Kwanini unaishi Dar es salaam?

Kwanini unaishi Dar es salaam?

Dar ni sehemu yenye raha nyingi kama kulivyo na karaha nyingi pia. Japo kwangu nikipima naona karaha ndio zimezidi.

Ni kawaida sana kukuta misururu ya foleni ya watu wakigombea usafiri tena unakuta ni mida mibovu kabisa. watu wanalundikwa kwenye daladala na mwendokasi utadhani ni bidhaa. hata km una usafiri binafsi foleni ni kila kona.

Ukitaka kuwahi sehemu ili uwahi asbh kwa mfano hospitali bac hakikisha unaamka mapema sana tena ikiwezekana saa nane uko au tisa usiku.

Hali ya usafi mitaani mitaa michafu, vyoo vya paspoti na kuwekwa mapipa chini, , mapusha na wateja wao wa madawa ya kulevya, wadangaji, chemba zilizowazi zinazochangia hewa chafu ni changamoto na kero zingine lundo. Licha ya haya yote kuna mtu humtoi nje Dar!

Sasa ndugu yangu wew nini hasa kinachokufanya ung'ang'anie kuishi mahali yenye karaha hivyo.

Mnaongangania kuishi huko niwajulishe tu nje ya Dar kuna maisha pia. Tena maisha ya stress kabisa na kila kitu kinaenda sawa.
Kwa nini mkuu unapimia ubovu wa Dar kwenye mitaa ya walalahoi? Sasa wewe mkuu ukaishi Tandale Kwa Mtogole halafu useme Dar yote mbovu? In short Dar ni kila kitu ni wewe tu na roho yako! Kila unakoangalia ni fursa tu!
 
Dar ni sehemu yenye raha nyingi kama kulivyo na karaha nyingi pia. Japo kwangu nikipima naona karaha ndio zimezidi.

Ni kawaida sana kukuta misururu ya foleni ya watu wakigombea usafiri tena unakuta ni mida mibovu kabisa. watu wanalundikwa kwenye daladala na mwendokasi utadhani ni bidhaa. hata km una usafiri binafsi foleni ni kila kona.

Ukitaka kuwahi sehemu ili uwahi asbh kwa mfano hospitali bac hakikisha unaamka mapema sana tena ikiwezekana saa nane uko au tisa usiku.

Hali ya usafi mitaani mitaa michafu, vyoo vya paspoti na kuwekwa mapipa chini, , mapusha na wateja wao wa madawa ya kulevya, wadangaji, chemba zilizowazi zinazochangia hewa chafu ni changamoto na kero zingine lundo. Licha ya haya yote kuna mtu humtoi nje Dar!

Sasa ndugu yangu wew nini hasa kinachokufanya ung'ang'anie kuishi mahali yenye karaha hivyo.

Mnaongangania kuishi huko niwajulishe tu nje ya Dar kuna maisha pia. Tena maisha ya stress kabisa na kila kitu kinaenda sawa.
Braza Kende utakuwa umejichanganya mahali! Kwani nwenyeji wako anaishi wapi? Na ana kazi gani hapa mjini?
 
Mkuu, akili zangu siku zote ziko juu na mtu mbumbumbu lazima atajichanganya tu kuongea nami because I am that special
Sawa, kumbe akili zako ziko juu, thats y am telling u next time make sure unatumia akil zilizoko kichwani, achana na hizo zilizoko juu
 
mtu anaishi chanika sijui mvuti ndanindani uko ila naye utamskia "unajua mi naishi Daa"
Chanika au Mvuti ni sehemu ziko Tunduma mkuu? Si ziko Dar sasa kwanini asiseme anaishi Dar au Dar imejengwa na mitaa na territories kutoka visiwa vya Madagascar..!!
 
Back
Top Bottom