viongozi wa serikali ya ccm wasanii, isssue ya wachina ni kwa sababu wananchi walala hoi wamelalamika kule sokoni kariakoo, tatizo la wageni wanaongia isivyo halali ni kubwa sana kuliko mnavyodhani, hapa tuna makundi ya wahindi, waarabu, wakenya, wasomali, wazungu wa kutoka east europe nk. mbaya wengi wao kutokana na mitandao ya rushwa wameendelea kuwepo hapa nchini kwa muda mrefu tu, wakifanya kazi na biashara ambazo watanzania wanauwezo wa kuzifanya, mfano wakenya wanajipanga kwenye baadhi ya makampuni na kujihakikishia uwepo wao kwa muda mrefu wakishirikiana na immigration na taasisi zingine zinazotoa approval za wao kupata vibali....utaratibu ni kwamba wageni wanatakiwa wawe na utaalamu maalumu ndiyo wapewe hizo nafasi nia ikiwa ku impart kmowledge kwa locals baada ya muda wao kuisha wawaachie, lakini inakuwa sivyo, atatafuta kila sababu hata kumvictimise yule local ili aonekane kwamba hafai....wengine kazi yao kuhamaham....hii imeshindikana kwa sababu hao wageni wakija cha kwanza ni kupata political connection for protection....unajuwa viongozi wetu wengi ni wapenda rushwa.....naomba tuendeleze mjadala huu kwa umakini na kina