Kwanini wabunge wa CCM wanahariri michango ya wenzao kuliko kuchangia bajeti?

Magobe T

JF-Expert Member
Mar 19, 2008
4,621
2,567
Ndugu wanaJF, nimekuwa nikifuatilia bunge kwa karibu sana na nimeweza kubaini haya.

1. Wabunge wa CCM wanawaonea wivu wabunge wanaoikosoa bajeti ya serikali na hviyo kwa vile wao wanaogopa kufanya hivyo, wanaonesha kukerwa na michango inayoikosoa bajeti ya serikali ili iboreshwe vizuri zaidi.

2. Wabunge wa CCM wanageuka wasemaji wa serikali kuliko kuisadia serikali iwajibike na kuwatumikia wananchi vizuri zaidi.

3. Wanaunga mkono hoja asilimia 100 hata kama ina kasoro za msingi. Kwa vile wabunge wa CCM ni wengi zaidi na kwa vile iwe na kasoro au isiwe nazo, bejeti itapita tu. Ni mara chache sana wanaweza kusababisha bajeti ifanyiwe marekebisho na kuboreshwa.

4. Kama serikali imeleta bajeti bungeni ili ijadiliwe - kujadili maana yake ni kusema yale mazuri na mabaya na kupendekeza namna ya kuiboresha.

5. Badala ya wabunge wa CCM kuchangia bajeti wao wanapoteza muda wao mwingi kuanza kukosoa na kuhariri michango ya wabunge wasio wa CCM. Je, ni kweli wanajua maana ya kujadili?
 
Wana jipya basi???, hadi tuongee ndo watafute point kwetu, sio wabunge tu,bali serikali yao pia!
 
hiyo inaonyesha kuwa huwa hawasomi na kuchambua makarabrasha wanayopewa kabla ya kuingia bungeni .wao kazi yao ni kusikiliza mbunge wa cdm kasema nini ili wapate points za kuzungumza.
 
Ukweli unauma lazima wafanye hivyo ili kuona kama wanaweza kupunguza makali na asila za wananchi walizonazo kwani bila kufanya hivyo 2015 hawana nafasi.
 
​kwa sababu si wabunge wa wananchi wameingia bungeni kwa kununua kura
 
Kila mtu anaona jinsi wabunge hasa wa CCM wanavochangia maoni ya kambi ya upinzani zaid kuliko bajeti ya wizara. Mwisho wa siku si maoni ya Upinzani yanafuatwa wala marekebisho ya bajeti ya serikali.

Jambo lingine la wazi ni jinsi mawaziri wa zamani na wapya wanavoshindwa kuwawakilisha wapiga kura wao. Mustafa Mkulo, Andrew Chenge, Wasira, Lowasa, Nagu, Ngeleja, na wengine wengi hawazungumzi kabisa kuhusu majimbo yao. Michango yao ni kuelekea tu Kambi ya Upinzani imesema nn!!

Ndio maana, ili tuwasikie na kuwakilishwa ni lazima Waziri, Naibu wawe nje ya mfumo wa kuchaguliwa. Hawa waombe kazi katika wizara hizo na wabunge wote wawe na uhuru na namna ya kuwahoji.
 
Naishauri kambi ya upinzani kwa pamoja ikubaliane majadiliano ya wizara moja wasichangie kabisa na sisi wananchi tufahamishwe kuwa hiyo budget wameachiwa CCM waichambue wao kisha wananchi wataelewa nini kinaendelea bungeni
 
CCM has lost leadership. Every one is trying to show capabilities to lead by being against every thing from opposition. This stupid attitude has paid divident to Nyalandu and Simbachawene. They were every where like they were elected to protect the government. It this hypocritical behavior which is prevalent as you have correctly observed
 
CCM has lost leadership. Every one is trying to show capabilities to lead by being against every thing from opposition. This stupid attitude has paid divident to Nyalandu and Simbachawene. They were every where like they were elected to protect the government. It this hypocritical behavior which is prevalent as you have correctly observed
 
Back
Top Bottom