Kwanini Tanzania hatuna Airline?

Kwanini Tanzania hatuna Airline?

KakaKiiza

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2010
Posts
11,902
Reaction score
9,323
Hivi hakuna Watanzanaia wanaoweza kuendesha Shirika la ndege la Tanzania? Ina maana hakuna wachumi wa utawala wa biashara?

Kwa nini Tanzania hatuna Airline?
 
Hatujashindwa kuwa na Airline, ila kuna wajanja wananufaika na kutokuwa na shirika la ndege.
 
Wewe unauliza airline hali hata dawa za binadamu tunashindwa kutengeneza.kila kitu cha nje.uliza ccm ndiyo inataka tuishi hivi.dawa wanaleta wahindi.
 
Hatuzitaki maana sio twiga tu watapanda humo sasa hadi na sungura na mamba!
 
Saba fisadi ameshaondoka basi tutaanza binafsisha kwanza ndege yake

IMG_20150818_161728.jpg IMG_20150818_160251.jpg
 
Nothing can be the pride of CCM in Tanzania for about 54 years, but only begging and scandals
 
Hatujashindwa kuwa na Airline, ila kuna wajanja wananufaika na kutokuwa na shirika la ndege.

Watanzania tulio wengi tunataka mabadiliko haya yote yalipaswa kufanywa na serikali ya chama cha Mapinduzi wameshindwa kwa miaka hamsini!!hakuna wimbo watakaopiga tuuelewe tumechoka na ahadi hewa
 
WaTz wengi husafiria ticket za "'infant fare" au "LPO" hata "Ticket FEKI"sasa Airline itasavaivu vipi? Kweli inauma kwa kutokuwa na shirika la ndege Maarufu!!!
 
Ni kwasababu ya CCM na kuliua Azimio la Arusha, mgongano wa maslahi........ Waziri anahisa za kufa mtu PW na FN unategemea Tanzanair itasimama?
 
airlines zilizopo zinatosha,mkulima wa kijijini kipaumbele chake sio airline
 
Mbona umeenda mbali sana , anza na shirika la reli halafu ulizia shirika la ndege,mabehewa mitumba , kivuko kilichonunuliwa eti cha usafiri Dar to Bagamoyo sub standard , Wahusika unawajua Magufuli na Mwakyembe .Hivi leo wanapanda majukwaani na kumsema Lowassa .
Ni aibu kubwa sana kukosa shirika la ndege na reli
 
Umeuliza jambo nyeti sana....ukizingatia ukanda huu ni wa utaliii, KQ na mashirika mengine wanachukua nafasi yetu na kuwanufaisha sana tena sana.
wataalamu tunao, uwezo tunao, na wezi tunao, Vilevile Serikali ya CCM iliuwa ATC,kwa mfano viongozi walikuwa wanapandisha mpaka mademu wao bure kwenda sehemu mbalimbali enzi hizo za boeing 737 serengeti na kilimanjaro.
Inauma aisee,inauma asikuambie mtu.Daaah Rest in Peace Five Hotel....
 
Tuna kandege kamoja ka kukodi na wafanyakazi mia mbili. Yaani ndege ya kubeba abiria sitini inahudumiwa na jumla ya wafanyakazi mia mbili, kuanzia wa ofisini mpaka on board.
 
Kama umeshindwa kuwadhibiti wajanja ndio umeshindwa hivyo .Tatizo kubwa wanakodi ndege lakini maslahi yao kwanza
 
airlines zilizopo zinatosha,mkulima wa kijijini kipaumbele chake sio airline

Mawazo mgando. unafikiri huyo mkulima ni lazima apande hiyo ndege ndio aone au apate faida zake?! bei ya vitu tu mfano pembejeo za kilimo na dawa za binadamu inategemea tena sana uwepo au kutokuwepo kwa shirika la ndege la Taifa lenye tija.akili zako zimekaa kiccm ccm kweli.
 
Wanaoangusha nchi hii tangu enzi za mwalimu ni wasomi na wafanyabiashara,alafu kundi la pili ni wakulima na wafugaji hawa hawabadiliki haraka kifikra na ubunifu kama wanavyotakiwa.Hakuna siku CCM imewahi tunga sera mbovu bali makundi hayo hapo juu na ndio wananchi wanaboronga.
 
Back
Top Bottom