtu aliyempiga mtoto wao au aliyempa mimba binti yao.

Muda pekee wanaokoga pamoja ni pale wote wanapochelewa kwenda kazini. Muda pekee ambao mke huyatazama kwa ukaribu macho ya mumewe ni pale jicho la mume linapopatwa na uchafu.

Kwa bahati mbaya, Waafrika wana mawazo kuwa kila mwanaume romantic na mbembezi anakuwa ametawaliwa na mke. Hapo wataanza kueneza umbea. Tubadilike.... Mabadiliko yanaanza na WEWE.
Hahahahahah....kuna familia nyingine namna wanavyoishi utafikiri ni KANDA MAALUM
 
Hahaaa. Mbali na yote hayo bado zinadumu na maisha yanaendelea.

Ni ukweli tu kwamba tangia mwanzo wa mahusiano hakuwagi na hivyo vitu kama vipo ni vichache kati ya hivyo na hiyo ndio sababu hivyo wanapofika ndani ya ndoa ndio vinakufa kabisa.
hao wazungu wanayafanya yote hayo na bdo wanaachana sana kuliko huku
 
Ndoa nyingi ni kwa ajili tu ya kulala na kuamka, kulea watoto na kuzeeka pamoja mpaka kifo. Wanandoa wengi ni mara chache sana kupeana busu na kukumbatiana wanapopata habari njema. Mume humuwekea mkewe chakula mdomoni pale tu mke anapokuwa mgonjwa akawa hawezi kujilisha.

Ukimuona mwanaume anamfungulia mlango mkewe basi ujue mlango huo ni mbovu au una kasoro. Kitu pekee kinachomfanya mwanaume wa kiafrika kuigusa shingo ya mkewe ni pale mke huyo anapolalamika kuwa ana homa. Hatoigusa tena mpaka atakapopata homa nyingine. Muda pekee ambao atambeba mkewe mikononi mwake ni pale anapojifungua. Ukiwaona wamekaa nje wakati wa usiku, usifikiri wanaenziana. Wanasubiri tu harufu ya dawa waliyopulizia ndani iishe.

Wanawake wengi wanawanunulia zawadi waume zao pale tu mume anapokuwa mgonjwa hospitalini. Muda pekee ambao wanakimbia pamoja ni pale inapotokea hatari na kila mtu akawa anakimbia. Muda pekee wanaokaa pamoja jioni ni pale wanapotaka kwenda kupeleka malalamiko kwa wazazi wa mtu aliyempiga mtoto wao au aliyempa mimba binti yao.

Muda pekee wanaokoga pamoja ni pale wote wanapochelewa kwenda kazini. Muda pekee ambao mke huyatazama kwa ukaribu macho ya mumewe ni pale jicho la mume linapopatwa na uchafu.

Kwa bahati mbaya, Waafrika wana mawazo kuwa kila mwanaume romantic na mbembezi anakuwa ametawaliwa na mke. Hapo wataanza kueneza umbea. Tubadilike.... Mabadiliko yanaanza na WEWE.
Je wewe upo romanti? Isije ukawa unafanya tathimini ya vitu ambavyo hata wewe mwenye unaweza kujijibu kwa sababu wewe ni wa style hiyo.
 
Back
Top Bottom