Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Author

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2014
Posts
1,745
Reaction score
8,230
Huwa kuna sababu mbalimbali ambazo humfanya mtu kutokupenda kuhudhuria ibada siku ya Jumamosi au Jumapili (kutokana na dhehebu).

Mimi sababu ilinifanya nisiwe nahudhuria kanisani ni pale mchungaji alipokuwa anahubiri kuhusu sadaka na matoleo tu kwa ibada tatu mfululizo.

Nini sababu yako?
 
Wachungaji matapeli kama Ngwajiboi..wachungaji kutafuna kondoo zao hadharani..mahubiri yasiyo na wokovu wala kukemea dhambi wao ni kupanda na kuvuna..wachungaji wasaka pesa..michango makanisani iliyokithiri we uliona wapi pipi kununuliwa kwa milioni kama sio kuongezeana umaskini.

Viongozi wa dini kutokemea na kushirikiana na wanasiasa wanafiki na wauaji.

Ila mahubiri ya mchungaji mgogo yananivutia sana hope nikianza kusali ntaaza kwenye kanisa analohubiria.

#MaendeleoHayanaChama
 
Ninyi endeleeni tu kutokwenda kanisani kwa amani, hakuna anayewahukumu, japokuwa naamini hapa yenyewe nafsi zenu zinawasuta ndiyo maana mnajifanya kutafuta justification tu ya matendo yenu hamna lolote..!
 
Carleen Ungekuwa muumini wa kanisa la Gwajiboy ungeendelea kwenda kanisani.. kwa sasa akiwa ni mchungaji/mwanasiasa. Ukijumuisha na swala la wazi lililotokea Kawe linalovunja amri ya 'Usiibe' na 'Usiseme uongo'....Kuna msemo unasema 'hauwezi kuwa mwanasiasa bila kusema uongo'
 
Viongozi wengi wa kiroho wametoka kwenye msingi mkuu wa imani, yaani kukemea maovu na kuhubiri juu ya pepo badala yake wamekuwa wasifia watawala na wasaka fedha kwa michango lukuki.
 
Ninyi endeleeni tu kutokwenda kanisani kwa amani, hakuna anayewahukumu, japokuwa naamini hapa yenyewe nafsi zenu zinawasuta ndiyo maana mnajifanya kutafuta justification tu ya matendo yenu hamna lolote..!
Wengi wanaenda kanisani kuogopa kutokuzikwa na kanisa either kwa wao wrnyewe watoto wao au ndugu..
Ukweli hauna dini.
 
Ibada inafanyika kokote penye utulivu... sadaka iliyo kamili ni ile unayo itoa kwa moyo...ata ukimtumia mdogo wako pocket money shule kwa moyo basi ni sadaka sio lazima kujengea mapadri ma castle while kwenu mnakula ugali na chumvi uo kingreza inaitwa

Burden
 

Ni kweli kabisa, “asiyewajali wa nyumbani mwake ni mbaya kuliko asiyeamini”... nimenukuu maandiko.
 
Ulitaka uhubiriwe nini mtoa mada? Hayo unayotaka kuhubiriwa una uhakika utayafuata? Ukiambiwa mpende jirani yako kama nafsi yako utafanya hivyo? Ukiambiwa uache wivu, masengenyo, uzinzi n.k utaacha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…