kwanini usalitii

kwanini usalitii

dodoso33

Member
Joined
Oct 9, 2012
Posts
38
Reaction score
11
Sijawahi kuona popote pale mtu afike
ngazi ya kuwa CEO halafu ghafla aseme
amechoka uboss, anataka kuwa
Messenger...Sijawahi...Nakushangaa
wewe kijana, Mungu amekupa
mwanamke mzuri tu,ana kila kitu,anakupenda,watu wanamtolea
macho hawampati,ila wewe unaenda
unacheat na Kinyamkera cha
ajabu,kifurugobe hakina hata
shape,kimekomaa kama goti la mbuzi,
unakosa nini kwa mpenzi wako?Hata ukifumaniwa unak
osa pozi kujibu ulifuata nini...Na wewe
mwanamke, unapewa kila kitu na
mwanaume wako,he is handsome,very
caring,ya nini kumgeuza Soko la Hisa
kuuzia wengine Share zake, halafu vijitu unavyocheat navyo ni vifutu tu havina
hatadili...Kama mpenzi hajui shughuli na
kusimamia kucha, mwambie, mfundishe,
na sio kujiiba na Vifuu tundu,
ukikamatwa unasema Shetani
amekupitia, Huyo Shetani hana kazi aje kukupitia wewe tu peke yako...Respect
your partners,ukimchoka sema sio
unacheat na watu hawaeleweki wana
Shape ya Nazi au Kibatari!!!!!
 
wacha uongo, ina maana wewe hujawahi kuchepuka out?
 
history will never end i dont want know kabisaaa .shetani anageuzaga watu macho nakuwashikia mguu??

Shetani anacheza na mawazo yako na hisia zako, kama huna Roho wa Mungu you are trapped my dear.

Nikuulize, hivi wewe hauna kitu ambacho unakifanya japo ni kibaya? tunaweza ita tabia mbaya; na unajaribu kuiacha unashindwa? Ni kazi ya shetani. Ila ukiiruhusu roho ya Mungu, unaweza mshinda shetani. So role yako, nikuchagua kumtegemea Mungu.
 
dawa ni kumjua MUNGU,af mtoa mada mbona huyo hawara umedhalilisha sana hakuna binadamu mkalifu ndugu yangu.kwko anaweza kuwa lulu kwangu akawa fedha upo hapo
 
mtoa mada nae ni 'wale wale!',hv kwanini tunabaki kufanya artistic descripition ya mapenzi badala ya kufanya analysis za kina,filosofikali?ndio tunapofeli.ni hilo tu,kwa sasa!
 
hivi hili ni shairi au ujumbe,,, maaana umeongea kwa ujuzi fulani ambao sijauelewa vizuri
ila ol in ol,, message delivered
 
ndugu uhandsome kunipa kila kitu hakuna uhusiano na kucheat sometime small things like attention , lugha mbaya kila saa csikilizwi, naamrishwa tu hata kama kanipa atm kadi yake ntamcheat tu
 
Tatizo nahisi kuna kautamu ka ziada kalifichwa kule kunako mvunguni..............
 
bupa tamu nyie acheni....alafu tatizo ni kwamba wote wanawake na wanaume wanapenda game....
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa!! Saurce ....bible!!
Hiki ni kizazi cha nyoka.
 
Kumsingizia shetani ni kuondoa responsibility ya matendo yako. mtu akikufanyia Jambo baya akakuambia ni shetani utamsamehe mara ngapi? Utawezaje kujua ni shetani? Personally nafikiri mambo ya kucheat haitokei ghafla. Unatamani, una plan , unajificha na kufanya mambo yako kisirisiri ukijua unatenda Jambo baya. Ina maana unajua unachokifanya ni kitendo kibaya ndio maana unajificha. hakuna cha mdudu anaeitwa shetani Kama mungu amekuumba ukiwa na akili na maarifa. Hauhitaji roho spesho toka kwake. Kama kuna tatizo kwenye ndoa ongea na mwenzako, suluhisha, ikishindikana move on.


Shetani anacheza na mawazo yako na hisia zako, kama huna Roho wa Mungu you are trapped my dear.

Nikuulize, hivi wewe hauna kitu ambacho unakifanya japo ni kibaya? tunaweza ita tabia mbaya; na unajaribu kuiacha unashindwa? Ni kazi ya shetani. Ila ukiiruhusu roho ya Mungu, unaweza mshinda shetani. So role yako, nikuchagua kumtegemea Mungu.
 
Shetani anacheza na mawazo yako na hisia zako, kama huna Roho wa Mungu you are trapped my dear.

Nikuulize, hivi wewe hauna kitu ambacho unakifanya japo ni kibaya? tunaweza ita tabia mbaya; na unajaribu kuiacha unashindwa? Ni kazi ya shetani. Ila ukiiruhusu roho ya Mungu, unaweza mshinda shetani. So role yako, nikuchagua kumtegemea Mungu.
hahahahah aise nachokaga sana na hizi ngonjera za dini i dont believe in any supernatural power claimed to exists Kaunga
 
Last edited by a moderator:
hata chakula huwa kinapikwa nyumbani lakini cha hotel ama mghahawa huwa kinakuwa kitamu kwa sababu ya manjonjo
 
Back
Top Bottom