Kwanini tukiugua hamu ya kula inapotea?

Kwanini tukiugua hamu ya kula inapotea?

tindikalikali

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2011
Posts
4,854
Reaction score
1,145
Hivi wadau kwanini magonjwa mengi katika mwili wa binadamu yanaambatana na kukosa hamu ya kula, kuanzia minyoo, malaria, typhoid na mengine!!

Je ni mwili unafanya hivyo kujihami na vijidudu vya magonjwa au hivyo vijidudu ndiyo vinasababisha!?

Na ni kipi cha kufanya ili ule kama kawaida ukiwa mgonjwa!!
 
Chakushangaza mimi hamu huwa haziniishi nakula kama kawaida
 
Hivi wadau kwanini magonjwa mengi katika mwili wa binadamu yanaambatana na kukosa hamu ya kula, kuanzia minyoo, malaria, typhoid na mengine!!

Je ni mwili unafanya hivyo kujihami na vijidudu vya magonjwa au hivyo vijidudu ndiyo vinasababisha!?

Na ni kipi cha kufanya ili ule kama kawaida ukiwa mgonjwa!!



ukiwa na vijidudu kwenye mwili (infection), mwili unatengeneza chemicals (cytokines) kwenye sehemu ya hiyo infection...hizi cytokines sana sana interlukin 1 na tumor necrosis factor kazi yake kubwa ni kuelekeza seli za kinga za mwili sehemu infection ilipo ilikuzui na kuua hivyo vijidudu!

sasa hizi chemicals ukiacha kazi yake muhimu niliyotaja hapo juu, hua zinaenda kwenye ubongo kwa njia ya damu kwenye sehemu muhimu sana inaitwa hypothalamus

hypothalamus inahusika na kucontrol joto (temperature center) , kucontrol ulaji (satiety center) na kazi nyingine nyingi

zikifika kule zinavuruga mambo, na ni kwa manufaa ya mwili, mfano kitu cha kwanza kitafanya ni kushusha joto la mwili ambalo mwili umezoea, kwahiyo mtu atajihisi homa, nadhani hii inamanufaa kwasababu joto lina wapa vijidudu mazingira ya kukua na kuongezeka so mwili unaamua kushusha ilikuzuia hii


then itavuruga ulaji wa mtu, na utakua unajihisi kutokula , kama unavyojua kwamba vijidudu nao wanahitaji virutubisho kutoka kwenye chakula, mfano madini ya chuma ili waweze kukua na kuongezeka, kwahio mwili unajaribu kuzuia hilo
 
Mdau hapo juu kaelezea mtiririko wa kikemikali unavyotokea mwilini pindi mtu anapopata homa...

Sasa turudi katika swali lako la msingi...

Je ni mwili unafanya hivyo kujihami na vijidudu vya magonjwa au hivyo vijidudu ndiyo vinasababisha!?

Mtu mwenye homa huwa anapoteza hamu ya kula kwa sababu kupoteza hamu ya kula ni mbinu mojawapo ya uhifadhi nishati mwilini...

Kupoteza hamu ya kula maana yake mwili hautumii tena nishati kubwa ambayo hutumika wakati wa kumeng'enya chakula...

Sasa hii ni msaada kwa mwili kwa sababu kile kiasi cha nishati kilichotakiwa kumeng'enya chakula kinaelekezwa katika kupambana na ugonjwa...

Ukiacha hilo kuna baadhi ya magonjwa kama mafua huwa yanatibua mfumo wa hewa/kunusa...

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kunusa na kuonja. Hali ya unusaji inapopotea hata hamu ya kula nayo hupungua...

Na ni kipi cha kufanya ili ule kama kawaida ukiwa mgonjwa!!

Huwa inashauriwa ule vyakula vyepesi vyepesi kama supu, uji au vyakula vilivyopondwa au vikavu mathalani mkate...

Mtu anapozidiwa zaidi hupigwa dripu yenye chakula ndani yake...
 
Mdau hapo juu kaelezea mtiririko wa kikemikali unavyotokea mwilini pindi mtu anapopata homa...

Sasa turudi katika swali lako la msingi...



Mtu mwenye homa huwa anapoteza hamu ya kula kwa sababu kupoteza hamu ya kula ni mbinu mojawapo ya uhifadhi nishati mwilini...

Kupoteza hamu ya kula maana yake mwili hautumii tena nishati kubwa ambayo hutumika wakati wa kumeng'enya chakula...

Sasa hii ni msaada kwa mwili kwa sababu kile kiasi cha nishati kilichotakiwa kumeng'enya chakula kinaelekezwa katika kupambana na ugonjwa...

Ukiacha hilo kuna baadhi ya magonjwa kama mafua huwa yanatibua mfumo wa hewa/kunusa...

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kunusa na kuonja. Hali ya unusaji inapopotea hata hamu ya kula nayo hupungua...



Huwa inashauriwa ule vyakula vyepesi vyepesi kama supu, uji au vyakula vilivyopondwa au vikavu mathalani mkate...

Mtu anapozidiwa zaidi hupigwa dripu yenye chakula ndani yake...

Asante mkuu kwa ufafanuzi mzuri!!
 
Mdau hapo juu kaelezea mtiririko wa kikemikali unavyotokea mwilini pindi mtu anapopata homa...

Sasa turudi katika swali lako la msingi...



Mtu mwenye homa huwa anapoteza hamu ya kula kwa sababu kupoteza hamu ya kula ni mbinu mojawapo ya uhifadhi nishati mwilini...

Kupoteza hamu ya kula maana yake mwili hautumii tena nishati kubwa ambayo hutumika wakati wa kumeng'enya chakula...

Sasa hii ni msaada kwa mwili kwa sababu kile kiasi cha nishati kilichotakiwa kumeng'enya chakula kinaelekezwa katika kupambana na ugonjwa...

Ukiacha hilo kuna baadhi ya magonjwa kama mafua huwa yanatibua mfumo wa hewa/kunusa...

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kunusa na kuonja. Hali ya unusaji inapopotea hata hamu ya kula nayo hupungua...



Huwa inashauriwa ule vyakula vyepesi vyepesi kama supu, uji au vyakula vilivyopondwa au vikavu mathalani mkate...

Mtu anapozidiwa zaidi hupigwa dripu yenye chakula ndani yake...
asante sana mkuu yaani nimetafuta uzi kama huu leo ni siku ya nne namaliza sili kabisa vile inavyotakiwa ni nalalia maembe na mananasi, juicy n.k ndio nàsikia vinaradha na vinamezeka.
 
Back
Top Bottom