Kwanini Unaamini Mungu yupo?

Mungu yupo kwasababu hata shetani yupo angalia maovu na unyama unaofanyika kutokana na nguvu za giza then nguvu ya nuru ipo action and reaction are opposite but equal to each other
 
Kwanini unaamin uwepo wa upepo umeshawahi kuuona??
Kwanini unaamini uwepo wa kujaa na kupwaa kwa maji ya bahari
Kwnn unaamin kua ipo siku utafufuka na ulipwe kwa ulilolitenda duniani?? Nani atakuhukumu kama sio mungu??
Swali la kwanza na la pili ni relevant... la tatu na la nne yamebase kwenye kuamini hoja ambayo ndip ipo kwenye post hii.

Swali lako la kwanza na la pili... majibu yake yanafall kwenye five senses (mfano oxygen haionekani ila inaweza kuwa tested same as carbondioxide etc)
Ili uweze kujua existence ya kitu lazima uhusishe milango yako mitano ya fahamu i. kunusa sharti kuwe na harufu kama vile kuoza kwa mzoga, kuungua kwa chakula n,k,
ii. kuona hapa sharti kuwe na physical object,
Iii.Kusikia hapa sharti kuwe na sauti, mlio, muungurumo, kuvuma n.k
Iv. Ladha, hapa sharti kuwe na kitu chenye utamu,uchungu,uchachu n.k
V. Kuhisi ili ni jukumu la ngozi yako..hii inatokea pale unapoguswa, unapopulizwa n.k.
ili umthibitishie mtu kwamba hewa ya oxygen ipo sharti ulete matokeo yake base on five senses.... kinyume cha hapo hiyo itakuwa ni ramli... mfano kuna watu wanashindwa kuvuta hewa na hivyo kulazimika kutumia oxyegen machine, hapa ndipo unapoona matumizi yake.....
 
Mwanadamu amtumikie na viumbe vingine ili iweje???
 
Kwahiyo Mungu ni kipi hapo? Ni mim? Ni hivyo vitu vinavyoota?? Mifano yako ni indirect kwanin usimthibitishe yeye kama yeye... hivi si mnadai huwa mnaongea nae kwenye sala.. ni kwanin amumuulizi haya maswali ili mje mtupe majibu sahihi na yasiyotofautiana.
Kwanin hamumuulizi kwamba yesu ni mwanae au ndio mungu mwenyewe???
 
Ushasema hakuna mwenye uwezo huo alafu unasema ni Mungu pekee...
 
Mungu ameandika mimi nipo ambae nipo.
Biblia inasema Mungu ni roho.

Wewe unaangalia ndege , wanyama, wadudu unasema Mungu hayupo?

Labda nikuulize ulimwengu huu umetokeaje?
Kuna kosa ukisema haujui.... mpaka tufanye assumptions? kwani kuna tofauti gani na yale tusiyoyajua ambayo we dont real care.....
 
Naomba nikuulize, kama unaamini hayupo, je ukimkuta yupo utachukua uamuzi gani au utajisikiaje?
Nitapata hasira sana... kwani hakujidhihirisha na hivyo sikujua anataka nini???
Je anataka nifanyd yale yanahubiriwa na organizing religions.... je anataka nimsalie kila siku swala 5 au kila jumapili au jumamosi????
Kuamini hayupo sio kosa kwa vile reasoning ni sifa ya binadamu....hauwezi kuitenganisha nae)
 
Wewe kwanini uamini kuwa Mungu hayupo?

Kwako dini ni nini?

Kuna uhusiano gani kati ya dini na Mungu unaye amini kuwa hayupo?

Imani tulizodumisha ni zipi? Imani ni nini?

Tuanzie hapo.
Unafikir nani anaweza kukujibu kama wewe haukujibu yalioulizwa??
 
Kwa vile na wao wamekubali kwamba ni bora uamini lakini usimkute.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
SOMA
Ushauri Bora.

