Kwanini tuna hofu na kifo?

Nov 2, 2023
60
50
Tukisia neno kifo huwa tunaingiwa na taharuki na kuchanganyikiwa kwa kuona mwisho wa mtu umefika. Embu tujiulize, kwanini tunahofu sana na kifo?. Ni kweli kifo ni kitu kibaya hivyo kwetu. Au ni kwasababu matendo yetu mengi mabaya sana haya endani na inavyopaswa tunahofia kitatokea nini kwetu. Pengine hatutaki kumaliza raha zetu tunazopata kwenye maisha tunataka tubaki nazo milele.

Kwa tafsiri zetu za kifo tunavyo sikia ni kama mwanzo wa mateso makubwa yasiyo na mfano, na jinsi tunavyoishi maisha yetu inaonyesha ni vigumu kuendana na matakwa ya kufikia sehemu salama hofu huanzia hapo ya kuogopa kifo. Ila hakuna aliye thibitisha kuwa tiketi ya kutenda mema itakusaidia wakati unaishi ama ukishamaliza kuonana na binadamu.

Na akili zetu hazipendi kuishi bila kujua mategemeo yajayo, kwa kuishi kwa akili tu kuwa na mashaka lazima tuogope. Akili zetu zinapenda uhakika wa usalama. Kinachotokea ni hatuelewi maana ya kifo, akili haijawahi kupata jibu kamili ndio maana ni kitendawili mpaka sasa. Je, inakuwaje kama kuna maisha zaidi ya tunachoweza kufikiri, tunaweza kuishi bila hofu ya kifo tunayo itengeneza?.

Tunakuwa na mahusiano mabaya na kifo kwakuwa tumekuwa waathirika wa akili zetu kimawazo. Akili zetu zinajihusisha sana na kuwa salama kwenye wakati kuliko kujihushisha na kinachoendelea muda uliopo chenye uhalisia. Kama tutashindwa kuwa makini na kuupa thamani wakati uliopo kwa kuushi kwa ufahamu zaidi kujitambua nnjee ya vikomo vya akili kwenye mawazo yetu na kubaki na uhalisia wa maisha tu basi tutaishi kwa furaha na amani yote na hatutohisi kama kifo ni kupoteza kitu kwetu.

Tuna mahusiano mabaya na kifo kwakuwa tumeshindwa kujitambua na tunaweka hofu ya kimawazo mbele. Kama uliweza kuwa na mwanzo basi na mwisho unakusubiri na sio jambo lakushangaza kwakuwa viumbe wote ndio mzunguko wetu. Ila ukiwa unataka kukipangana nalo kwa kutojitambua na wewe ni moja wapo wa mzunguko huu itakupashida.

NB: Kutojielewa kwako kwa kuishi kwenye vikomo vya akili kimawazo ndio vinakupashida ya hofu ya kifo. Chamuhimu ni kuishi vyema sasa kwa upendo, amani na furaha yote. Thamani ya maisha si kuwa marefu bali kwa muda wako umeyaishi vipi.
 
Nao wajumbe wakanena"kifo cha wengi ni harusi"

Hakiogopwi kifo, ila kutangulia mwenyewe na kuacha wanaokutegemea,marafiki,na kampany nyuma.

Ndio sababu vifo vya uzeeni, wengi hufa wakiwa wanatabasamu,maana wana uhakika na mazingira waliyoyaacha, wamewamiss waliowaacha wao,ni kama wakati sahihi wa kwenda kukutana nao kwa mara nyingine.
 
Ukitambua thamani ya uhai ulionao na kwanini unaishi duniani basi kamwe hautaogopa au kuhofia kifo au umauti.
 
Watu wanaogopa kifo maana hawana uhakika uhakikq wanaenda wapi baada ya kifo chao, mtu kama ni mwizi, mfisadi, mzinzi, mwasherati, anategemea waganga, muongo, nk! Mtu huyo lazima aogope kifo maana baada ya kifo chake ataenda kuchemka kwenye moto wa kuzimu!

Ufunuo wa Yohana 14:13
[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.



Waebrania 9:27
[27]Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;


Luka 16:22-31
[22]Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
[23]Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
[25]Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
[26]Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
[27]Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
[28]kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
[29]Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
[30]Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
[31]Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
 
Kifo sio inshu...inshu utakufaje...

Kwa mapanga
Kwa ajar
Maradhi
Ect......
 
Nao wajumbe wakanena"kifo cha wengi ni harusi"

Hakiogopwi kifo, ila kutangulia mwenyewe na kuacha wanaokutegemea,marafiki,na kampany nyuma.

Ndio sababu vifo vya uzeeni, wengi hufa wakiwa wanatabasamu,maana wana uhakika na mazingira waliyoyaacha, wamewamiss waliowaacha wao,ni kama wakati sahihi wa kwenda kukutana nao kwa mara nyingine.
Tatizo si unao wachaa kila mmoja kwanini kuhofia nafsi yake mwenyewe
 
Watu wanaogopa kifo maana hawana uhakika uhakikq wanaenda wapi baada ya kifo chao, mtu kama ni mwizi, mfisadi, mzinzi, mwasherati, anategemea waganga, muongo, nk! Mtu huyo lazima aogope kifo maana baada ya kifo chake ataenda kuchemka kwenye moto wa kuzimu!

Ufunuo wa Yohana 14:13
[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.



Waebrania 9:27
[27]Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;


Luka 16:22-31
[22]Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
[23]Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
[25]Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
[26]Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
[27]Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
[28]kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
[29]Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
[30]Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
[31]Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Ukitaka kuelewa uhalisia weka maneno yote pembeni na ungalie maisha kwa uhalisia wa macho yako na si kitu chochote kikae mbele yako.
 
Back
Top Bottom