victormztz
JF-Expert Member
- Apr 6, 2015
- 1,111
- 614
Anayeota ccm kushinDA mwaka huu anajidanganya???
Wewe ndio unaota,tehetehe!
Anayeota ccm kushinDA mwaka huu anajidanganya???
nashangaa tu:
katika andiko lililokosa maana, umeweza kuliona goli la mkono?
Ni kweli huelewi kushindwa vibaya au hutaki kuamini.
kwa chadema iliyopata chini ya 30% ktk chaguzi zote zilizotangulia, ikipata 40% hapo haijashindwa vibaya, lkn ikipata 10% itakuwa imeshindwa vibaya.
Msomaji mzuri naye anatakiwa kumsoma muandishi kila eneo na sio kuchagua paragraphs zinazomvutia tu!
Fikara nzuri sana. Kuongezea kwenye uliyoandika; pia tusidharau mambo mawili ambayo hayaongelewi sana:
- Udhalilishwaji wa Dr. Slaa, Prof. Lipumba n.k.: Wapo wengi ambao wamekatishwa tamaa na hili tendo. Kwa hiyo baadhi ya wafuasi wao sio ajabu hawatampigia kura LOWASSA na sio ajabu wakaamua hata kumpigia kura Magufuli.
- Wapo wana UKAWA wengi ambao hawamtaki LOWASSA: Sababu yao ni moja tu, UFISADI wake ambao wameupiga vita kwa miaka mingi. Hawa sauti zao zimenyamazishwa na wale wenye midomo mikubwa, lakini nina uhakika wapo wengi. Kwa hawa, sio ajabu wanashiriki hata kwenye mikusanyiko ya UKAWA lakini wakiulizwa na TWAWEZA, wanamchagua mtu tofauti na Lowassa.
Mtaji wa siasa ni watu, mtaji huu huwa unakuwa mkubwa sana ikiwa watu hao watakuwa katika mazingira ya kufanya maamuzi kishabiki. Mara nyingi ushabiki huwa na matokeo mabaya kwenye siasa, tofauti na kwenye mipira au muziki kwani katika siasa baada ya mechi ndipo malipo ya ushabiki yanahitajika sana. Ni kupitia ushabiki ndipo umuhimu wa kampeni na kusikiliza sera unakuwa haupo kwasababu wanaotakiwa wasikilize sera, tayari washakuwa washabiki. Sera hazina maana tena.
Kwa bahati mbaya, mwaka huu uchaguzi umetawaliwa na ushabiki, kuzidi au sawa na ule wa 2005. Wanasiasa wa Tanzania wamejua kuwa Watanzania tunapenda kufanya mambo kwa kishabiki.
Kamwe tusiingie kwenye mtego wa ushabiki linapokuja suala la uchaguzi. Ushabiki tuuache majukwaa ya mpira na muziki. Hapa tuchague mtu aje atufanyie kazi tunayotaka ifanywe kwa takribani miongo kadhaa.
Inawezekana, epuka ushabiki.
Time is present and telling you something "now", you don't need to wait and see.Only time will tell lets wait and see after 25 October
mbatia jana kasema ONLINE wanaongoza sasa sijui inakuwa huko online maana mtu mmoja anaweza piga kura zaidi ya mara 30 . huo ndio MBATIA anaoukubali
Ndivyo ulivyokaririshwa? Kwani CCM hamna kazi nyingine za kufanya?
Kuna tafiti zinafanyika ofisini na kuna tafiti zinafanyika mitaani...
![]()
Watu waliojingia maofisini vs wanatembea mitaani...kazi kwenu!
Kweli mkuu, mie nilikuwa CDM na kadi yangu ni 0393395 lakini kuja kwa Lowassa kumenifanya kuondoka na nasubiri niwape kichapo cha mbwa ..mwaka huu ni bora CCM itawale milele kuliko marehemu kuingia Ikulu natuko wengiiii sanaaaaa
ukawa watashindwa maana wameisha shindwa kusimamia vinywa vyao kuwa lowasa fisadi serikali ya ccm iache kumlinda lowasa eti tunaushahidi tosha dhidi ya lowasa leo lowasa msafi hahaha wananchi wengi hawaelewi na wanawashangaa sana pia ndani ya ukawa wenyewe hususani chadema wengi hawatampigia lowasa kura maana hawajiridhika na ujio wake ndani ya chadema na ukawa