Unapoenda dukani kununua kitu chochote lazima uulize manual ya bidhaa hiyo ili ujue imetengenezwaje, inatumikaje, inatunzwaje nk.
Hata unapoenda kinunua mbegu ya mmea, kama una ka busara kidogo ni lazima uulizie manual ya hiyo mbegu ili uiamini na kuinunua.

Swali kwa nyie wenye busara

Je umewahi kuiulizia manual yako wewe binafsi ?

Kama hujawahi je zile bidhaa za dukani ni bora kupita wewe ?

Kama sivyo basi wewe utakuwa ni (ashakum sio matusi) mpumbavu sana, kwani unaulizia manual ya redio kaseti na unadharau kuulizia manual yako.

Ewe mwenye busara
Umeshawahi kuiona manual yako ?

Kama hujawahi nakuomba chonde chote anza kuitafuta nina uhakika utaipata, kama manual ya kiberiti inapatikana basi na yako ipo.

Ewe mwenye busara,
Itafute kwanza manual yako inayokuelezea wewe umetengenezwa na kampuni gani, umetengenezwaje (umbo lako), unadumu miaka mingapi, unahalibiwa na nini, unatumikaje nk.
Kama huijui manual yako mwenyewe vipi uiulizie manual ya Mungu ?

Ewe mwenye busara,
kama huijui manual inayokuelezea wewe binafsi basi usiisumbukie ya Mungu ambaye hujawahi kumwona.

Ewe mwenye busara,
ni jambo la ajabu kama vitu dhaifu vina manual, lakini wewe mwenye nguvu na hekima huna manual inayoeleza ASILI na HATIMA yako.

Ewe mwenye busara,
Kama hujawahi kuiona na kuisoma manual yako.
Ni upumbavu uliopindukia kama utajidai eti unaiulizia manua ya Mungu.
(ashakum sio matusi ila ni kuelimishana tu)

Uwe mwenye busara, kuanzia leo jiite mjinga ili uaze kuiulizia manual yako na kujisoma mwenyewe na kujitambua.

Mimi nina busara na ninaijua manual yangu.

BIBLIA TAKATIFU ni manual yangu.
Inaeleza wazi jinsi nilivyotengenezwa, chakua nitakacho kula, masharti nitakayozingatia ili niishi vizuri, umri wa miaka nitakayo ishi, miiko na makatazo ninayopaswa kuyakwepa kufanya, nitakavyo owa mke na kuzaa watoto, nitakavyozeeka, nitakavyo kufa, nitakavyofufuka, nitakavyo enda mbinguni, na huko nitaishi milele nk.

Ewe mwenye busara,
Nani alikuruhusu ule chakula unachokula, maji unayokunywa, mavazi unayovaa, miaka unayoishi, dawa unazokunywa nk ?

Hatima yako ninini baada ya kuzeeka ?

Ivi kifo ndio mwisho wako na busara zako zote hizo ?

Ha..ha...ha..ha...

Niambie Ewe mwenye busara,
Kama huijui manual yako utaijuaje manual ya Mungu ?

Ewe mwenye busara,
Kumbe inaoneka wewe ni mpumbavu uliyepindukia.
Hata mwenyewe hujijui kumbe..!

Usikate tamaa anza kuitafuta manual yako kwanza, muda bado upo, nakuhakikishia utaiona.

Ewe mwenye busara, wacha upumbavu.

Ewe mpumbavu.
 
Je wajua kwamba kuna idadi kubwa ya watu wanaamini ukiwa ni mwenye zambi basi kaburini utakutana na nyoka, nge na adhabu yako inaanzia hapo.
Je wewe uko kwenye kundi lipi???
 
Siyo kwamba hakuna ushahidi wa uwepo wa Mungu bali hawataki tu kukubali hadharani kuwa Mungu yupo.....

Hawa wana ajenda yao.....
Thibitisha kama yupo
Nini kimekufanya uamini kama yupo?
 
acha stori, jibu maswali hapi juu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…