Kwanini serikali ya Tanzania haikuishtaki Acacia Mining Plc kwa makosa ya uhujumu uchumi ikiwa haina leseni?

gemmanuel265

JF-Expert Member
Feb 16, 2016
8,485
18,045
Kwa mujibu wa ripoti ya kamati maalum ya kuchunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusiana na mchanga wa madini unaosafirishwa nje ya nchi iliyoongozwa na Prof. Nehemiah Eliakim Osoro, ilibaini na kuthibitisha kwa mujibu wa nyaraka na maelezo kutoka ofisi ya Msajili wa Makampuni (BRELA) kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc haikusajiliwa (incorporation) nchini Tanzania na wala haina hati ya utambuzi (certificate of compliance) kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni, sura ya 212.

Kamati pia ilibaini kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc, ambayo inajinasibisha kuwa mmiliki wa Makampuni ya Bulyanhulu Gold Mines Ltd, North Mara Gold Mine Ltd na Pangea Minerals Ltd, haikuwahi kuwasilisha nyaraka wala taarifa yoyote kuonesha kuwa kampuni hiyo ni mmiliki wa Makampuni hayo wala kuwa na hisa katika Makampuni hayo. Kwa kuwa Acacia Mining Plc haina usajili wala utambuzi wa kisheria nchini, hivyo haina sifa ya kupata leseni, kuchimba wala kufanya biashara ya madini nchini Tanzania.

Hivyo basi, kamati ilibaini kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc, inafanya biashara ya madini nchini kinyume cha sheria za nchi.

Kamati hiyo pamoja na kubaini kuwa Acacia haina usajili kwa Msajili wa Makampuni (BRELA), pia imetenda makosa mbali mbali ya kijinai yakiwemo ya ukwepaji wa kodi, kutoa taarifa za uongo, kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu, uhujumu uchumi na kulisababishia taifa hasara kinyume cha:

i. Vifungu vya 18, 114 na 115 vya sheria ya madini, 2010

ii. Vifungu vya 101 na 106 vya sheria ya kodi ya mapato, 204

iii. Vifungu vya 79 na 82 vya sheria ya usimamizi wa kodi, 2015

iv. Kifungu cha 24 cha sheria ya uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini Tanzania, 2015

v. Kifungu cha 27 cha makosa ya uhujumu uchumi sura ya 200 na

vi. Kifungu cha 203 cha sheria ya usimamizi wa forodha ya jumuiya ya Afrika Mashariki, 204

Lakini pamoja na kamati kubaini makosa hayo kisheria sijawahi kusikia wala kuona serikali ikipeleka shauri mahamani ili kuifungulia kesi ya jinai ya uhujumu uchumi kampuni ya Acacia Mining Plc, na kinyume chake Barrik Gold Mines Ltd walipokwenda kufanya mazungumzo Mh Rais Ikulu, Rais aliwaita wanaume badala ya kutiwa korokoroni kwa kulisababishia taifa hasara kubwa.

Naona hii dhana ya kupambana na ufisadi ina macho, maeneo mengine inakwepa kuchukua hatua za kisheria inabaki kupambana na wazalendo wa nchi hii kwa sababu ya chuki au utofauti wa kiitikadi jambo ambalo mapambano haya hayawezi kufanikiwa pasipo umoja wetu kama taifa, tufanya mambo kwa misingi ya kisheria na siyo kwa mihemko na mbwembwe za kisiasa kwa kutaka huruma za wananchi.
 
Kwa mujibu wa ripoti ya kamati maalum ya kuchunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusiana na mchanga wa madini unaosafirishwa nje ya nchi iliyoongozwa na Prof. Nehemiah Eliakim Osoro, ilibaini na kuthibitisha kwa mujibu wa nyaraka na maelezo kutoka ofisi ya Msajili wa Makampuni (BRELA) kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc haikusajiliwa (incorporation) nchini Tanzania na wala haina hati ya utambuzi (certificate of compliance) kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni, sura ya 212.

Kamati pia ilibaini kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc, ambayo inajinasibisha kuwa mmiliki wa Makampuni ya Bulyanhulu Gold Mines Ltd, North Mara Gold Mine Ltd na Pangea Minerals Ltd, haikuwahi kuwasilisha nyaraka wala taarifa yoyote kuonesha kuwa kampuni hiyo ni mmiliki wa Makampuni hayo wala kuwa na hisa katika Makampuni hayo. Kwa kuwa Acacia Mining Plc haina usajili wala utambuzi wa kisheria nchini, hivyo haina sifa ya kupata leseni, kuchimba wala kufanya biashara ya madini nchini Tanzania.

Hivyo basi, kamati ilibaini kuwa kampuni ya Acacia Mining Plc, inafanya biashara ya madini nchini kinyume cha sheria za nchi.

Kamati hiyo pamoja na kubaini kuwa Acacia haina usajili kwa Msajili wa Makampuni (BRELA), pia imetenda makosa mbali mbali ya kijinai yakiwemo ya ukwepaji wa kodi, kutoa taarifa za uongo, kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu, uhujumu uchumi na kulisababishia taifa hasara kinyume cha:

i. Vifungu vya 18, 114 na 115 vya sheria ya madini, 2010

ii. Vifungu vya 101 na 106 vya sheria ya kodi ya mapato, 204

iii. Vifungu vya 79 na 82 vya sheria ya usimamizi wa kodi, 2015

iv. Kifungu cha 24 cha sheria ya uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini Tanzania, 2015

v. Kifungu cha 27 cha makosa ya uhujumu uchumi sura ya 200 na

vi. Kifungu cha 203 cha sheria ya usimamizi wa forodha ya jumuiya ya Afrika Mashariki, 204

Lakini pamoja na kamati kubaini makosa hayo kisheria sijawahi kusikia wala kuona serikali ikipeleka shauri mahamani ili kuifungulia kesi ya jinai ya uhujumu uchumi kampuni ya Acacia Mining Plc, na kinyume chake Barrik Gold Mines Ltd walipokwenda kufanya mazungumzo Mh Rais Ikulu, Rais aliwaita wanaume badala ya kutiwa korokoroni kwa kulisababishia taifa hasara kubwa.

Naona hii dhana ya kupambana na ufisadi ina macho, maeneo mengine inakwepa kuchukua hatua za kisheria inabaki kupambana na wazalendo wa nchi hii kwa sababu ya chuki au utofauti wa kiitikadi jambo ambalo mapambano haya hayawezi kufanikiwa pasipo umoja wetu kama taifa, tufanya mambo kwa misingi ya kisheria na siyo kwa mihemko na mbwembwe za kisiasa kwa kutaka huruma za wananchi.
bandiko hili naomba alione mh. Tundu Lisu ili akipona hapo ndo pa kuanzia, kuwakosao wale wazalendo wasiopenda kukosolewa
 
Raisi wa tifu tifu alishasema kuwa ana furasituasheni zake ndio maana huwa anaongeaga tu!! Rejea ziara yake bandarini aliyokwenda kuokota magari yasiyo na mwenyewe baadala ya kuokota pia mabehewa ya treni yenye nembo ya TRL sasa sijui ni nani mwingine Tanzania mwenye barabara ya reli!!!
 
Mwisho wa ubaya siku zote ni aibu. Muda si mrefu atajulikana nani mkweli kati ya Mh Lissu na Bw Yule.
Lissu alisimama peke yake taifa zima mbele ya vyombo vya habari kusema wazi kabisa kuwa zile ripoti zilikuwa takataka kabisa zilizotengenezwa kwa ajili ya kumchekesha mfalme, Zitto nakumbuka alisapoti zile ripoti na kuungana na wasifia wa kila kitu cha mfalme, Lissu alizisoma zile ripoti kwa jicho la kisheria na kuona hazina jipya
 
Lissu alisimama peke yake taifa zima mbele ya vyombo vya habari kusema wazi kabisa kuwa zile ripoti zilikuwa takataka kabisa zilizotengenezwa kwa ajili ya kumchekesha mfalme, Zitto nakumbuka alisapoti zile ripoti na kuungana na wasifia wa kila kitu cha mfalme, Lissu alizisoma zile ripoti kwa jicho la kisheria na kuona hazina jipya
Ni kweli kabisa Mkuu. Ukweli utabaki kuwa kweli. Wale wote waliokuwa wakishangilia na hata kutoa maneno ya kejeli kwa Mh Lissu hivi sasa wamebaki na aibu. Mh Lissu yuko hosp sio kwa kupatata ajali wala ugonjwa bali ni kwa mapenzi ya watu wachache wanaojidai wao ni wazalendo na Lissu msaliti.

Hadi sasa makinikia iko bandarini na hatma yake ni Mungu anajua ktk kunusuru taifa lisitumbukie kwenye dimbwi la fidia. Nisingependa tufike huko kwani ni mimi na wewe tutakaoumia kama si pamoja na watoto wetu wakati walitusbabishia majanga wakila mema ya nchi na familia zao.
 
Ni kweli kabisa Mkuu. Ukweli utabaki kuwa kweli. Wale wote waliokuwa wakishangilia na hata kutoa maneno ya kejeli kwa Mh Lissu hivi sasa wamebaki na aibu. Mh Lissu yuko hosp sio kwa kupatata ajali wala ugonjwa bali ni kwa mapenzi ya watu wachache wanaojidai wao ni wazalendo na Lissu msaliti.

Hadi sasa makinikia iko bandarini na hatma yake ni Mungu anajua ktk kunusuru taifa lisitumbukie kwenye dimbwi la fidia. Nisingependa tufike huko kwani ni mimi na wewe tutakaoumia kama si pamoja na watoto wetu wakati walitusbabishia majanga wakila mema ya nchi na familia zao.
Well said mkuu!
 
Mungu ni mwema sana kwake na alimwokoa Lissu sio kwa bahati mbaya bali tujifunze kuyatazama mambo kwa macho ya rohoni zaidi kuliko kuhemkwa!
Ni aibu ya kufungia mwaka kwa wale wote waliohusika kumuumiza ili kulazimisha uongo wao uwe ukweli! Vipi AG yupo likizoni? Mbona hajasema lolote juu ya Acacia?
 
Mungu ni mwema sana kwake na alimwokoa Lissu sio kwa bahati mbaya bali tujifunze kuyatazama mambo kwa macho ya rohoni zaidi kuliko kuhemkwa!
Ni aibu ya kufungia mwaka kwa wale wote waliohusika kumuumiza ili kulazimisha uongo wao uwe ukweli! Vipi AG yupo likizoni? Mbona hajasema lolote juu ya Acacia?
AG ndio hao wampotoshao rais ili kulinda nyadhifa zao za kazi, na ukizingatia Mh rais ile kauli ya Mkwere kuwa 'ukiambiwa jambo changanya na zako' haifanyii kazi hata kidogo
 
Back
Top Bottom